Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis

Numri i faqes:close

external-link copy
127 : 2

وَإِذۡ يَرۡفَعُ إِبۡرَٰهِـۧمُ ٱلۡقَوَاعِدَ مِنَ ٱلۡبَيۡتِ وَإِسۡمَٰعِيلُ رَبَّنَا تَقَبَّلۡ مِنَّآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na Kumbuka, ewe Nabii, wakati Ibrāhīm na Ismāīl walipoinua misingi ya Alkaba, huku wakimuomba Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu, “Ewe Mola wetu! Tutakabalie amali zetu njema na dua zetu! Kwani wewe Ndiye mwenye kusikia maneno ya waja wako, Ndiye mwenye kujua hali zao. info
التفاسير:

external-link copy
128 : 2

رَبَّنَا وَٱجۡعَلۡنَا مُسۡلِمَيۡنِ لَكَ وَمِن ذُرِّيَّتِنَآ أُمَّةٗ مُّسۡلِمَةٗ لَّكَ وَأَرِنَا مَنَاسِكَنَا وَتُبۡ عَلَيۡنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ

“Ewe Mola wetu, na utujaalie, sisi wawili, ni wenye kusimama imara juu ya Uislamu, ni wenye kukufuata kwa Imani. Utuonyeshe njia za kukuabudu. Utusamehe madhambi yetu. Hakika Wewe Ndiye Mwingi wa kukubali toba za waja wako, Ndiye mkunjufu wa rehema kwao. info
التفاسير:

external-link copy
129 : 2

رَبَّنَا وَٱبۡعَثۡ فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡهُمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَيُزَكِّيهِمۡۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

“Ewe Mola wetu, mtumilize katika ummah huu mjumbe miongoni mwa watu wa kizazi cha Ismāīl, awasomee aya Zako na awafundishe Kitabu na Sunnah, awasafishe na ushirikina na tabia mbaya. Hakika Wewe Ndiye Mshindi asiyeshindwa na kitu, Ndiye Mwenye hekima Anayeviweka vitu vyote mahali pake.” info
التفاسير:

external-link copy
130 : 2

وَمَن يَرۡغَبُ عَن مِّلَّةِ إِبۡرَٰهِـۧمَ إِلَّا مَن سَفِهَ نَفۡسَهُۥۚ وَلَقَدِ ٱصۡطَفَيۡنَٰهُ فِي ٱلدُّنۡيَاۖ وَإِنَّهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ لَمِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Hakuna yoyote anayeipa mgongo Dini ya Ibrahim, nayo ni Uislamu, isipokuwa safihi aliye mjinga. Na hakika tulimchagua Ibrahim duniani kuwa Nabii na Mtume, na kesho Akhera kuwa ni miongoni mwa watu wema ambao wana daraja za juu kabisa. info
التفاسير:

external-link copy
131 : 2

إِذۡ قَالَ لَهُۥ رَبُّهُۥٓ أَسۡلِمۡۖ قَالَ أَسۡلَمۡتُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na sababu ya kuchaguliwa kwake huku ni kukimbilia kwake kwenye Uislamu bila kusita. Alipoambiwa na Mola wake, “Itakase nafsi yako kwa Mwenyezi Mungu kwa kujisalimisha Kwake.» alikubali Ibrāhīm na kusema, “Nimejisalimisha kwa Mola wa viumbe vyote, kwa kumtakasa, kumpwekesha, kumpenda na kurudi Kwake kwa kutubia.” info
التفاسير:

external-link copy
132 : 2

وَوَصَّىٰ بِهَآ إِبۡرَٰهِـۧمُ بَنِيهِ وَيَعۡقُوبُ يَٰبَنِيَّ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰ لَكُمُ ٱلدِّينَ فَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسۡلِمُونَ

Na Ibrāhīm na Ya’qūb waliwahimiza watoto wao kusimama imara juu ya Uislamu wakiwaambia, “Enyi watoto wetu! Mwenyezi Mungu Amewachagulia Dini hii, nayo ni Uislamu, Msiiache muda wa uhai wenu, na msifikiwe na mauti isipokuwa na nyinyi muko kwenye Dini hii.” info
التفاسير:

external-link copy
133 : 2

أَمۡ كُنتُمۡ شُهَدَآءَ إِذۡ حَضَرَ يَعۡقُوبَ ٱلۡمَوۡتُ إِذۡ قَالَ لِبَنِيهِ مَا تَعۡبُدُونَ مِنۢ بَعۡدِيۖ قَالُواْ نَعۡبُدُ إِلَٰهَكَ وَإِلَٰهَ ءَابَآئِكَ إِبۡرَٰهِـۧمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ إِلَٰهٗا وَٰحِدٗا وَنَحۡنُ لَهُۥ مُسۡلِمُونَ

Je mlikuwa muko, enyi Mayahudi, pindi kifo kilipomjia Ya’qūb, alipowakusanya watoto wake na kuwauliza, “Mtaabudu nini baada ya kufa kwangu?” Wakasema, “Tutamuabudu Mola wako na Mola wa baba zako: Ibrāhīm, Ismā'īl na Is’ḥāq Ambaye ni Mola Mmoja; na sisi ni wenye kufuata amri Yake na kumdhalilikia.” info
التفاسير:

external-link copy
134 : 2

تِلۡكَ أُمَّةٞ قَدۡ خَلَتۡۖ لَهَا مَا كَسَبَتۡ وَلَكُم مَّا كَسَبۡتُمۡۖ وَلَا تُسۡـَٔلُونَ عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Hao ni Ummah waliopita miongoni mwa wale waliowatangulia nyinyi. Wao wana amali zao, na nyinyi muna amali zenu. Wala hamtaulizwa kuhusu amali zao. Na wao hawataulizwa kuhusu amali zenu. Na kila mmoja atalipwa kulingana na aliyoyatenda. Mtu hateswi kwa kosa la yoyote mwengine. Na haimnufaishi mtu ila Imani yake na uchaji Mungu wake. info
التفاسير: