Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis

Numri i faqes:close

external-link copy
94 : 2

قُلۡ إِن كَانَتۡ لَكُمُ ٱلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ عِندَ ٱللَّهِ خَالِصَةٗ مِّن دُونِ ٱلنَّاسِ فَتَمَنَّوُاْ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia Mayahudi ambao wanadai kuwa Pepo ni yao peke yao, kwa kudai kuwa wao tu, bila watu wengine, ndio mawalii wa Mwenyezi Mungu na kuwa wao ni watoto Wake na vipenzi Vyake, “Mambo yakiwa ni hivyo, waapizeni kufa waliyo warongo katika nyinyi au wasiokuwa katika nyinyi, iwapo nyinyi ni wakweli katika madai yenu haya.” info
التفاسير:

external-link copy
95 : 2

وَلَن يَتَمَنَّوۡهُ أَبَدَۢا بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيهِمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّٰلِمِينَ

Na hawatalifanya hilo kabisa, kwa wanayoyajua ya ukweli wa Nabii Muhammad, rehema na amani zimshukie, na ya urongo na uzushi wao, na kwa ukafiri na uasi walioufanya unaopelekea kukoseshwa Pepo na kuingia Motoni. Na Mwenyezi Mungu Anawajua madhalimu miongoni mwa waja wake na Atawalipa kwa dhulma zao. info
التفاسير:

external-link copy
96 : 2

وَلَتَجِدَنَّهُمۡ أَحۡرَصَ ٱلنَّاسِ عَلَىٰ حَيَوٰةٖ وَمِنَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْۚ يَوَدُّ أَحَدُهُمۡ لَوۡ يُعَمَّرُ أَلۡفَ سَنَةٖ وَمَا هُوَ بِمُزَحۡزِحِهِۦ مِنَ ٱلۡعَذَابِ أَن يُعَمَّرَۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na utajua tena utajua, ewe Mtume, kuwa Mayahudi ni wenye kupenda mno, miongoni mwa watu, maisha marefu, hata yawe ni maisha ya unyonge na udhalilifu namna gani. Kupenda kwao maisha marefu kunazidi vile washirikina wanavyoyapenda. Myahudi anatamani lau ataishi miaka elfu moja. Na umri huo, lau aufikia, hautamwepusha na adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, hakuna kitu chochote chenye kufichika Kwake katika matendo yao, na Atawalipa, kwa hiyo matendo yao, adhabu wanayostahiki. info
التفاسير:

external-link copy
97 : 2

قُلۡ مَن كَانَ عَدُوّٗا لِّـجِبۡرِيلَ فَإِنَّهُۥ نَزَّلَهُۥ عَلَىٰ قَلۡبِكَ بِإِذۡنِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَهُدٗى وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia Mayahudi waliposema, “Jibrili ni adui yetu miongoni mwa Malaika.”: “Mwenye kuwa ni adui wa Jibrili, basi ajue kuwa yeye ameiteremsha Qur’ani na kuitia ndani ya moyo wako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, ikiwa ni yenye kuvisadikisha vitabu vya Mwenyezi Mungu vilivyoitangulia, yenye kuongoza kwenye njia ya haki na yenye kuwapa wenye kuamini bishara ya kila wema wa dunia na Akhera.” info
التفاسير:

external-link copy
98 : 2

مَن كَانَ عَدُوّٗا لِّلَّهِ وَمَلَٰٓئِكَتِهِۦ وَرُسُلِهِۦ وَجِبۡرِيلَ وَمِيكَىٰلَ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَدُوّٞ لِّلۡكَٰفِرِينَ

Mwenye kumfanyia uadui Mwenyezi Mungu, Malaika Wake, Wajumbe Wake ambao ni Malaika au binadamu, hasahasa Malaika wawili: Jibrili na Mikaili, huwa amemfanyia uadui Mwenyezi Mungu. Sababu Mayahudi walidai kwamba Jibrili ni adui wao na Mikaili ni rafiki yao. Mwenyezi Mungu Akawajulisha kwamba mwenye kuwa adui wa mmoja katika wao huwa ni adui wa Mwengine na pia ni adui wa Mwenyezi Mungu. Kwani Mwenyezi Mungu ni adui wa wenye kuyakanusha yale aliyoyateremsha kwa Mtume wake Muhammad, rehema na amani zimshukie. info
التفاسير:

external-link copy
99 : 2

وَلَقَدۡ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ءَايَٰتِۭ بَيِّنَٰتٖۖ وَمَا يَكۡفُرُ بِهَآ إِلَّا ٱلۡفَٰسِقُونَ

Hakika tulikuteremshia aya zilizo wazi, zinazoonyesha kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kikweli; na hawazikanushi aya hizo isipokuwa wenye kutoka nje ya Dini ya Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
100 : 2

أَوَكُلَّمَا عَٰهَدُواْ عَهۡدٗا نَّبَذَهُۥ فَرِيقٞ مِّنۡهُمۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Ni ubaya ulioje wa hali ya Wana wa Isrāīl katika kuvunja kwao ahadi! Kila wanapotoa ahadi, kinatoka kikundi cha watu katika wao wakaitupa na wakaivunja. Utawaona wanaifunga ahadi leo na kuitangua kesho. Bali wengi wao hawayaamini aliyokuja nayo Nabii wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake Muhammad, rehema na amani zimshukiye yeye. info
التفاسير:

external-link copy
101 : 2

وَلَمَّا جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٞ لِّمَا مَعَهُمۡ نَبَذَ فَرِيقٞ مِّنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ كِتَٰبَ ٱللَّهِ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ كَأَنَّهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na alipowajia Muhammad, rehema na amani zimshukie, na Qur’ani inayoafikiana na Taurati waliyonayo, kilitoka kikundi cha watu katika wao wakakitupa kitabu cha Mwenyezi Mungu, na kukiweka nyuma ya migongo yao. Hali yao ni hali ya wajinga wasiojua uhakika wake. info
التفاسير: