《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼

页码:close

external-link copy
187 : 3

وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ لَتُبَيِّنُنَّهُۥ لِلنَّاسِ وَلَا تَكۡتُمُونَهُۥ فَنَبَذُوهُ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ وَٱشۡتَرَوۡاْ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلٗاۖ فَبِئۡسَ مَا يَشۡتَرُونَ

Na pale Mwenyezi Mungu alipo fungamana na walio pewa Kitabu kuwa: Lazima mtawabainishia watu, wala hamtokificha, walikitupa nyuma ya migongo yao, na wakanunua kwacho thamani duni. Basi ni kiovu hicho walicho nunua. info

Ewe Nabii! Kumbuka na utaje pale Mwenyezi Mungu alipo chukua ahadi madhbuti kwa Watu wa Kitabu, kuwa wayaeleze wazi maana ya Kitabu chao, na wala wasiwafiche watu chochote, na wao wakakitupilia mbali nyuma ya migongo yao, na badala yake wakatafuta starehe za dunia. Na starehe za dunia kama zitakavyo kuwa ni kitu chenye thamani duni kabisa kulinganisha na uwongofu na uwongozi. Ama wamejua kutenda uovu! (Hayo yalikuwa zamani na bado yanaendelea. Kuficha na kugeuza na kupotosha Biblia hakusiti. Vipo vitabu vyao vinavyo itwa "Apokrifa", maana yake "Vilivyo fichwa", kwa kuwa hivyo ni marfuku visisomwe ila na mapadri tu, na vingine vimeteketezwa. Miongoni mwa hivyo ni Injili ya Barnaba.)

التفاسير:

external-link copy
188 : 3

لَا تَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ يَفۡرَحُونَ بِمَآ أَتَواْ وَّيُحِبُّونَ أَن يُحۡمَدُواْ بِمَا لَمۡ يَفۡعَلُواْ فَلَا تَحۡسَبَنَّهُم بِمَفَازَةٖ مِّنَ ٱلۡعَذَابِۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Usiwadhanie kabisa wale wanao furahia waliyo yafanya, na wakapenda kusifiwa kwa wasiyo yatenda, usiwadhanie kuwa watasalimika na adhabu. Yao wao ni adhabu chungu. info

Usiwadhanie kabisa kuwa wataepuka adhabu wale wanao tenda maovu, na wakapenda kusifiwa kwa wasilo lifanya. Shani yao hao ni kujifungia mlango wa Imani na Haki, kama Mayahudi. Nao watapata adhabu chungu Siku ya Kiyama.

التفاسير:

external-link copy
189 : 3

وَلِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Na Ufalme wa Mbingu na Ardhi ni wa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza juu ya kila kitu. info

Mwenyezi Mungu pekee ndiye Mwenye mamlaka ya kila jambo la Mbinguni na duniani. Naye ni Muweza wa kila kitu. Atawashika wenye dhambi kwa dhambi zao, na atawalipa thawabu watendao mema kwa wema wao.

التفاسير:

external-link copy
190 : 3

إِنَّ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱخۡتِلَٰفِ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ لَأٓيَٰتٖ لِّأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili. info

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na viliomo ndani yao kwa vile vilivyo umbwa tangu mwanzo na mipango yake, na kukhitalifiana usiku na mchana kwa mwangaza na giza, kwa urefu wake na ufupi, zipo dalili na ishara zilizo wazi kwa watu wenye akili na kutambua za kuthibitisha Umoja wa Mwenyezi Mungu na Uwezo wake. "Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na mchana ziko ishara kwa wenye akili" - Aya hii ina ukweli unao onyeshea taadhima ya Muumba. Mbingu ni moja katika Ishara za Mwenyezi Mungu inayo tubainikia kwetu kwa miale ya jua inayo piga juu ya anga linalo izunguka dunia. Miale hii inapo angukia chembe chembe na vumbi vumbi jembamba liliopo angani humulika mianga hiyo na kutawanyika kila upande. Huu mwanga mweupe kwa hakika ni mkusanyiko wa rangi zote zionekanazo. Hizi chembe chembe za angani huzimeza baadhi ya hizo rangi. Imedhihiri kuwa rangi yenye kuenea zaidi ni rangi ya kibuluu. Na hii inazidi kuzagaa linapo kuwa jua liko utosini, na ubuluu wake unapungua kidogo kidogo mpaka jua linapo kuwa upeo wa macho wakati wa magharibi au alfajiri. Wakati huo ile miale ya jua inakwenda masafa makubwa zaidi kabisa. Kwa hivyo zile chembe chembe za angani huzimeza rangi zote isipo kuwa rangi nyekundu. Usafi wa maneno ni: mwangaza wa mchana unahitaji miale ya jua na kuwepo vumbi la kutosha katika anga. Dalili ya hayo ni yale yaliyo tokea mwaka 1944 mbingu ilipo ingia kiza ghafla kati ya mchana. Jinsi ya kiza mchana ukawa kama usiku. Kwa wakati mfupi yakawa hayo, kisha mbingu ikawa nyekundu, kisha kidogo kidogo ikawa rangi ya machungwa, na kisha ya manjano mpaka mbingu ikarejea rangi yake ya tabia, baada ya saa au zaidi. Baadae ilibainika kuwa mambo hayo yalitokana na mripuko mbinguni likatokea jivu, likachukuliwa na upepo mbali mpaka Afrika ya kati na kaskazini, na kufika magharibi ya Asia. Huko ndiko ikaonekana hali hiyo katika pande za Syria. Maelezo yake ni kuwa vumbi lilioko hewani liliifunika nuru ya jua. Lilipo pungua jivu ulidhihiri mwangaza mwekundu na baadae wa manjano n.k. Mwanaadamu akipaa angani katika chombo atapitia matabaka yanayo khitalifiana sifa. Ataiona mbingu inazidi ubuluu mpaka akifika kwenye anga la nje lisio kuwa na hayo mavumbi n.k. ataona mbingu yote ni kiza kitupu kama kwamba ni usiku juu ya kuwa jua lipo juu. Kwa ufupi ni kuwa zipo mbingu nyingi si moja ziliyo pandana tabaka kwa tabaka kama maqubba, zinazo khitalifiana katika sifa zake na rangi zake. Haya ni katika Ishara za Mwenyezi Mungu Mtukufu Aliye takasika kuwa vyote viliomo mbinguni na ardhini vinamtukuza Yeye. Ama kukhitalifiana usiku na mchana, tumekwisha fahamu kuwa mwanga wa mchana unategemea miale ya jua kuanguka juu ya hili funiko la anga, lenye chembe chembe za vumbi kwa kiasi maalumu. Mwangaza huu ni mkali hata unaficha mwangaza unao toka kwenye nyota n.k. Ama wakati wa usiku mwangaza wa jua unapo fichika, inakuwa hapana katika anga isipo kuwa vumbi linalo tuzunguka na mianga dhaifu ya nyota. Kupishana usiku na mchana ni kwa sababu ya kuzunguka dunia kwa nafsi yake wenyewe, na tafauti ya misimu na kurefuka na kufupika usiku na mchana ni kwa mzunguko wa hii dunia kulizunguka jua. Na katika hikima yake Mwenyezi Mungu na uwezo wake ni kuwa kubadilika usiku na mchana, na kubadilika misimu ya joto na baridi, ni kutengeneza hali ya hewa iwe wastani, yaani kati na kati, kwa kusilihi maisha ya vilivyo hai.

التفاسير:

external-link copy
191 : 3

ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَٰمٗا وَقُعُودٗا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَٰذَا بَٰطِلٗا سُبۡحَٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ

Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa Mbingu na Ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto. info

Ni shani ya wenye akili kuwa kila pahali wao wanahudhurisha katika nafsi zao adhama na utukufu wa Mwenyezi Mungu, wakiwa wamesimama au wamekaa au wamejinyoosha kitandani, na wanazingatia uumbaji wa mbingu na ardhi pamoja na viliomo ndani yake, na huku wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuumba haya ila kwa hikima uliyo ikadiria. Na Wewe umetakasika na kila upungufu. Bali umeumba hivi vyote kuwa ni dalili ya kudra yako, na ishara ya upeo wa hikima yako. Utuhifadhi na adhabu ya Moto kwa kutuwezesha kukut'ii.

التفاسير:

external-link copy
192 : 3

رَبَّنَآ إِنَّكَ مَن تُدۡخِلِ ٱلنَّارَ فَقَدۡ أَخۡزَيۡتَهُۥۖ وَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ

Mola wetu Mlezi! Hakika unaye mtia Motoni umemhizi; na walio dhulumu hawana wasaidizi. info

Ewe Muumba wetu, na Mwenye kutusimamia mambo yetu, na Mlinzi wetu! Hakika mwenye kustahiki Moto na ukamuingiza, basi umempa hizaya. Na mwenye kudhulumu akastahiki Moto hana wa kumnusuru nao.

التفاسير:

external-link copy
193 : 3

رَّبَّنَآ إِنَّنَا سَمِعۡنَا مُنَادِيٗا يُنَادِي لِلۡإِيمَٰنِ أَنۡ ءَامِنُواْ بِرَبِّكُمۡ فَـَٔامَنَّاۚ رَبَّنَا فَٱغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرۡ عَنَّا سَيِّـَٔاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ ٱلۡأَبۡرَارِ

Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tumemsikia mwenye kuita akiitia Imani kwamba: Muaminini Mola wenu Mlezi; nasi tukaamini. Basi tusamehe madhambi yetu, na utufutie makosa yetu, na utufishe pamoja na watu wema. info

Ewe Muumba wetu, na Mwenye kutusimamia mambo yetu, na Mlinzi wetu! Hakika sisi tumemsikia Mtume wako akiita watu wakuamini Wewe, nasi tukamt'ii na tukamuamini. Ewe Mola wetu Mlezi! Tughufirie madhambi yetu makubwa, na tufutie maovu yetu madogo madogo, na baada ya kufa kwetu tujaalie tuwe pamoja na waja wako walio bora.

التفاسير:

external-link copy
194 : 3

رَبَّنَا وَءَاتِنَا مَا وَعَدتَّنَا عَلَىٰ رُسُلِكَ وَلَا تُخۡزِنَا يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ إِنَّكَ لَا تُخۡلِفُ ٱلۡمِيعَادَ

Mola wetu Mlezi! Na utupe uliyo tuahidi kwa Mitume wako, wala usituhizi Siku ya Kiyama. Hakika Wewe huvunji miadi. info

Ewe Muumba wetu, na Mwenye kutusimamia mambo yetu, na Mlinzi wetu! Tupe uliyo tuahidi kwa ndimi za Mitume yako, nayo ni ushindi na kuungwa mkono duniani. Wala usituingize Motoni ukatuhizi Siku ya Kiyama. Shani yako ni kuwa huendi kinyume na miadi yako.

التفاسير: