Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Abdullah Muchamed ir Nasir Khamis

Puslapio numeris:close

external-link copy
20 : 4

وَإِنۡ أَرَدتُّمُ ٱسۡتِبۡدَالَ زَوۡجٖ مَّكَانَ زَوۡجٖ وَءَاتَيۡتُمۡ إِحۡدَىٰهُنَّ قِنطَارٗا فَلَا تَأۡخُذُواْ مِنۡهُ شَيۡـًٔاۚ أَتَأۡخُذُونَهُۥ بُهۡتَٰنٗا وَإِثۡمٗا مُّبِينٗا

Na mnapotaka kubadilisha mke mahali pa mke mwengine, na mkawa mumempa yule mnayetaka kumtaliki mali mengi yakiwa ni mahari yake. Si halali kwenu kuchukua chochote katika mali hayo. Je mnayachukua kwa njia ya urongo na uzushi ulio wazi? info
التفاسير:

external-link copy
21 : 4

وَكَيۡفَ تَأۡخُذُونَهُۥ وَقَدۡ أَفۡضَىٰ بَعۡضُكُمۡ إِلَىٰ بَعۡضٖ وَأَخَذۡنَ مِنكُم مِّيثَٰقًا غَلِيظٗا

Na vipi itakuwa ni halali kwenu kukichukua mlichowapa cha mahari, na kila mmoja kati yenu amejiliwaza na mwenzake kwa kuingiliana na walichukua kutoka kwenu ahadi iliyo nzito ya kuwa mtashikamana nao kwa wema au mtaepukana nao kwa ihsani? info
التفاسير:

external-link copy
22 : 4

وَلَا تَنكِحُواْ مَا نَكَحَ ءَابَآؤُكُم مِّنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۚ إِنَّهُۥ كَانَ فَٰحِشَةٗ وَمَقۡتٗا وَسَآءَ سَبِيلًا

Wala msiwaoe wanawake walioolewa na baba zenu, isipokuwa yaliyopita mliyoyafanya katika zama za jahiliyyah (kabla ya Uislamu). Hayo hamtalipwa kwayo. Hakika ndoa ya watoto kuwaoa waliokuwa wake wa baba zao ni jambo baya lenye upeo wa ubaya, na ni jambo lenye kuchukiza ambalo Mwenyezi Mungu Anamchukia mwenye kulifanya. Na ubaya wa njia na mwenendo ni huo mliokuwa mkiufanya zama za ujinga wenu( kabla ya Uislamu). info
التفاسير:

external-link copy
23 : 4

حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمۡ أُمَّهَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُمۡ وَعَمَّٰتُكُمۡ وَخَٰلَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُ ٱلۡأَخِ وَبَنَاتُ ٱلۡأُخۡتِ وَأُمَّهَٰتُكُمُ ٱلَّٰتِيٓ أَرۡضَعۡنَكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُم مِّنَ ٱلرَّضَٰعَةِ وَأُمَّهَٰتُ نِسَآئِكُمۡ وَرَبَٰٓئِبُكُمُ ٱلَّٰتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَآئِكُمُ ٱلَّٰتِي دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمۡ تَكُونُواْ دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ وَحَلَٰٓئِلُ أَبۡنَآئِكُمُ ٱلَّذِينَ مِنۡ أَصۡلَٰبِكُمۡ وَأَن تَجۡمَعُواْ بَيۡنَ ٱلۡأُخۡتَيۡنِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Mwenyezi Mungu Amewaharamishia kuwaoa mama zenu, wanaingia kwenye uharamu huu manyanya wa upande wa baba na upande wa mama, na mabinti zenu, wanaingia kwenye uharamu huu mabinti wa watoto wa kiume au wa kike na kwenda chini, na dada zenu kwa baba na mama au kwa baba au kwa mama, na mashangazi zenu, nao ni ndugu wa kike wa baba zenu na babu zenu, na makhalati zenu, nao ni dada za mama zenu na nyanya zenu, na mabinti wa ndugu wa kiume na mabinti wa ndugu wa kike; na waingia humo watoto wao, na mama zenu waliowanyonyesha, na dada zenu mlionyonya nao; na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameharamisha kwa ajili ya kunyonya kila aliyeharamishwa kwa ajili ya ukaribu wa nasaba. Pia ni haramu kuwaoa mama za wake zenu, muwe mumewaingilia hao wake zenu au hamukuwaingilia, na mabinti wa wake zenu wa mababa wengine ambao kawaida wanalelewa majumbani mwenu na chini ya uangalizi wenu, wao ni haramu kuwaoa hata kama hawamo majumbani mwenu, lakini kwa sharti ya kuwaingilia mama zao. Na iwapo hamkuwaingilia mama zao , na mkawataliki au wakafa kabla ya kuwaingilia, hapo hapana makosa kuwaoa mabinti wao. Pia amewaharamishia Mwenyezi Mungu kuwaoa waliokuwa wake wa watoto wenu watokao migongoni mwenu, na wale walioshikanishwa na wao ambao ni watoto wenu wa kiume kwa kunyonya. Kuharamishwa huku kunakuwa kwa kufunga ndoa, awe yule mtoto wa kiume amemuingilia mkewe au hakumuingilia. Pia Amewaharamishia kuwakusanya pamoja, kwenye ndoa, dada wawili wa nasaba au wa kunyonya, isipokuwa yale yaliopita mlioyafanya katika zama za kabla ya Uislamu. Kadhalika, haifai kuwakusanya, kindoa, mwanamke na shangazi yake au khalati yake, kama ilvyokuja katika Sunnah. Mwenyezi Mungu daima ni Mwenye kuwasamehe watenda madhambi pindi wanapotubia. Ni Mwenye huruma nao, Hawakalifishi wasiloliweza. info
التفاسير: