Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Vertimas į suahilių k. - Abdullah Muchamed ir Nasir Khamis

Puslapio numeris:close

external-link copy
148 : 4

۞ لَّا يُحِبُّ ٱللَّهُ ٱلۡجَهۡرَ بِٱلسُّوٓءِ مِنَ ٱلۡقَوۡلِ إِلَّا مَن ظُلِمَۚ وَكَانَ ٱللَّهُ سَمِيعًا عَلِيمًا

Hapendi Mwenyezi Mungu kwa yoyote adhihirishe neno ovu. Lakini yaruhusiwa kwa aliyedhulumiwa amtaje aliyemdhulumu kwa uovu alionao, ili akibainishe alichodhulumiwa nacho. Na daima Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyasikia mnayoyadhihirisha na ni Mwenye kuyajua mnayoyaficha kati ya hayo. info
التفاسير:

external-link copy
149 : 4

إِن تُبۡدُواْ خَيۡرًا أَوۡ تُخۡفُوهُ أَوۡ تَعۡفُواْ عَن سُوٓءٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَفُوّٗا قَدِيرًا

Amehimiza Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwamba watu wasamehe, na Akaweka msingi wa jambo hilo kwa kuwa Muumini, ima aidhihirishe kheri au aifiche. Na vilevile katika kukosewa, ima adhihirishe kuwa amekosewa katika hali ya kutafuta haki yake kwa aliyemkosea au asamehe na apuuze. Na kusamehe ni bora. Kwani miongoni mwa sifa za Mwenyezi Mungu ni kuwasamehe waja Wake pamoja na uwezo Wake juu yao. info
التفاسير:

external-link copy
150 : 4

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡفُرُونَ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦ وَيُرِيدُونَ أَن يُفَرِّقُواْ بَيۡنَ ٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦ وَيَقُولُونَ نُؤۡمِنُ بِبَعۡضٖ وَنَكۡفُرُ بِبَعۡضٖ وَيُرِيدُونَ أَن يَتَّخِذُواْ بَيۡنَ ذَٰلِكَ سَبِيلًا

Hakika wanaomkanusha Mwenyezi Mungu na Mitume Wake, kati ya Mayahudi na Wanaswara, na kutaka kutenganisha baina ya Mwenyezi Mungu na Mitume Wake, kwa kumuamini kwao Mwenyezi Mungu na kuwakanusha Mitume Wake Aliowatuma kwa viumbe Wake, au wautambue ukweli wa baadhi ya Mitume na kuacha kuwatambua wengine na wadai kwamba baadhi yao wamemzulia Mola wao urongo na wanataka kujifanyia njia ya kuelekea kwenye upotofu waliouanzisha na uzushi waliouzua. info
التفاسير:

external-link copy
151 : 4

أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ حَقّٗاۚ وَأَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٗا مُّهِينٗا

Hao ndio wenye ukafiri wa hakika usiokuwa na shaka. Na tumewaandalia makafiri adhabu itakayowadhili na kuwatweza. info
التفاسير:

external-link copy
152 : 4

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦ وَلَمۡ يُفَرِّقُواْ بَيۡنَ أَحَدٖ مِّنۡهُمۡ أُوْلَٰٓئِكَ سَوۡفَ يُؤۡتِيهِمۡ أُجُورَهُمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Na wale walioukubali upweke wa Mwenyezi Mungu na wakautambua unabii wa wajumbe Wake wote na wasimbague yoyote kati yao na wakaifuata kivitendo sheria ya Mwenyezi Mungu, hao Atawapa malipo yao na thawabu zao kwa kumuamini kwao Yeye na Mitume Wake. Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa waja Wake, ni Mwenye huruma kwao. info
التفاسير:

external-link copy
153 : 4

يَسۡـَٔلُكَ أَهۡلُ ٱلۡكِتَٰبِ أَن تُنَزِّلَ عَلَيۡهِمۡ كِتَٰبٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِۚ فَقَدۡ سَأَلُواْ مُوسَىٰٓ أَكۡبَرَ مِن ذَٰلِكَ فَقَالُوٓاْ أَرِنَا ٱللَّهَ جَهۡرَةٗ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّٰعِقَةُ بِظُلۡمِهِمۡۚ ثُمَّ ٱتَّخَذُواْ ٱلۡعِجۡلَ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ فَعَفَوۡنَا عَن ذَٰلِكَۚ وَءَاتَيۡنَا مُوسَىٰ سُلۡطَٰنٗا مُّبِينٗا

Wanakutaka Mayahudi, ewe Mtume, uwaonyeshe miujiza mfano wa miujiza ya Mūsā iwe ni ushahidi kwako kuwa ni mkweli, nao ni uwateremshie kurasa zitokazo kwa Mwenyezi Mungu hali ya kuwa zimeandikwa, kama vile Mūsā alivyoleta mbao kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Usione ajabu, ewe Mtume, kwani wakale wao walimtaka Mūsā, amani imshukie, awaletee makubwa zaidi. Walimtaka Awaonyeshe Mwenyezi Mungu waziwazi, hapo wakateremshiwa moto uliowaua kwa sababu ya kuzidhulumu nafsi zao walipolitaka jambo ambalo si haki yao. Na baada ya Mwenyezi Mungu kuwahuisha, baada ya kufa kwao, na wakaishuhudia miujiza iliyo waziwazi, kutoka kwa Mtume Mūsā, inayopinga katakata ushirikina, waliabuduu kigombe badala ya Mwenyezi Mungu. Kisha tuliwasamehe kosa lao la kuabudu ndama kwa sababu ya kutubia kwao na tukampa Mūsā hoja kubwa zilizotilia nguvu ukweli wa utume wake info
التفاسير:

external-link copy
154 : 4

وَرَفَعۡنَا فَوۡقَهُمُ ٱلطُّورَ بِمِيثَٰقِهِمۡ وَقُلۡنَا لَهُمُ ٱدۡخُلُواْ ٱلۡبَابَ سُجَّدٗا وَقُلۡنَا لَهُمۡ لَا تَعۡدُواْ فِي ٱلسَّبۡتِ وَأَخَذۡنَا مِنۡهُم مِّيثَٰقًا غَلِيظٗا

Na tukaliinua juu ya vichwa vyao jabali la Tūr walipokataa kujilazimisha na ahadi iliyotiliwa mkazo waliyoitoa ya kuwa watazitumia hukumu za Taurati. Na tukawaamrisha waingie lango la Bait al-Maqdis hali ya kusujudu , nao wakaingia wakijikokota kwa matako yao. Na tukawaamrisha wasifanye uadui kwa kuvua siku ya Jumamosi, wakafanya uadui hivyo hivyo na wakavua. Na tukachukua kutoka kwao ahadi ya mkazo, pia waliivunja hivyo hivyo. info
التفاسير: