[1] Maana ya 'ukafiri' katika lugha ya Kiarabu ni kufunika kitu. Kwa hivyo, mtu kafiri ameitwa kwa hilo jina kwa sababu yeye huifunika haki. (Zaad Al-Masiir fii 'ilm At-Tafsiir, cha Ibn Al-Jawzii).
[2] Alipowataja Waumini na hali zao (katika aya ya pili hadi ya tano), akawataja makafiri na hatima yao (katika aya ya sita na saba) (Tafsir Al-Qurtubii).
[1] Na kauli yake "wana" inaashiria kwamba hali yao inaitisha sana adhabu hii, na kwamba wanaistahiki, na kwamba nafsi zao zinaelekea kwenye adhabu hiyo mpaka waione waziwazi. Na kauli yake "kubwa" ni kwa sababu itaiadhibu miili yao kiujumla bila kuacha chochote, kwa sababu miili yao na nafsi zao na roho zao havikugusa chochote cha kuwazuia kutokana na adhabu. (Tafsir Al-Baqa'ii)
[1] Alipowaeleza Waumini mwanzoni mwa sura hii kwa aya nne (kuanzia aya ya pili hadi ya tano), kisha akabainisha hali ya makafiri kwa aya mbili (ya sita na saba). Mwenyezi Mungu Mtukufu akaanza kueleza hali ya wanafiki wanaodhihirisha imani na kuficha ukafiri. Na kwa kuwa jambo lao huwa linawachanganya watu wengi, akarefusha mno katika kuwataja kwa sifa zao nyingi (katika aya kumi na tatu). (Tafsir Ibn Kathir)
[1] Wanaitakidi kwa ujinga wao kuwa wao wanamhadaa Mwenyezi Mungu na Waumini kwa kudhihirisha kwao Imani na kuficha kwao ukafiri. Nao hawamhadai yoyote isipokuwa wao wenyewe, kwa kuwa, madhara ya kuhadaa kwao yanawarudia wao. Na kwa sababu ujinga wao umekolea na nyoyo zao zimeharibika, huwa hawana hisia ya hilo. (Tafsir Muyasar cha jopo la wanachuoni)
[1] Kilichokusudiwa na maradhi hapa ni maradhi ya shaka, dhana potovu na unafiki. (Tafsir Assa'dii).
[2] Al-Junayd alisema: Ugonjwa wa nyoyo ni kufuata matamanio, kama vile ugonjwa wa viungo ni yale maradhi ya kiwiliwili. (Tafsir Al-Qurtubii).
[1] Na kujengeka kwa kitendo hiki (wanapoambiwa) katika hali ya kutomtaja anayewaambia, kunaashiria kwamba wao humuasi yeyote yule anayewaambia hata awe ni nani. (Tafsir Nidhaam Addurar fii Tanasub Al-Aayat Wassuwar cha Al-Baqaa'ii)
[1] Na huu ni katika mifano mizuri kabisa. Kwani (mnafiki) aliufanya upotovu ambao ndio shari kubwa zaidi kuwa bidhaa, na akaufanya uwongofu ambao ndio kutengenea kukubwa zaidi pahali pa bei. Kwa hivyo, wakautoa uwongofu (ambayo ndiyo bei) kwa kuukataa na kuutaka upotovu (ambayo ndiyo bidhaa). (Tafsir Assa'dii) Lakini biashara hiyo yao haikupata faida, pamoja na kudai kwao kwamba wao ndio wajuzi zaidi katika hilo la kutengeneza. Na wala hawakuongoka, yaani walipoteza mpaka mtaji wao, yani uwongofu wa Qur-aani. (Tafsir Nidhaam Addurar fii Tanasub Al-Aayat Wassuwar cha Al-Baqaa'ii)