[1] Alipowaeleza Waumini mwanzoni mwa sura hii kwa aya nne (kuanzia aya ya pili hadi ya tano), kisha akabainisha hali ya makafiri kwa aya mbili (ya sita na saba). Mwenyezi Mungu Mtukufu akaanza kueleza hali ya wanafiki wanaodhihirisha imani na kuficha ukafiri. Na kwa kuwa jambo lao huwa linawachanganya watu wengi, akarefusha mno katika kuwataja kwa sifa zao nyingi (katika aya kumi na tatu). (Tafsir Ibn Kathir)