[1] Maana ya 'ukafiri' katika lugha ya Kiarabu ni kufunika kitu. Kwa hivyo, mtu kafiri ameitwa kwa hilo jina kwa sababu yeye huifunika haki. (Zaad Al-Masiir fii 'ilm At-Tafsiir, cha Ibn Al-Jawzii).
[2] Alipowataja Waumini na hali zao (katika aya ya pili hadi ya tano), akawataja makafiri na hatima yao (katika aya ya sita na saba) (Tafsir Al-Qurtubii).