[1] Na maana wenza ni yule anayekaa na kuandamana nawe na hamuachani. (Tafsir Al-Alusii) Hao pia wataandamana na Moto bila ya kuachana kama wenza.
[1] “Enyi Wana wa Israili!” Anayekusudiwa na Israili hapa ni (Nabii) Yaaqub, amani iwe juu yake. (Tafsir Assa'dii)
[1] Aya hii inawaonya wana wa Israili dhidi ya kuyauza mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa kuficha maelezo ya Muhammad - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - yaliyopo katika vitabu vyao. Na kuchukua "thamani ndogo" ya duniani kama vile yale wanayopata kutoka kwa wafuasi wao kama vile chakula, uongozi n.k. (Tafsir Al-Wajiiz cha Al-Waahidii)
[1] Na alipowakataza kufuata matamanio yao, akawaongoza kwenye dawa ya hilo, ambayo ni maadili makubwa zaidi ya kinafsi na matendo bora ya kimwili, ambayo ni kuwa na "subira" katika kudhihirisha haki na kutotii matamanio ya nafsi zao katika hilo. Na "swala" ambayo inafikisha katika vyeo vikubwa zaidi kuliko hivyo vya kidunia. (Tafsir Al-Baqaa'ii)
[1] Aya hii imekanusha (huko Akhera) mambo ambayo wanadamu wamezoea kuyafanya katika dunia hii wanapopatwa na shida. (Tafsir Assa'dii). Nayo ni kufanyiwa uombezi, au kutoa fidiya, au kunusuriwa. (Tafsir Al-Muharrar Al-Wajiiz cha Ibn Atwiyya)