ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߙߎ߬ߥߊ߯ߘߎ-ߕߊ߬ߙߑߖߡߊ ߝߊ߲ߓߊ ߓߟߏ߫

ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ:close

external-link copy
38 : 2

قُلۡنَا ٱهۡبِطُواْ مِنۡهَا جَمِيعٗاۖ فَإِمَّا يَأۡتِيَنَّكُم مِّنِّي هُدٗى فَمَن تَبِعَ هُدَايَ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Tukasema: Shukeni nyote; na kama ukikufikieni uwongofu utokao kwangu, basi watakaofuata uwongofu wangu huo, haitakuwa hofu juu yao wala hawatahuzunika. info
التفاسير:

external-link copy
39 : 2

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na wenye kukufuru na kuzikanusha ishara zetu, hao ndio wenza wa Moto, wao watadumu humo.[1] info

[1] Na maana wenza ni yule anayekaa na kuandamana nawe na hamuachani. (Tafsir Al-Alusii) Hao pia wataandamana na Moto bila ya kuachana kama wenza.

التفاسير:

external-link copy
40 : 2

يَٰبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتِيَ ٱلَّتِيٓ أَنۡعَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ وَأَوۡفُواْ بِعَهۡدِيٓ أُوفِ بِعَهۡدِكُمۡ وَإِيَّٰيَ فَٱرۡهَبُونِ

Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni neema yangu niliyokuneemesheni, na timizeni ahadi yangu, na Mimi nitatimiza ahadi yenu, na niogopeni Mimi tu.[1] info

[1] “Enyi Wana wa Israili!” Anayekusudiwa na Israili hapa ni (Nabii) Yaaqub, amani iwe juu yake. (Tafsir Assa'dii)

التفاسير:

external-link copy
41 : 2

وَءَامِنُواْ بِمَآ أَنزَلۡتُ مُصَدِّقٗا لِّمَا مَعَكُمۡ وَلَا تَكُونُوٓاْ أَوَّلَ كَافِرِۭ بِهِۦۖ وَلَا تَشۡتَرُواْ بِـَٔايَٰتِي ثَمَنٗا قَلِيلٗا وَإِيَّٰيَ فَٱتَّقُونِ

Na aminini niliyoyateremsha ambayo yanasadikisha mliyo nayo, wala msiwe wa kwanza kuyakataa. Wala msiuze Ishara zangu kwa thamani ndogo. Na niogopeni Mimi tu.[1] info

[1] Aya hii inawaonya wana wa Israili dhidi ya kuyauza mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa kuficha maelezo ya Muhammad - rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - yaliyopo katika vitabu vyao. Na kuchukua "thamani ndogo" ya duniani kama vile yale wanayopata kutoka kwa wafuasi wao kama vile chakula, uongozi n.k. (Tafsir Al-Wajiiz cha Al-Waahidii)

التفاسير:

external-link copy
42 : 2

وَلَا تَلۡبِسُواْ ٱلۡحَقَّ بِٱلۡبَٰطِلِ وَتَكۡتُمُواْ ٱلۡحَقَّ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Wala msichanganye kweli na uwongo, na mkaificha kweli nanyi mnajua. info
التفاسير:

external-link copy
43 : 2

وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ وَٱرۡكَعُواْ مَعَ ٱلرَّٰكِعِينَ

Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na inameni pamoja na wanaoinama. info
التفاسير:

external-link copy
44 : 2

۞ أَتَأۡمُرُونَ ٱلنَّاسَ بِٱلۡبِرِّ وَتَنسَوۡنَ أَنفُسَكُمۡ وَأَنتُمۡ تَتۡلُونَ ٱلۡكِتَٰبَۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Je, mnawaamrisha watu mema na mnazisahau nafsi zenu, na hali nyinyi mnasoma Kitabu? Basi je, hamzingatii? info
التفاسير:

external-link copy
45 : 2

وَٱسۡتَعِينُواْ بِٱلصَّبۡرِ وَٱلصَّلَوٰةِۚ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلَّا عَلَى ٱلۡخَٰشِعِينَ

Na tafuteni msaada kwa kusubiri na kwa kusali; na kwa hakika jambo hilo ni gumu isipokuwa kwa wanyenyekevu.[1] info

[1] Na alipowakataza kufuata matamanio yao, akawaongoza kwenye dawa ya hilo, ambayo ni maadili makubwa zaidi ya kinafsi na matendo bora ya kimwili, ambayo ni kuwa na "subira" katika kudhihirisha haki na kutotii matamanio ya nafsi zao katika hilo. Na "swala" ambayo inafikisha katika vyeo vikubwa zaidi kuliko hivyo vya kidunia. (Tafsir Al-Baqaa'ii)

التفاسير:

external-link copy
46 : 2

ٱلَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَٰقُواْ رَبِّهِمۡ وَأَنَّهُمۡ إِلَيۡهِ رَٰجِعُونَ

Ambao wana yakini kuwa hakika watakutana na Mola wao Mlezi na ya kuwa hakika watarejea kwake. info
التفاسير:

external-link copy
47 : 2

يَٰبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتِيَ ٱلَّتِيٓ أَنۡعَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ وَأَنِّي فَضَّلۡتُكُمۡ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Enyi Wana wa Israili! Kumbukeni zile neema zangu nilizokuneemesheni, na nikakuteueni kuliko wote wengineo. info
التفاسير:

external-link copy
48 : 2

وَٱتَّقُواْ يَوۡمٗا لَّا تَجۡزِي نَفۡسٌ عَن نَّفۡسٖ شَيۡـٔٗا وَلَا يُقۡبَلُ مِنۡهَا شَفَٰعَةٞ وَلَا يُؤۡخَذُ مِنۡهَا عَدۡلٞ وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Na icheni Siku ambayo mtu hatomfaa mtu kwa lolote, wala hayatakubaliwa kwake maombezi, wala hakitapokewa kikomboleo kwake; wala hawatanusuriwa.[1] info

[1] Aya hii imekanusha (huko Akhera) mambo ambayo wanadamu wamezoea kuyafanya katika dunia hii wanapopatwa na shida. (Tafsir Assa'dii). Nayo ni kufanyiwa uombezi, au kutoa fidiya, au kunusuriwa. (Tafsir Al-Muharrar Al-Wajiiz cha Ibn Atwiyya)

التفاسير: