[1] Vipi hali yako unapooambiwa kumcha Mwenyezi Mungu? Ilipokewa kwamba 'Umar Ibn Al-Khattwab - Mwenyezi Mungu amwiye radhi - aliambiwa, "Ittaqillah (mche Mwenyezi Mungu"). Kwa hivyo, akaliweka shavu lake juu ya ardhi kwa kumnyenyekea Mwenyezi Mungu.(Tafsir Assam'aanii)
[1] Mwenyezi Mungu alipoeleza katika Aya iliyotangulia hali ya mtu anayeitoa dini yake kwa ajili ya mambo ya kidunia. Akaitaja katika Aya hii hali ya mtu anayeyatoa maisha yake ya duniani, nafsi yake na mali yake ili kutafuta dini. (Tafsir Ar-Raazii)