[1] Mayahudi na Manaswara hawawaridhii Waislamu kwa chochote isipokuwa kwamba wawafuate katika dini yao. Lakini hayo waliyo nayo ni matamanio tu, siyo dini ya haki, kwa dalili ya kauli yake. "Na kama ukifuata matamanio yao baada ya yale yaliyokujia katika elimu, basi hutapata mlinzi wala msaidizi yeyote kando na Mwenyezi Mungu." (Tafsir Assa'dii)