[1] Taghut inamaanisha Shetani, mchawi, kuhani, sanamu, waovu katika watu na majini. Chochote kipitacho mipaka ya Mwenyezi Mungu na kinaabudiwa badala yake ima kwa kulazimisha hilo au kutiiwa tu sawa kiwe mwanadamu au sanamu (Tafsir ya Al-Mawardii).
[2] Na wala hakuna upinzani baina ya maana hii na Aya nyingi zinazolazimu kuwepo kwa Jihadi. Kwani, Mwenyezi Mungu ameamrisha kupigana vita ili Dini yote iwe ya Mwenyezi Mungu tu. Na kuzuia uadui wa wenye kufanya uadui dhidi ya dini. (Tafsir Assa'dii)