ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
62 : 3

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡقَصَصُ ٱلۡحَقُّۚ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّا ٱللَّهُۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Hakika hili nililokuhadithia, ewe Mtume, kuhusu mambo ya ‘Īsā ndio habari ya kweli isiyo na shaka. Na hakuna muabudiwa anayestahiki ibada isipokuwa ni Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na hakika Mwenyezi Mungu Ndiye Mshindi katika ufalme Wake, Ndiye Mwenye hekima katika upelekaji mambo Wake na vitendo Vyake. info
التفاسير:

external-link copy
63 : 3

فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُفۡسِدِينَ

Na wakikataa kukuamini na kukufuata, basi wao ndio waharibifu. Na Mwenyezi Mungu Anawajua na Atawalipa kwa hilo. info
التفاسير:

external-link copy
64 : 3

قُلۡ يَٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ كَلِمَةٖ سَوَآءِۭ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ أَلَّا نَعۡبُدَ إِلَّا ٱللَّهَ وَلَا نُشۡرِكَ بِهِۦ شَيۡـٔٗا وَلَا يَتَّخِذَ بَعۡضُنَا بَعۡضًا أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَقُولُواْ ٱشۡهَدُواْ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia Watu wa Kitabu miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, «Njooni kwenye neno la uadilifu na haki tushikamane nalo sote. Nalo ni sisi kuielekeza ibada yetu kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na tusimfanye yoyote kuwa ni mshirika pamoja na Yeye, awe ni sanamu au msalaba au Shetani au kinginecho. Na wala wasiwadhalilikie baadhi yetu watu wengine kwa kuwatii badala ya Mwenyezi Mungu.» Basi wakiukataa mwito huu mzuri, waambieni wao, enyi Waumini, «Kuweni ni mashahidi kwetu kuwa sisi tumejisalimisha kwa Mola wetu na tumenyosha shingo zetu Kwake kwa kukubali kuwa ni waja Wake na kwa kumtakasa.» Na mwito huu kwenye neno la sawa, kama unavyoelekezwa kwa Mayahudi na Wanaswara, unaelekezwa pia kwa wenye mwenendo kama wao. info
التفاسير:

external-link copy
65 : 3

يَٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تُحَآجُّونَ فِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمَآ أُنزِلَتِ ٱلتَّوۡرَىٰةُ وَٱلۡإِنجِيلُ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Enyi watu wa vitabu vilivyoteremshwa, miongoni Mwa Mayahudi na Wanaswara, vipi kila mmoja kati yenu anabisha kwamba Ibrāhīm, amani imshukie, alikuwa kwenye mila yake. Ilhali Taurati na Injili hazikuteremshwa ela baada yake? Kwani hamufahamu upotofu wa maneno yenu kwamba Ibrāhīm alikuwa Myahudi au Mnaswara, na hali mnajua kuwa Uyahudi na Unaswara ulizuka baada ya kufa kwake kwa muda? info
التفاسير:

external-link copy
66 : 3

هَٰٓأَنتُمۡ هَٰٓؤُلَآءِ حَٰجَجۡتُمۡ فِيمَا لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞ فَلِمَ تُحَآجُّونَ فِيمَا لَيۡسَ لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

Ndio nyinyi enyi hawa, mliomjadili Mtume wa Mwenyezi Mungu , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, juu ya mambo ya dini yenu ambayo muna ujuzi nayo, katika yale yaliyomo ndani ya vitabu vyenu mnayoitakidi usahihi wake. Lakini ni kwa nini nyinyi mnayajadili mambo ya Ibrāhīm ambayo hamuna ujuzi nayo? Na Mwenyezi Mungu Anayajua mambo pamoja na kuwa yamefichika, na nyinyi hamjui. info
التفاسير:

external-link copy
67 : 3

مَا كَانَ إِبۡرَٰهِيمُ يَهُودِيّٗا وَلَا نَصۡرَانِيّٗا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفٗا مُّسۡلِمٗا وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Ibrāhīm hakuwa ni Myahudi wala Mnaswara, kwa kuwa Uyahudi haukuwa, wala Unaswara, isipokuwa baada yake. Lakini alikuwa mfuasi na mtiifu wa amri ya Mwenyezi Mungu, aliyejisalimisha Kwake, na hakuwa ni miongoni mwa washirikina. info
التفاسير:

external-link copy
68 : 3

إِنَّ أَوۡلَى ٱلنَّاسِ بِإِبۡرَٰهِيمَ لَلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُ وَهَٰذَا ٱلنَّبِيُّ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۗ وَٱللَّهُ وَلِيُّ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika wenye haki zaidi na Ibrāhīm na wanaohusika naye zaidi ni wale waliomuamini, wakausadiki utume wake na wakaifuata dini yake na huyu Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na waliomuamini yeye.Na Mwenyezi Mungu ni Msaidizi wa wenye kumuamini yeye na kufuata Sheria Yake. info
التفاسير:

external-link copy
69 : 3

وَدَّت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَوۡ يُضِلُّونَكُمۡ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Lilitamani kundi la Mayahudi na Manaswara lau wangaliwapoteza nyinyi, enyi Waislamu, wakawatoa kwenye Uislamu. Wao hawampotezi yoyote isipokuwa nafsi zao na wafuasi wao; na wao hawalielewi hilo wala hawalijui. info
التفاسير:

external-link copy
70 : 3

يَٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَأَنتُمۡ تَشۡهَدُونَ

Enyi watu wa Taurati na Injili! Vipi nyinyi mnakanusha aya za Mwenyezi Mungu ambazo aliziteremsha kwa Mitume wake katika Vitabu vyenu, na ndani yake muna kuwa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ndiye Mtume anayengojewa na kuwa aliyowajia nayo ndio haki. Na nyinyi mnashuhudia hilo, lakini mnalikanusha. info
التفاسير: