ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
133 : 3

۞ وَسَارِعُوٓاْ إِلَىٰ مَغۡفِرَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ وَجَنَّةٍ عَرۡضُهَا ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ أُعِدَّتۡ لِلۡمُتَّقِينَ

Na kimbilieni, kwa kumtii kwenu Mwenyezi Mungu na Mtume wake, ili kupata msamaha mkubwa utokao kwa Mola wenu na mpate Pepo kunjufu, upana wake ni sawa na mbingu na ardhi, Ameiandaa Mweyezi Mungu kwa wachamungu. info
التفاسير:

external-link copy
134 : 3

ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي ٱلسَّرَّآءِ وَٱلضَّرَّآءِ وَٱلۡكَٰظِمِينَ ٱلۡغَيۡظَ وَٱلۡعَافِينَ عَنِ ٱلنَّاسِۗ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Wale ambao wanatoa mali yao katika hali ya wepesi na uzito, na wanaozuia hasira zilizo ndani ya nafsi zao kwa kusubiri, na wanaowasamehe waliowadhulumu wanapokuwa na uwezo. Huu ndio wema ambao Mwenyezi Mungu Anawapenda wenye kuwa nao. info
التفاسير:

external-link copy
135 : 3

وَٱلَّذِينَ إِذَا فَعَلُواْ فَٰحِشَةً أَوۡ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ ذَكَرُواْ ٱللَّهَ فَٱسۡتَغۡفَرُواْ لِذُنُوبِهِمۡ وَمَن يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ إِلَّا ٱللَّهُ وَلَمۡ يُصِرُّواْ عَلَىٰ مَا فَعَلُواْ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Na wale ambao wakitenda dhambi kubwa au wakizidhulumu nafsi zao kwa kutenda dhambi chini ya hizo, wanaikumbuka ahadi ya Mwenyezi Mungu ya malipo mema kwa wanaomtii na malipo mabaya kwa wanaomuasi na wanaelekea kwa Mola wao hali ya kutubia wakawa wanamuomba Awasamehe madhambi yao na wakawa wana yakini kwamba hapana anayasamehe madhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu. Na wao kwa sababu hiyo hawaendelei kwenye maasia, na wao wanajua kwamba wakitubia Mwenyezi Mungu Atawakubalia toba yao. info
التفاسير:

external-link copy
136 : 3

أُوْلَٰٓئِكَ جَزَآؤُهُم مَّغۡفِرَةٞ مِّن رَّبِّهِمۡ وَجَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ وَنِعۡمَ أَجۡرُ ٱلۡعَٰمِلِينَ

Hao waliosifiwa kwa sifa hizo, malipo yao ni kwamba Mwenyezi Mungu Atayasitiri madhambi yao na watapata mabustani ya Peponi ambayo maji tamu yatakuwa yanapita chini ya miti yake na majumba yake ya fahari, ilhali ya kukaa humo milele; hawatotoka humo kamwe. Na malipo bora ya wenye kutenda mema ni msamaha na Pepo. info
التفاسير:

external-link copy
137 : 3

قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِكُمۡ سُنَنٞ فَسِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Mwenyezi Mungu Anawazungumzia Waumini walipopatwa na mikasa siku ya vita vya Uhud kwa kuwaliwaza kwamba wamepita kabla yao ummah wengi ambao waumini kati yao walitahiniwa kwa kupigana na makafiri na ukawa ushindi ni wao. Basi, tembeeni katika ardhi mkizingatia yale yaliyowafika wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na na Mtume Wake. info
التفاسير:

external-link copy
138 : 3

هَٰذَا بَيَانٞ لِّلنَّاسِ وَهُدٗى وَمَوۡعِظَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ

Hii Qur’ani ni ufafanuzi uliyo wazi na ni uongozi kwenye njia ya haki na ni ukumbusho ambao nyoyo za wachamungu zainyenyekea. Nao (hao wachamungu) ni wale wanaomuogopa Mwenyezi Mungu. Wamehusishwa nayo (hiyo Qur’ani kuwa nyoyo zao zinainyenyekea na kuikubali) kwa kuwa wao ndio wanaofaidika nayo, si wengine. info
التفاسير:

external-link copy
139 : 3

وَلَا تَهِنُواْ وَلَا تَحۡزَنُواْ وَأَنتُمُ ٱلۡأَعۡلَوۡنَ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Wala msidhoofike, enyi Waumini, kupigana na maadui wenu, wala msihuzunike kwa yaliyowapata huko Uhud. Na nyinyi ndio washindi na mwisho mwema ni wenu iwapo mtamuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mtafuata Sheria Zake. info
التفاسير:

external-link copy
140 : 3

إِن يَمۡسَسۡكُمۡ قَرۡحٞ فَقَدۡ مَسَّ ٱلۡقَوۡمَ قَرۡحٞ مِّثۡلُهُۥۚ وَتِلۡكَ ٱلۡأَيَّامُ نُدَاوِلُهَا بَيۡنَ ٱلنَّاسِ وَلِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَيَتَّخِذَ مِنكُمۡ شُهَدَآءَۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلظَّٰلِمِينَ

Iwapo yatawapata, enyi Waumini, majaraha au mauaji kwenye vita vya Uḥud, na mkahuzunika kwa hilo, washirikina pia walipatwa na majaraha na mauaji kama hayo katika vita vya Badr. Hizo ni siku Mwenyezi Mungu huzigeuza kati ya watu: wakati mwengine kushinda na wakati mwengine kushindwa. Kwani katika hayo kuna hekima, mpaka yadhihiri yale Aliyoyajua Mwenyezi Mungu hapo azal (kale isiyokuwa na mwanzo), ili Mwenyezi Mungu Ampambanue aliyekuwa mkweli wa Imani na asiyekuwa mkweli, na ili Awakirimu watu miongoni mwenu kwa kuwafanya wafe mashahidi. Na Mwenyezi Mungu Hawapendi waliozidhulumu nafsi zao na wakakaa kwa kuacha kupigana katika njia Yake. info
التفاسير: