ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
187 : 3

وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ لَتُبَيِّنُنَّهُۥ لِلنَّاسِ وَلَا تَكۡتُمُونَهُۥ فَنَبَذُوهُ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ وَٱشۡتَرَوۡاْ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلٗاۖ فَبِئۡسَ مَا يَشۡتَرُونَ

Na kumbuka, ewe Mtume, pindi Mwenyezi Mungu Alipochukua ahadi ya mkazo juu ya wale ambao Mwenyezi Mungu Amewapa Kitabu, miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, Mayahudi walipewa Taurati na Wanaswara walipewa Injili, ili wavitumie na wawafahamishe watu yaliyomo ndani yake wala wasiyafiche. Lakini wao waliiacha ahadi hiyo na hawakujilazimisha nayo. Na wakachukua thamni duni ikiwa ni badali ya wao kuificha haki na kukipotoa Kitabu. Ni mabaya yalioje manunuzi waliyonunua ya kuipoteza kwao ahadi na kubadilisha kwao Kitabu. info
التفاسير:

external-link copy
188 : 3

لَا تَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ يَفۡرَحُونَ بِمَآ أَتَواْ وَّيُحِبُّونَ أَن يُحۡمَدُواْ بِمَا لَمۡ يَفۡعَلُواْ فَلَا تَحۡسَبَنَّهُم بِمَفَازَةٖ مِّنَ ٱلۡعَذَابِۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Wala msiwadhanie wale wanaofurahia matendo maovu waliyoyafanya, kama Mayahudi, wanafiki na wengineo, na wakawa wanapenda kuwa watu wawataje vizuri kwa mambo ambayo hawakuyafanya, basi msiwadhanie wao kuwa ni wenye kuokoka na adhabu ya Mwenyezi Mungu duniani. Na watakuwa na adhabu iumizayo kesho Akhera. Katika haya kuna onyo kali kwa kila mwenye kutenda kitendo kiovu na kukifurahia na kwa kila mwenye kujigamba kwa ambacho hakukifanya ili watu wamsifu na kumshukuru. info
التفاسير:

external-link copy
189 : 3

وَلِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Ni wa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, ufalme wa mbinguni na ardhini na vilivyomo humo. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu. info
التفاسير:

external-link copy
190 : 3

إِنَّ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱخۡتِلَٰفِ ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ لَأٓيَٰتٖ لِّأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Hakika, katika kuziumba mbingu na ardhi, pasi na kuwa na mfano uliotangulia, na katika kufuatana usiku na mchana na kutafautiana kwao, urefu na ufupi, pana dalili na hoja kubwa zinazobainisha upweke wa Mwenyezi Mungu kwa walio na akili timamu. info
التفاسير:

external-link copy
191 : 3

ٱلَّذِينَ يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ قِيَٰمٗا وَقُعُودٗا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمۡ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلۡقِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ رَبَّنَا مَا خَلَقۡتَ هَٰذَا بَٰطِلٗا سُبۡحَٰنَكَ فَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ

Ambao wanamtaja Mwenyezi Mungu katika hali zao zote, wakiwa wamesimama, wakiwa wameketi na wakiwa wamelala kwa mbavu zao, huku wana mazingatio juu ya uumbaji wa mbingu na ardhi hali ya kusema, «Ewe Mola wetu, Hukuuleta uumbaji huu kwa upuzi; Wewe Umetakasika na hilo! Basi tuepushie adhabu ya Moto. info
التفاسير:

external-link copy
192 : 3

رَبَّنَآ إِنَّكَ مَن تُدۡخِلِ ٱلنَّارَ فَقَدۡ أَخۡزَيۡتَهُۥۖ وَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ

«Ewe Mola wetu! Tuokue na Moto, kwani hakika Wewe, ewe Mwenyezi Mungu, yoyote Utakayemuingiza Motoni kwa madhambi yake, ushamfedhehesha na kumtweza. Na watenda madhambi, wanaozidhulumu nafsi zao, hawatakuwa na yoyote wa kuwatetea wasipate adhabu ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama. info
التفاسير:

external-link copy
193 : 3

رَّبَّنَآ إِنَّنَا سَمِعۡنَا مُنَادِيٗا يُنَادِي لِلۡإِيمَٰنِ أَنۡ ءَامِنُواْ بِرَبِّكُمۡ فَـَٔامَنَّاۚ رَبَّنَا فَٱغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرۡ عَنَّا سَيِّـَٔاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ ٱلۡأَبۡرَارِ

«Ewe Mola wetu! Sisi Tumemsikia mlinganizi, naye ni Mtume wako Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anawaita watu wakuamini Wewe na kukubali Umoja wako na kuzifuata kivitendo Sheria zako, tukauitikia ulinganizi wake na tukauamini utume wake. Basi tusamehe madhambi yetu, uzisitiri aibu zetu na utukutanishe na watu wema. info
التفاسير:

external-link copy
194 : 3

رَبَّنَا وَءَاتِنَا مَا وَعَدتَّنَا عَلَىٰ رُسُلِكَ وَلَا تُخۡزِنَا يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ إِنَّكَ لَا تُخۡلِفُ ٱلۡمِيعَادَ

«Ewe Mola wetu! Tupe yale uliyotuahidi kwenye ndimi za Mitume wako, ya kupata ushindi, umakinifu, taufiki na uongofu. Wala usitufedheheshe, kwa madhambi yetu, Siku ya Kiyama. Hakika wewe ni Mkarimu, Huendi kinyume na ahadi ulizowaahidi waja wako.» info
التفاسير: