ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

رقم الصفحة:close

external-link copy
79 : 10

وَقَالَ فِرۡعَوۡنُ ٱئۡتُونِي بِكُلِّ سَٰحِرٍ عَلِيمٖ

Na Firauni akasema: Nileteeni kila mchawi mjuzi! info

Firauni na kaumu yake wakadai kuwa Musa na nduguye ni wachawi, wala si Mitume! Akawataka watu wake wamhudhurishe kila aliye hodari katika fani za uchawi katika mamlaka yake.

التفاسير:

external-link copy
80 : 10

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ

Basi walipo kuja wachawi, Musa aliwaambia: Tupeni mnavyo tupa! info

Walipo hudhuria wachawi, na wakasimama mbele ya Musa kupambana naye kwa uchawi wao mbele ya watu, Musa aliwaambia: Leteni huo uchawi mlio nao!

التفاسير:

external-link copy
81 : 10

فَلَمَّآ أَلۡقَوۡاْ قَالَ مُوسَىٰ مَا جِئۡتُم بِهِ ٱلسِّحۡرُۖ إِنَّ ٱللَّهَ سَيُبۡطِلُهُۥٓ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُصۡلِحُ عَمَلَ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Walipo tupa, Musa alisema: Mliyo leta ni uchawi. Hakika Mwenyezi Mungu haitengenezi kazi ya waharibifu. info

Walipo tupa kamba zao na fimbo zao, Musa aliwaambia: Huo mlio fanya ni uchawi kweli, na Mwenyezi Mungu Subhanahu atauvunja kwa mkono wangu! Hakika Mwenyezi Mungu hawasahilishii mafisadi vitendo vyao vikawa vizuri na vyenye nafuu.

التفاسير:

external-link copy
82 : 10

وَيُحِقُّ ٱللَّهُ ٱلۡحَقَّ بِكَلِمَٰتِهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Na Mwenyezi Mungu huhakikisha Haki kwa maneno yake, hata wanga chukia wakosefu info

Ama Haki hapana shaka Mwenyezi Mungu atainusuru na ataiunga mkono kwa uwezo wake na hikima yake hata makafiri wakisaidiana katika kuichukia na kuipiga vita.

التفاسير:

external-link copy
83 : 10

فَمَآ ءَامَنَ لِمُوسَىٰٓ إِلَّا ذُرِّيَّةٞ مِّن قَوۡمِهِۦ عَلَىٰ خَوۡفٖ مِّن فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِمۡ أَن يَفۡتِنَهُمۡۚ وَإِنَّ فِرۡعَوۡنَ لَعَالٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَإِنَّهُۥ لَمِنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Basi hawakumuamini Musa isipo kuwa baadhi ya vijana vya kaumu yake, kwa kumwogopa Firauni na wakuu wao wasiwatese. Kwani hakika Firauni alikuwa jeuri katika nchi. Na kwa yakini alikuwa miongoni mwa walio pita kiasi. info

Na juu ya kudhihiri Ishara zote za kusadikisha Ujumbe, wale walio muamini Musa hawakuwa ila ni kikundi cha watu wachache tu katika kaumu ya Firauni. Waliamini juu ya kuwa wakiogopa asije Firauni na walio pamoja naye wakawaachisha waliyo yaamini. Jeuri za Firauni zilikuwa kubwa mno katika Misri! Hakika yeye ni katika walio pita upeo katika kutakabari na kujivuna.

التفاسير:

external-link copy
84 : 10

وَقَالَ مُوسَىٰ يَٰقَوۡمِ إِن كُنتُمۡ ءَامَنتُم بِٱللَّهِ فَعَلَيۡهِ تَوَكَّلُوٓاْ إِن كُنتُم مُّسۡلِمِينَ

Na Musa alisema: Enyi watu wangu! Ikiwa nyinyi mmemuamini Mwenyezi Mungu, basi mtegemeeni Yeye, ikiwa nyinyi ni Waislamu. info

Ama Musa aliwaambia Waumini kwa kuwawasa na kuwashajiisha: Enyi watu wangu! Ikiwa Imani imekwisha ingia nyoyoni mwenu kwa kumsafishia niya Mwenyezi Mungu, basi msimwogope yeyote mwenginewe. Nanyi msalimishie Yeye mambo yenu yote, na mtegemeeni Yeye, na muwe na yakini mwishoe atakunusuruni, ikiwa nyinyi mmethibiti katika Uislamu.

التفاسير:

external-link copy
85 : 10

فَقَالُواْ عَلَى ٱللَّهِ تَوَكَّلۡنَا رَبَّنَا لَا تَجۡعَلۡنَا فِتۡنَةٗ لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ

Wakasema: Tunamtegemea Mwenyezi Mungu. Ewe Mola wetu Mlezi! Usitufanye wenye kutiwa misukosuko na hao watu madhaalimu. info

Waumini wakasema: Tunamtegemea Mwenyezi Mungu peke yake. Kisha wakamwomba Mola wao Mlezi asiwatie katika mitihani na mateso ya makafiri.

التفاسير:

external-link copy
86 : 10

وَنَجِّنَا بِرَحۡمَتِكَ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na utuokoe kwa rehema yako na watu makafiri. info

Wakamwomba Mola wao Mlezi wakisema: Kwa vile ulivyo tumiminia neema na rehema, na kwa wingi wa rehema yako unayo sifika nayo, tuokoe na hawa watu wanao kataa, wenye kudhulumu.

التفاسير:

external-link copy
87 : 10

وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰ وَأَخِيهِ أَن تَبَوَّءَا لِقَوۡمِكُمَا بِمِصۡرَ بُيُوتٗا وَٱجۡعَلُواْ بُيُوتَكُمۡ قِبۡلَةٗ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na tukampelekea Musa na ndugu yake wahyi huu: Watengenezeeni majumba watu wenu katika Misri na zifanyeni nyumba zenu ndio mwahali mwa ibada, na mshike Swala, na wabashirie Waumini. info

Tukawafunulia Musa na nduguye Haruni kuwapa amri wafanye nyumba za kukaa watu wao katika nchi ya Misri, na watu wa Imani wenye kufuata wito wa Mwenyezi Mungu wazielekee nyumba hizo, na wawe wanashika Swala kwa sura ya ukamilifu. Na Waumini wanabashiriwa kheri!

التفاسير:

external-link copy
88 : 10

وَقَالَ مُوسَىٰ رَبَّنَآ إِنَّكَ ءَاتَيۡتَ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَأَهُۥ زِينَةٗ وَأَمۡوَٰلٗا فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا رَبَّنَا لِيُضِلُّواْ عَن سَبِيلِكَۖ رَبَّنَا ٱطۡمِسۡ عَلَىٰٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ وَٱشۡدُدۡ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَلَا يُؤۡمِنُواْ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ

Na Musa akasema: Mola wetu Mlezi! Hakika wewe umempa Firauni na wakuu wake mapambo na mali katika maisha ya dunia. Hivyo wanapoteza watu na Njia yako. Mola wetu Mlezi! Yafutilie mbali mali yao na zifunge nyoyo zao, wasiamini mpaka waione adhabu chungu. info

Walivyo shikilia makafiri katika kumfanyia inda Musa, alimwomba Mwenyezi Mungu kwa kusema: Ewe Mola Mlezi wangu! Hakika Wewe umempa Firauni na watukufu wake starehe za duniani, na mali, na wana, na utawala. Na matokeo ya neema hizi ni kupita kwao mipaka katika kupotea na kupoteza watu waache Njia ya Haki! Ewe Mwenyezi Mungu! Yafutilie mbali mali yao, na uwaache katika kiza cha nyoyo zao, wasijaaliwe kuipata Imani mpaka waione kwa macho adhabu iliyo chungu, ambayo ndiyo mwisho unao wangojea, ili wawe ni onyo kwa wengineo.

التفاسير: