قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - سەۋاھىلچە تەرجىمىسى. ئەلىي مۇھسىن بەرۋانىي قىلغان

بەت نومۇرى:close

external-link copy
51 : 28

۞ وَلَقَدۡ وَصَّلۡنَا لَهُمُ ٱلۡقَوۡلَ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Na sasa kwa yakini tumewafikishia Neno ili wapate kukumbuka. info

Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu amewateremshia Qur'ani kwa utungo, baadhi yake ikifuatia baadhi kwa mujibu wa inavyo takikana na hikima, na kulingana na ahadi, na maonyo, na hadithi, na mazingatio, ili wapate kupima na kuyaamini yaliomo ndani yake.

التفاسير:

external-link copy
52 : 28

ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِهِۦ هُم بِهِۦ يُؤۡمِنُونَ

Wale tulio wapa Kitabu kabla yake wanakiamini hiki. info

Wale ambao tuliwateremshia Taurati na Injili kabla ya kuteremka Qur'ani, na wakaviamini vitabu hivyo viwili, na wakasadiki yaliyo tajwa humo juu ya khabari za Muhammad na Kitabu chake, hao wanamuamini Muhammad na Kitabu chake.

التفاسير:

external-link copy
53 : 28

وَإِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِهِۦٓ إِنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّنَآ إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلِهِۦ مُسۡلِمِينَ

Na wanapo somewa wanasema: Tunaiamini. Hakika hii ni Haki inayo toka kwa Mola wetu Mlezi. Hakika sisi kabla yake tulikuwa ni Waislamu, tulio nyenyekea. info

Na hao wakisomewa Qur'ani hufanya haraka kutangaza Imani yao, na husema: Tumeyaamini hayo, kwani hayo ni Haki inayo toka kwa Mola wetu Mlezi; na sisi tulimjua Muhammad na Kitabu chake hata kabla ya kuteremka kwake, nasi tukanyenyekea kabla ya kusomwa kwake.

التفاسير:

external-link copy
54 : 28

أُوْلَٰٓئِكَ يُؤۡتَوۡنَ أَجۡرَهُم مَّرَّتَيۡنِ بِمَا صَبَرُواْ وَيَدۡرَءُونَ بِٱلۡحَسَنَةِ ٱلسَّيِّئَةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ يُنفِقُونَ

Basi hao watapewa ujira wao mara mbili kwa walivyo vumilia, na wakaondoa ubaya kwa wema, na wakatoa katika tuliyo waruzuku. info

Hao ambao waliiamini Qur'ani na yaliyo teremshwa kabla yake, watapewa malipo yao maradufu - kwa ajili ya kuvumilia kwao mateso yaliyo wapata kwa ajili ya Imani, na wakakhiari vitendo vyema, na wakayakabili maovu kwa kusamehe na ihsani, na wakatoa katika njia ya kheri kutokana na mali aliyo wapa Mwenyezi Mungu.

التفاسير:

external-link copy
55 : 28

وَإِذَا سَمِعُواْ ٱللَّغۡوَ أَعۡرَضُواْ عَنۡهُ وَقَالُواْ لَنَآ أَعۡمَٰلُنَا وَلَكُمۡ أَعۡمَٰلُكُمۡ سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡ لَا نَبۡتَغِي ٱلۡجَٰهِلِينَ

Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema: Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum, Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga. info

Na wanapo sikia upotovu wa wajinga hujitenga mbali nao, kwa kujiepusha na kuondoka, na husema: Sisi tuna a'mali yetu na hatuiachi, na nyinyi mna a'mali yenu ya upotovu na madhambi yake yapo juu yenu. Na sisi tunakuacheni na mambo yenu, kwani sisi hatupendi kusuhubiana na majaahili.

التفاسير:

external-link copy
56 : 28

إِنَّكَ لَا تَهۡدِي مَنۡ أَحۡبَبۡتَ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Kwa hakika wewe humwongoi umpendaye, lakini Mwenyezi Mungu humwongoa amtakaye. Na Yeye ndiye anawajua zaidi waongokao. info

Ewe Mtume! Hakika wewe una pupa sana kutaka hawa watu wako waongoke. Lakini wewe huwezi kumuingiza katika Uislamu kila umpendaye. Lakini Mwenyezi Mungu humwongoa kuendea Imani yule anaye mjua kuwa ameelekea uwongofu na ameukhiari. Na Yeye ndiye Mwenye kujua, wala hapana ajuaye zaidi kuliko Yeye, nani atakaye ingia katika safu za wenye kuongoka.

التفاسير:

external-link copy
57 : 28

وَقَالُوٓاْ إِن نَّتَّبِعِ ٱلۡهُدَىٰ مَعَكَ نُتَخَطَّفۡ مِنۡ أَرۡضِنَآۚ أَوَلَمۡ نُمَكِّن لَّهُمۡ حَرَمًا ءَامِنٗا يُجۡبَىٰٓ إِلَيۡهِ ثَمَرَٰتُ كُلِّ شَيۡءٖ رِّزۡقٗا مِّن لَّدُنَّا وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na wakasema: Tukiufuata uwongofu huu pamoja nawe tutanyakuliwa kutoka nchi yetu. Je! Kwani Sisi hatukuwaweka imara katika pahala patakatifu, penye amani, ambapo huletewa matunda ya kila aina kuwa ni riziki itokayo kwetu? Lakini wengi wao hawajui. info

Na washirikina wa Makka walimwambia Mtume s.a.w. kwa kujitolea udhuru kwa kubakia kwao katika dini yao: Tukikufuata wewe katika dini yako Waarabu watatutoa katika nchi yetu, na watatushinda katika utawala wetu. Na hakika wao ni waongo katika kutoa udhuru wao huo. Kwani Mwenyezi Mungu alikuwa kawaweka imara na madhubuti katika nchi yao. Na akaifanya nchi takatifu yenye amani, hawashambuliwi wala hawauwawi, na hali wao ni makafiri. Na wanaletewa matunda na kheri nyengine za aina nyingi, ambazo Mwenyezi Mungu anawaletea kutoka kila upande. Basi huwaje awaondolee amani, na awaachilie wakinyakuliwa wakiongeza juu ya utakatifu wa Nyumba ya Alkaaba Imani kumuamini Muhammmad! Lakini wengi wao hawaijui Haki. Lau kuwa wanaijua wasinge khofu kunyakuliwa.

التفاسير:

external-link copy
58 : 28

وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةِۭ بَطِرَتۡ مَعِيشَتَهَاۖ فَتِلۡكَ مَسَٰكِنُهُمۡ لَمۡ تُسۡكَن مِّنۢ بَعۡدِهِمۡ إِلَّا قَلِيلٗاۖ وَكُنَّا نَحۡنُ ٱلۡوَٰرِثِينَ

Na miji mingapi iliyo jifakharisha tumeiangamiza! Na hayo maskani yao hayakukaliwa tena baada yao, ila kwa uchache tu. Na Sisi ndio tumekuwa warithi wao. info

Watu hawa hawazingatii yaliyo wapata kaumu zilizo kwisha tangulia. Iliangamizwa miji ya walio ghurika na neema za Mwenyezi Mungu, na kisha wakazikanusha na wakamkanusha Mwenyezi Mungu. Na haya majumba yao yamekuwa matupu, magofu, hayafai kukaliwa ila nadra tu kwa wapita njia. Na yamebaki hayana mwenye kuyamiliki baada yao ila Mwenyezi Mungu Mwenye utukufu na ukarimu.

التفاسير:

external-link copy
59 : 28

وَمَا كَانَ رَبُّكَ مُهۡلِكَ ٱلۡقُرَىٰ حَتَّىٰ يَبۡعَثَ فِيٓ أُمِّهَا رَسُولٗا يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِنَاۚ وَمَا كُنَّا مُهۡلِكِي ٱلۡقُرَىٰٓ إِلَّا وَأَهۡلُهَا ظَٰلِمُونَ

Na Mola wako Mlezi haangamizi miji mpaka ampeleke Mtume katika miji yake mikuu awasomee Ishara zetu. Wala hatuiangamizi miji mpaka watu wake wawe madhaalimu. info

Na haikuwa katika hikima ya Mwenyezi Mungu Mtukufu - naye ndiye Mola wako Mlezi aliye kuumba na kukuteuwa - kuiangamiza miji mikubwa ila baada ya kuwapelekea watu wake Mtume mwenye miujiza iliyo wazi awasomee Kitabu kilicho teremshwa, na awabainishie sharia, na kisha wawe hawaamini. Wala Sisi hatuangamizi miji mikubwa ila wakiwa watu wake wanaendelea na udhalimu na uadui.

التفاسير: