[1] Aya hii inamaanisha kwamba kila mtu miongoni mwa Watu waliopewa Kitabu kama vile Wayahudi na Wakristo kabla ya kufa kwake humwamini Isa (Yesu) kwamba ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kwamba ni Mungu wala mototo wa Mungu. Kwani wakati anapokufa, huonyeshwa uhakika wa jambo hili. Kisha Siku ya Kiyama, Isa (Yesu) atakuwa shahidi dhidi yao kwamba aliwafikishia wito wa Mola wao Mlezi, lakini wakaupuuza na kwamba Wakristo waliubadilisha. (Tafsir At-Tahriir wat-Tanwiir, cha Ibn 'Aashuur)