[1] Waarabu wakati wa Jahiliyya kwa sababu ya ukatili wao na ugumu wao walikuwa hawawarithishi wanyonge kama vile wanawake na watoto. Na walikuwa wakiwagawia urithi wanaume wenye nguvu tu. Kwa sababu walikuwa wakidai kuwa wao tu ndio wanaoweza vita, na kunyang’anya, na kupora.
[1] Kiliekwa kiwango cha mwanamke kuwa ni nusu ya kiwango anachokirithi mwanamume kwa sababu mwanamke hutoshelezwa na jamii, au mumewe. Naye mwanamume huwa amejukumishwa kumlea mwanamke katika maisha. (Uadilifu wa Mirathi ndani ya Usilamu cha Mnaswab Abdulrahman)