ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
43 : 16

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ إِلَّا رِجَالٗا نُّوحِيٓ إِلَيۡهِمۡۖ فَسۡـَٔلُوٓاْ أَهۡلَ ٱلذِّكۡرِ إِن كُنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

Na hatukuwatuma kwa waliotangulia kabla yako, ewe Mtume, isipokuwa Mitume miongoni mwa wanaume, sio Malaika, tunaowaletea wahyi. Na iwapo nyinyi, enyi washirikina wa Kikureshi, hamliamini hilo, basi waulizeni waliopewa vitabu vilivyopita, watawapa habari kwamba Manabii walikuwa ni binadamu, mkiwa hamjui kwamba wao ni binadamu. Aya hii inakusanya kila suala kati ya masuala ya Dini, iwapo mtu hana ujuzi nalo amuulize anayelijua miongoni mwa wanavyuoni waliovama katika elimu. info
التفاسير:

external-link copy
44 : 16

بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَٱلزُّبُرِۗ وَأَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلذِّكۡرَ لِتُبَيِّنَ لِلنَّاسِ مَا نُزِّلَ إِلَيۡهِمۡ وَلَعَلَّهُمۡ يَتَفَكَّرُونَ

Na tuliwatuma Mitume waliotangulia wakiwa na dalili waziwazi na vitabu vya mbinguni. Na tumekuteremshia wewe, ewe Mtume, Qur’ani upate kuwafunulia watu maana yake na hukumu zake zilizofichika, na ili wapate kuizingatia na waongoke kwayo. info
التفاسير:

external-link copy
45 : 16

أَفَأَمِنَ ٱلَّذِينَ مَكَرُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ أَن يَخۡسِفَ ٱللَّهُ بِهِمُ ٱلۡأَرۡضَ أَوۡ يَأۡتِيَهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ

Je, wanajiaminisha wale makafiri wanaopanga vitimbi kwamba Mwenyezi Mungu Hatawadidimiza ndani ya ardhi kama Alivyomfanya Qarun au kwamba adhabu haitawafikia kutoka mahali wasipopadhania na wasipopatarajia info
التفاسير:

external-link copy
46 : 16

أَوۡ يَأۡخُذَهُمۡ فِي تَقَلُّبِهِمۡ فَمَا هُم بِمُعۡجِزِينَ

au adhabu haitawapata hali wakiwa wanazunguka kwenye safari zao na shughuli zao? Wao si wenye kumtangulia Mwenyezi Mungu wala kumponyoka wala kuokoka na adhabu Yake, kwani Yeye Ndiye Mwenye nguvu Ambaye hakuna chenye kumuelemea. info
التفاسير:

external-link copy
47 : 16

أَوۡ يَأۡخُذَهُمۡ عَلَىٰ تَخَوُّفٖ فَإِنَّ رَبَّكُمۡ لَرَءُوفٞ رَّحِيمٌ

Au Mwenyezi Mungu Awapatilize kwa upungufu wa mali na watu na matunda au katika hali ya kuogopa kwao Asiwatie mkononi. Kwani Mola wenu ni Mpole kwa waja Wake, ni Mwenye huruma kwao. info
التفاسير:

external-link copy
48 : 16

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَىٰ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ مِن شَيۡءٖ يَتَفَيَّؤُاْ ظِلَٰلُهُۥ عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَٱلشَّمَآئِلِ سُجَّدٗا لِّلَّهِ وَهُمۡ دَٰخِرُونَ

Je, kwani makafiri hawa wamekuwa vipofu wakawa hawaangalii vitu venye vivuli Alivyoviumba Mwenyezi Mungu, kama vile majabali na miti ambayo vivuli vyake vinapinduka, mara nyingine upande wa kulia na mara nyingine upande wa kushoto, kufuatia mwendo wa jua kipindi cha mchana na mwendo wa mwezi kipindi cha usiku.Vyote hivyo ni vyenye kuunyenyekea ukuu wa Mwenyezi Mungu na utukufu Wake. Navyo viko chini ya uendeshaji Wake, mipango Yake na utendeshaji nguvu Wake. info
التفاسير:

external-link copy
49 : 16

وَلِلَّهِۤ يَسۡجُدُۤ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ مِن دَآبَّةٖ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ وَهُمۡ لَا يَسۡتَكۡبِرُونَ

Na vinamsujudia Mwenyezi Mungu Peke Yake vyote vilivyo mbinguni na vilivyo ardhini, miongoni mwa vinavyotambaa. Na Malaika wanamsujudia Mwenyezi Mungu, na wao hawafanyi ujeuri kwa kukataa kumuabudu Yeye. Na Amewahusu Malaika kwa kuwataja baada ya kuwakusanya pamoja na viumbe wengine, kutokana na utukufu wao, ubora wao na wingi wa kuabudu kwao. info
التفاسير:

external-link copy
50 : 16

يَخَافُونَ رَبَّهُم مِّن فَوۡقِهِمۡ وَيَفۡعَلُونَ مَا يُؤۡمَرُونَ۩

Hao Malaika wanamuogopa Mola wao Ambaye Yuko juu yao kwa dhati Yake, utendeshaji nguvu Wake na ukamilifu wa sifa Zake, na wanafanya wanayoamrishwa ya kumtii Mwenyezi Mungu. Katika aya hii pana kuthibitisha sifa ya kuwa Mwenyezi Mungu Yuko juu ya viumbe vyake vyote, kama inavyonasibiana na utukufu Wake na ukamilifu Wake. info
التفاسير:

external-link copy
51 : 16

۞ وَقَالَ ٱللَّهُ لَا تَتَّخِذُوٓاْ إِلَٰهَيۡنِ ٱثۡنَيۡنِۖ إِنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ فَإِيَّٰيَ فَٱرۡهَبُونِ

Na Alisema Mwenyezi Mungu kuwaambia waja Wake, «Msiabudu waungu wawili, kwani muabudiwa wenu ni Mola Mmoja. Basi niogopeni mimi na sio mwingine asiyekuwa mimi.» info
التفاسير:

external-link copy
52 : 16

وَلَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلَهُ ٱلدِّينُ وَاصِبًاۚ أَفَغَيۡرَ ٱللَّهِ تَتَّقُونَ

Na ni vya Mwenyezi Mungu, Peke Yake, vyote vilivyoko mbinguni na ardhini, kwa kuviumba, kuvimiliki na kuviendesha. Na ibada inaelekezwa Kwake PekeYake, na pia kutiiwa na kutakaswa daima. Basi je, inafaa kwenu nyinyi mumuogope asiyekuwa Yeye na mumuabudu? info
التفاسير:

external-link copy
53 : 16

وَمَا بِكُم مِّن نِّعۡمَةٖ فَمِنَ ٱللَّهِۖ ثُمَّ إِذَا مَسَّكُمُ ٱلضُّرُّ فَإِلَيۡهِ تَجۡـَٔرُونَ

Na neema yoyote mliyonayo ya uongofu au afya ya mwili, ukunjufu wa riziki na watoto na yasiyokuwa hayo, inatoka kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake, Yeye Ndiye Mwenye kuwaneemesha nayo. Kisha yanapowapata magonjwa, matatizo na ukame, basi ni kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake mnalia kwa maombi. info
التفاسير:

external-link copy
54 : 16

ثُمَّ إِذَا كَشَفَ ٱلضُّرَّ عَنكُمۡ إِذَا فَرِيقٞ مِّنكُم بِرَبِّهِمۡ يُشۡرِكُونَ

Kisha Anapowaondolea matatizo na magonjwa, kitahamaki linatoka kundi la watu miongoni mwenu wakawa wanawafanya asiyekuwa Yeye kuwa ni washirika pamoja na Yeye na wategemewa. info
التفاسير: