ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
103 : 16

وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّهُمۡ يَقُولُونَ إِنَّمَا يُعَلِّمُهُۥ بَشَرٞۗ لِّسَانُ ٱلَّذِي يُلۡحِدُونَ إِلَيۡهِ أَعۡجَمِيّٞ وَهَٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيّٞ مُّبِينٌ

Na kwa hakika tunajua kuwa washirikina wanasema kwamba Nabii anapokea Qur’ani kutoka kwa kiumbe miongoni mwa wanadamu. Wamesema urongo! Kwani ulimi wa yule waliomsingizia kuwa amemfundisha Nabii, rehema na amani zimshukie, si wa Kiarabu usiyotasua, na hii Qur’ani ni kwa lugha ya Kiarabu, imefikia upeo wa ufafanuzi na ubainifu. info
التفاسير:

external-link copy
104 : 16

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ لَا يَهۡدِيهِمُ ٱللَّهُ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Hakika hao makafiri wasioiamini Qur’ani, Mwenyezi Mungu Hatawaelekeza kuipata haki, na Siku ya Akhera watakuwa na adhabu kali iumizayo. info
التفاسير:

external-link copy
105 : 16

إِنَّمَا يَفۡتَرِي ٱلۡكَذِبَ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِۖ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰذِبُونَ

Kwa hakika wanaozua urongo ni wale wasiomuamini Mwenyezi Mungu na aya Zake, na wao ndio warongo kwa neno lao hilo. Ama Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, anayemuamini Mola wake na kumnyenyekea, haiwezekani kwake yeye kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumsingizia Asiyoyasema. info
التفاسير:

external-link copy
106 : 16

مَن كَفَرَ بِٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ إِيمَٰنِهِۦٓ إِلَّا مَنۡ أُكۡرِهَ وَقَلۡبُهُۥ مُطۡمَئِنُّۢ بِٱلۡإِيمَٰنِ وَلَٰكِن مَّن شَرَحَ بِٱلۡكُفۡرِ صَدۡرٗا فَعَلَيۡهِمۡ غَضَبٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Hakika wanaozua urongo ni wanaotamka neno la ukafiri na akaritadi baada ya kuamini. Hao itawashukia wao hasira kutoka kwa Mwenyezi Mungu, isipokuwa yule aliyelazimishwa kutamaka maneno ya ukafiri na akayatamka kwa kuchelea kuangamia, hali moyo wake umejikita kwenye Imani, basi huyo hana lawama. Lakini mwenye kutamka ukafiri na moyo wake ukatulia juu yake, hao watashukiwa na hasira kali kutoka kwa Mwenyezi Munngu na watapata adhabu kubwa. info
التفاسير:

external-link copy
107 : 16

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمُ ٱسۡتَحَبُّواْ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا عَلَى ٱلۡأٓخِرَةِ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Hiyo ni kwa sababu ya kuchagua kwao dunia na pambo lake na kuifanya kwao hiyo dunia kuwa ni bora kuliko Akhera na malipo yake na kwamba Mwenyezi Mungu Hawaongozi makafiri wala hawaelekezi kwenye haki na usawa. info
التفاسير:

external-link copy
108 : 16

أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ طَبَعَ ٱللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ وَسَمۡعِهِمۡ وَأَبۡصَٰرِهِمۡۖ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡغَٰفِلُونَ

Hao ndio wale ambao Mwenyezi Mungu Amewapiga muhuri nyoyo zao kwa ukafiri na ufadhilishaji dunia juu ya Akhera, hazitafikiwa na nuru ya uongofu, na Amewafanya viziwi masikio yao kutozisikia aya za Mwenyezi Mungu , kusikia kwa kuzingatia, na Amewafanya vipofu macho yao wasizione hoja zinazojulisha uungu wa Mwenyezi Mungu , na hao ndio wenye kughafilika na ile adhabu Aliyowaandalia Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
109 : 16

لَا جَرَمَ أَنَّهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Ni kweli kabisa kwamba wao, huko Akhera, ndio wenye hasara wenye kuangamia, waliotumia maisha yao kwa mambo yaliyopelekea kuadhibiwa na kuangamizwa. info
التفاسير:

external-link copy
110 : 16

ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا فُتِنُواْ ثُمَّ جَٰهَدُواْ وَصَبَرُوٓاْ إِنَّ رَبَّكَ مِنۢ بَعۡدِهَا لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Kisha Mola wako, kwa wale waliofanywa wanyonge ndani ya Makkah na wakaadhibiwa na washirikina mpaka wakakubali matendo yao kijuujuu, wakawafitini kwa kutamka yanayowaridhi, na hali nyoyo zao zimetulia katika Imani, na ilipowezekana kwao kujiokoa waligura kwenda Madina kisha wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na wakavumilia mashaka ya majukumu, hakika Mola wako , baada ya kutubia kwao ni Mwenye kuwasamehe , ni Mwenye kuwarehemu. info
التفاسير: