ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
87 : 12

يَٰبَنِيَّ ٱذۡهَبُواْ فَتَحَسَّسُواْ مِن يُوسُفَ وَأَخِيهِ وَلَا تَاْيۡـَٔسُواْ مِن رَّوۡحِ ٱللَّهِۖ إِنَّهُۥ لَا يَاْيۡـَٔسُ مِن رَّوۡحِ ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡقَوۡمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ

Ya’qūb akasema, «Enyi wanangu! Rudini Misri mpeleleze habari za Yūsuf na ndugu yake , wala msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu, kwani hawakati tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu isipokuwa wenye kuukanusha uwezo Wake, wenye kumkataa Yeye.» info
التفاسير:

external-link copy
88 : 12

فَلَمَّا دَخَلُواْ عَلَيۡهِ قَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡعَزِيزُ مَسَّنَا وَأَهۡلَنَا ٱلضُّرُّ وَجِئۡنَا بِبِضَٰعَةٖ مُّزۡجَىٰةٖ فَأَوۡفِ لَنَا ٱلۡكَيۡلَ وَتَصَدَّقۡ عَلَيۡنَآۖ إِنَّ ٱللَّهَ يَجۡزِي ٱلۡمُتَصَدِّقِينَ

Wakaenda Misri. Na walipoingia kwa Yūsuf walisema, «Ewe kiongozi, tumepatikana na ukame na ukavu, na tumekujia na thamani isiyokuwa nzuri na iliyo chache, basi tupe kwa hii thamani kiasi ulichokuwa ukitupa kabla kwa thamani nzuri. Na utunuku kwa kukubali kupokea thamani hii mbaya iliyo chache, na utulegezee juu ya hiyo thamani, hakika Mwenyezi Mungu Anawalipa wema wale wenye kuwasaidia wahitaji kwa mali zao.» info
التفاسير:

external-link copy
89 : 12

قَالَ هَلۡ عَلِمۡتُم مَّا فَعَلۡتُم بِيُوسُفَ وَأَخِيهِ إِذۡ أَنتُمۡ جَٰهِلُونَ

Aliposika maneno yao alilainika juu yao, akajitambulisha kwao na akasema, «Je, mnayakumbuka mabaya mliyomfanyia Yūsuf na ndugu yake mlipokuwa katika hali ya kutojua vile matendo yenu yataishia?» info
التفاسير:

external-link copy
90 : 12

قَالُوٓاْ أَءِنَّكَ لَأَنتَ يُوسُفُۖ قَالَ أَنَا۠ يُوسُفُ وَهَٰذَآ أَخِيۖ قَدۡ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَآۖ إِنَّهُۥ مَن يَتَّقِ وَيَصۡبِرۡ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Wakasema, «Je, kwa kweli wewe ni Yūsuf?»Akasema, «Ndio. Mimi ni Yūsuf na huyu ni ndugu yangu. Mwenyezi Mungu Ametukirimu, akatukusanya pamoja baada ya kupambanukana. Hakika Mwenye kumcha Mwenyezi Mungu na akavumilia shida, Mwenyezi Mungu hamuondolei malipo ya wema wake, Hakika atamlipa malipo mema zaidi.» info
التفاسير:

external-link copy
91 : 12

قَالُواْ تَٱللَّهِ لَقَدۡ ءَاثَرَكَ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَإِن كُنَّا لَخَٰطِـِٔينَ

Wakasema, «Tunaapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba Mwenyezi Mungu amekutukuza juu yetu na Amekufanya bora kwa elimu, upole na utukufu, ingawa sisi ni wakosa kwa yale tuliyokufanyia wewe na ndugu yako kwa kukusudia.» info
التفاسير:

external-link copy
92 : 12

قَالَ لَا تَثۡرِيبَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡيَوۡمَۖ يَغۡفِرُ ٱللَّهُ لَكُمۡۖ وَهُوَ أَرۡحَمُ ٱلرَّٰحِمِينَ

Yūsuf akawaamia, «Hamlaumiwi leo; Mwenyezi Mungu Atawasamehe. Na Yeye ni Mwenye huruma zaidi ya wenye huruma kwa anayetubia dhambi zake na akarejea kwenye utiifu Kwake.» info
التفاسير:

external-link copy
93 : 12

ٱذۡهَبُواْ بِقَمِيصِي هَٰذَا فَأَلۡقُوهُ عَلَىٰ وَجۡهِ أَبِي يَأۡتِ بَصِيرٗا وَأۡتُونِي بِأَهۡلِكُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na alipowauliza kuhusu baba yake, walimpa habari ya kupofuka macho yake kwa kumlilia. Akawaambia, «Rudini kwa baba yenu mkiwa na kanzu yangu hii, mtupieni usoni mwake na macho yake yatarudi kuona, kisha waleteni kwangu watu wenu wote.» info
التفاسير:

external-link copy
94 : 12

وَلَمَّا فَصَلَتِ ٱلۡعِيرُ قَالَ أَبُوهُمۡ إِنِّي لَأَجِدُ رِيحَ يُوسُفَۖ لَوۡلَآ أَن تُفَنِّدُونِ

Msafara ulipotoka nchi ya Misri wakiwa na ile kanzu, Ya’qūb alisema kuwaambia wale waliokuwa na yeye, «Mimi nasikia harufu ya Yūsuf, ingawa nyinyi mtanifanya ni mchache wa akili, mtanicheza shere na mtadai kwamba maneno haya yametoka kwangu bila ya fahamu.» info
التفاسير:

external-link copy
95 : 12

قَالُواْ تَٱللَّهِ إِنَّكَ لَفِي ضَلَٰلِكَ ٱلۡقَدِيمِ

Waliohudhuria hapo kwake walisema, «Tunaapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba wewe bado uko kwenye telezo lako la zamani la kumpenda Yūsuf na kwamba wewe hutamsahau.» info
التفاسير: