ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
79 : 12

قَالَ مَعَاذَ ٱللَّهِ أَن نَّأۡخُذَ إِلَّا مَن وَجَدۡنَا مَتَٰعَنَا عِندَهُۥٓ إِنَّآ إِذٗا لَّظَٰلِمُونَ

Yūsuf akasema, «Tunaomba hifadhi ya Mwenyezi Mungu na himaya Yake, tusiwe ni wenye kumchukua yoyote isipokuwa yule ambaye tulipata kipimio chetu kwake, kama mlivyoamua wenyewe. Kwani sisi tukifanya hayo ambayo mnataka tutakuwa ni miongoni mwa wanaohesabiwa kuwa ni waonevu.» info
التفاسير:

external-link copy
80 : 12

فَلَمَّا ٱسۡتَيۡـَٔسُواْ مِنۡهُ خَلَصُواْ نَجِيّٗاۖ قَالَ كَبِيرُهُمۡ أَلَمۡ تَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ أَبَاكُمۡ قَدۡ أَخَذَ عَلَيۡكُم مَّوۡثِقٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَمِن قَبۡلُ مَا فَرَّطتُمۡ فِي يُوسُفَۖ فَلَنۡ أَبۡرَحَ ٱلۡأَرۡضَ حَتَّىٰ يَأۡذَنَ لِيٓ أَبِيٓ أَوۡ يَحۡكُمَ ٱللَّهُ لِيۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلۡحَٰكِمِينَ

Walipokata tamaa ya kukubali kwake matakwa yao, walikaa kando na watu wakawa wanashauriana baina yao. Mkubwa wao kimyaka alisema, «Je hamjui kuwa baba yenu alichukuwa kwenu ahadi ya mkazo kuwa mtamrudisha ndugu yenu mpaka mshindwe, Na kabla ya tukio hili mlifanya kasoro kuhusu Yūsuf na mkamzungukia kinyume kwa hiana. Kwa hivyo sitaondoka kwenye ardhi ya Misri mpaka baba yangu aniamuru niondoke au Mola wangu Anihukumie niondoke na niweze kumchukua ndugu yangu. Na Mwenyezi Mungu ni Bora wa wanaohukumu na ni muadilifu zaidi wa wenye kutoa uamuzi baina ya watu. info
التفاسير:

external-link copy
81 : 12

ٱرۡجِعُوٓاْ إِلَىٰٓ أَبِيكُمۡ فَقُولُواْ يَٰٓأَبَانَآ إِنَّ ٱبۡنَكَ سَرَقَ وَمَا شَهِدۡنَآ إِلَّا بِمَا عَلِمۡنَا وَمَا كُنَّا لِلۡغَيۡبِ حَٰفِظِينَ

Rudini nyinyi kwa baba yenu, mpeni habari ya yaliyojiri na mwambieni, «Mwano Binyamin ameiba, na hatukushuhudia isipokuwa kwa lile ambalo tuna uhakika nalo. Kwani tumekiona kipimio kwenye mzigo wake, na hatukuwa na ujuzi wa ghaibu kuwa yeye ataiba tulipokuahidi kumrudisha.» info
التفاسير:

external-link copy
82 : 12

وَسۡـَٔلِ ٱلۡقَرۡيَةَ ٱلَّتِي كُنَّا فِيهَا وَٱلۡعِيرَ ٱلَّتِيٓ أَقۡبَلۡنَا فِيهَاۖ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ

Waliporejea, wakampa habari baba yao yaliyotokea na wakamtaka ahakikishe yale waliyomwambia wakisema, «Na waulize, ewe baba yetu, watu wa Misri na wale waliokuwa pamoja na sisi kwenye msafara tuliorudi nao. Na sisi ni wakweli kwa yale tuliyokusimulia.» info
التفاسير:

external-link copy
83 : 12

قَالَ بَلۡ سَوَّلَتۡ لَكُمۡ أَنفُسُكُمۡ أَمۡرٗاۖ فَصَبۡرٞ جَمِيلٌۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَأۡتِيَنِي بِهِمۡ جَمِيعًاۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَلِيمُ ٱلۡحَكِيمُ

Akawaambia, «Bali nafsi zenu zinazoamrisha mabaya ndizo zilizowapambia njama mlizozipanga, kama mlivyomfanyia Yūsuf. Basi uvumilivu wangu ni uvumilivu mzuri usio na babaiko wala ulalamishi. Kwani huenda Mwenyezi Mungu Akanirudishia wanangu watatu: Yūsuf, nduguye wa kwa baba na mama na ndugu yao mkubwa aliyebaki nyuma kwa sababu ya ndugu yake. Hakika Yeye Ndiye Mjuzi wa hali yangu , Ndiye Mwenye hekima katika uendeshaji mamboWake.» info
التفاسير:

external-link copy
84 : 12

وَتَوَلَّىٰ عَنۡهُمۡ وَقَالَ يَٰٓأَسَفَىٰ عَلَىٰ يُوسُفَ وَٱبۡيَضَّتۡ عَيۡنَاهُ مِنَ ٱلۡحُزۡنِ فَهُوَ كَظِيمٞ

Ya’qūb akawapa mgongo na asishughulike nao, ukiwa moyo wake umeingia dhiki kwa maneno waliyoyasema, na akasema, «Ewe hasara yangu juu ya Yūsuf!» Na macho yake yakawa meupe, kwa kuondoka weusi wake kwa masikitiko mengi. Moyo wake umejaa tele huzuni, lakini alikuwa akiificha sana. info
التفاسير:

external-link copy
85 : 12

قَالُواْ تَٱللَّهِ تَفۡتَؤُاْ تَذۡكُرُ يُوسُفَ حَتَّىٰ تَكُونَ حَرَضًا أَوۡ تَكُونَ مِنَ ٱلۡهَٰلِكِينَ

Wanawe wakasema, «Tunaapa kwa Mwenyezi Mungu, utendelea kumkumbuka Yūsuf na kuwa na huzuni nyingi juu yake mpaka ukaribie kuangamia au uangamie kikweli, basi ipumzishe nafsi yako.» info
التفاسير:

external-link copy
86 : 12

قَالَ إِنَّمَآ أَشۡكُواْ بَثِّي وَحُزۡنِيٓ إِلَى ٱللَّهِ وَأَعۡلَمُ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Ya’qūb akasema kuwajibu, «Simuonyeshi hamu yangu na masikitiko yangu isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Yeye Ndiye Mwenye kuondoa shida na matatizo. Na ninayajua, kuhusu rehema ya Mwenyezi Mungu na maliwazo Yake, mambo msiyoyajua.» info
التفاسير: