Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯

external-link copy
12 : 6

قُل لِّمَن مَّا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ قُل لِّلَّهِۚ كَتَبَ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۚ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Ni ya nani mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake?» Sema, «Ni ya Mwenyezi Mungu. Na kama mnavyolikubali hilo na kulijua, basi muabuduni Yeye Peke Yake. Mwenyezi Mungu Amechukua ahadi juu ya nafsi Yake kurehemu, Hatawaangusiliza waja Wake kwa kuwatesa. Kwa hakika Atawakusanya nyinyi kwenye Siku ya Kiyama ambayo haina shaka ili mhesabiwe na mlipwe. Wale waliomshirikisha Mwenyezi Mungu wamejiangamiza nafsi zao; wao hawampwekeshi Mwenyezi Mungu wala hawaiamini ahadi Yake ya Pepo na Moto na hawaukubali unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,. info
التفاسير: