Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯

Số trang:close

external-link copy
58 : 5

وَإِذَا نَادَيۡتُمۡ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ ٱتَّخَذُوهَا هُزُوٗا وَلَعِبٗاۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَوۡمٞ لَّا يَعۡقِلُونَ

Na anapoadhini mwadhini wenu, enyi Waumini, kuita watu kwenye Swala, Mayahudi, Wanaswara na washirikina wanafanya shere na kuukejeli mwito wenu wa hiyo Swala. Hii ni kwa sababu ya ujinga wao wa kutomjua Mola wao na kwa kuwa wao hawajui uhakika wa ibada. info
التفاسير:

external-link copy
59 : 5

قُلۡ يَٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ هَلۡ تَنقِمُونَ مِنَّآ إِلَّآ أَنۡ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡنَا وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلُ وَأَنَّ أَكۡثَرَكُمۡ فَٰسِقُونَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia hao wanaofanya shere kati ya hao waliiopewa Kitabu, «Mnalolikuta kuwa ni jambo la kutukanika au ni la aibu, hilo kwetu ni zuri kusifika nalo. Na hilo ni lile la kumuamini kwetu Mwenyezi Mungu na vitabu Vyake vilivyoteremshwa kwetu na waliokuwa kabla yetu na kuamini kwetu kwamba wengi wenu muko nje ya njia ilyo nyofu.» info
التفاسير:

external-link copy
60 : 5

قُلۡ هَلۡ أُنَبِّئُكُم بِشَرّٖ مِّن ذَٰلِكَ مَثُوبَةً عِندَ ٱللَّهِۚ مَن لَّعَنَهُ ٱللَّهُ وَغَضِبَ عَلَيۡهِ وَجَعَلَ مِنۡهُمُ ٱلۡقِرَدَةَ وَٱلۡخَنَازِيرَ وَعَبَدَ ٱلطَّٰغُوتَۚ أُوْلَٰٓئِكَ شَرّٞ مَّكَانٗا وَأَضَلُّ عَن سَوَآءِ ٱلسَّبِيلِ

Sema, ewe Nabii, kuwaambia Waumini, «Je, niwajulishe yule ambaye atalipwa, Siku ya Kiyama, malipo makali zaidi kuliko hawa wenye kutoka nje ya utiifu?» Hao ni waliowatangulia wao ambao Mwenyezi Mungu Aliwafukuza kwenye rehema Yake, Aliwakasirikia na akawageuza maumbile yao Akawafanya manyani na ngurue kwa kuasi kwao, kuzua kwao urongo na kuwa na kiburi, kama ambavyo walikuwa kati yao wenye kuabudu Tāghūt (kila kinachoabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu nacho kimeridhika). Hao, ni pabaya mno mahali pao huko Akhera; na harakati zao ulimwenguni zilikosa mwelekeo wa njia ya sawa. info
التفاسير:

external-link copy
61 : 5

وَإِذَا جَآءُوكُمۡ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَقَد دَّخَلُواْ بِٱلۡكُفۡرِ وَهُمۡ قَدۡ خَرَجُواْ بِهِۦۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا كَانُواْ يَكۡتُمُونَ

Na wakiwajia nyinyi, enyi Waumini, wanafiki wa Kiyahudi husema, «Tumeamini,» na hali wao wako ukafirini na wanaendelea nao : hakika wameingia kwenu wakiwa na ukafiri wanaouitakidi ndani ya nyoyo zao, kisha wametoka wakiwa bado wanaushikilia ukafiri huo. Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa siri zao hata wakionyesha kinyume cha hivyo. info
التفاسير:

external-link copy
62 : 5

وَتَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَأَكۡلِهِمُ ٱلسُّحۡتَۚ لَبِئۡسَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Na utawaona, ewe Mtume, wengi miongoni mwa Mayahudi wanayakimbilia maasia ya kusema urongo, uzushi, kuzifanyia uadui hukumu za Mwenyezi Mungu na kula mali ya watu kinyume na haki. Ni maovu mno matendo yao na uadui wao. info
التفاسير:

external-link copy
63 : 5

لَوۡلَا يَنۡهَىٰهُمُ ٱلرَّبَّٰنِيُّونَ وَٱلۡأَحۡبَارُ عَن قَوۡلِهِمُ ٱلۡإِثۡمَ وَأَكۡلِهِمُ ٱلسُّحۡتَۚ لَبِئۡسَ مَا كَانُواْ يَصۡنَعُونَ

Mbona viongozi wao na wasomi wao hawawakatazi hawa ambao wanayakimbilia madhambi na kufanya uadui, kusema urongo, uzushi na kula mali za watu kinyume na haki? Ni kiovu mno walichokifanya, walipoacha kukataza munkar (mabaya). info
التفاسير:

external-link copy
64 : 5

وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ يَدُ ٱللَّهِ مَغۡلُولَةٌۚ غُلَّتۡ أَيۡدِيهِمۡ وَلُعِنُواْ بِمَا قَالُواْۘ بَلۡ يَدَاهُ مَبۡسُوطَتَانِ يُنفِقُ كَيۡفَ يَشَآءُۚ وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم مَّآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَ طُغۡيَٰنٗا وَكُفۡرٗاۚ وَأَلۡقَيۡنَا بَيۡنَهُمُ ٱلۡعَدَٰوَةَ وَٱلۡبَغۡضَآءَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ كُلَّمَآ أَوۡقَدُواْ نَارٗا لِّلۡحَرۡبِ أَطۡفَأَهَا ٱللَّهُۚ وَيَسۡعَوۡنَ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَسَادٗاۚ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Mwenyezi Mungu Anamjulisha Mtume Wake sehemu ya makosa ya Mayahudi, kitu walichokuwa wakikizungumza kwa siri baina yao, kuwa wao walisema, «Mkono wa Mwenyezi Mungu umefungwa kutotenda mema, Ametufanyia ubahili riziki kwa kutubania na kutotupanulia.» Walisema hilo wakati walipopatwa na ukame na ukosefu wa mvua. Mikono yao ndiyo iliyofungwa, kwa maana: mikono yao imezuiliwa kutenda mema, na Mwenyezi Mungu Amewafukuza kutoka kwenye rehema Yake kwa sababu ya neno lao. Mambo sivyo kama wanavyomzulia Mola wao, bali mikono Yake miwili imekunjuliwa, haikuzuiliwa wala hakuna pingamizi ya kumzuia kutoa. Kwani Yeye ni Mpaji, ni Karimu, Anatoa kulingana na hekima na yale yenye maslahi kwa waja. Kwenye aya hii kuna thibitisho la sifa ya Mikono miwili kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasita na kila sifa ya upungufu na kutukuka, kama inavyolingana na Yeye, pasi na kufananisha wala kueleza namna ilivyo. Lakini wao watazidi ukiukaji mipaka na ukafiri kwa sababu ya chuki yao na uhasidi wao kwa kuwa Mwenyezi Mungu Amekuchagua wewe kwa utume. Mwenyezi Mungu Anayatolea habari makundi ya Mayahudi kwamba wao wataendelea, mpaka Siku ya Kiyama, kufanyiana uadui wao kwa wao na kuchukiana wao kwa wao. Kila wanapopanga njama ya kuwafanyia vitimbi Waislamu, kwa kuzusha fitina na kuuwasha moto wa vita, Mwenyezi Mungu Anavikomesha vitimbi vyao na kuutenganisha mkusanyiko wao. Na Mayahudi hawataacha kuendelea kumuasi Mwenyezi Mungu kwa kufanya yanayoleta uharibifu na misukosuko katika ardhi. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Hawapendi waharibifu. info
التفاسير: