قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - سەۋاھىلچە تەرجىمىسى. ئەلىي مۇھسىن بەرۋانىي قىلغان

At-Tur

external-link copy
1 : 52

وَٱلطُّورِ

Naapa kwa mlima wa T'ur! info

Ninaapa kwa mlima wa T'ur ulioko katika Sinai. Kwenye mlima huo ndio Nabii Musa a.s. alisemezwa.

التفاسير:

external-link copy
2 : 52

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na Kitabu kilicho andikwa . info

Ninaapa kwa mlima wa T'ur ulioko katika Sinai. Kwenye mlima huo ndio Nabii Musa a.s.

التفاسير:

external-link copy
3 : 52

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika ngozi iliyo kunjuliwa! info

Kilicho andikwa katika kurasa zilio nyepesi kuzisoma,

التفاسير:

external-link copy
4 : 52

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na kwa Nyumba iliyo jengwa! info

Na kwa Nyumba iliyo jengwa kwa sababu ya wenye kuizunguka kwa ibada na wenye kusimama na kurukuu na kusujudu kwa Swala,

التفاسير:

external-link copy
5 : 52

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na kwa dari iliyo nyanyuliwa! info

Na naapa kwa mbingu iliyo nyanyuliwa bila ya nguzo, na bahari iliyo jaa.

التفاسير:

external-link copy
6 : 52

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na kwa bahari iliyo jazwa! info

Na bahari iliyo jaa.

التفاسير:

external-link copy
7 : 52

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea. info

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi waliyo ahidiwa makafiri bila ya shaka itawateremkia hapana hivi wala hivi.

التفاسير:

external-link copy
8 : 52

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia. info

Hapana wa kuizuia isiwafikilie.

التفاسير:

external-link copy
9 : 52

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso! info

Siku mbingu itapo tikisika kwa mtikiso mkubwa.

التفاسير:

external-link copy
10 : 52

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa. info

Na milima itapo ng'oka kutoka hapo ilipo kwa kuonekana khasa.

التفاسير:

external-link copy
11 : 52

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha, info

Maangamio makubwa yatawapata siku hiyo hao wanao kadhibisha Haki.

التفاسير:

external-link copy
12 : 52

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi. info

Ambao katika upotovu ndio mchezo wao wanapo chezea.

التفاسير:

external-link copy
13 : 52

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu, info

Siku watakapo sukumwa kuingizwa Motoni kwa nguvu.

التفاسير:

external-link copy
14 : 52

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha! info

Wataambiwa: Huu ndio Moto mlio kuwa mkiukanusha duniani.

التفاسير: