Yeye ndiye Mwenyezi Mungu aliye dhamini kutimiza Nuru yake kwa kumtuma Mtume wake, Muhammad s.a.w. na hoja zilizo wazi, na Dini ya Haki, Uislamu, ipate kutukuka Dini hii juu ya dini zote zilizo tangulia, ijapo kuwa washirikina watakasirika. Mwenyezi Mungu ataipa ushindi tu, wakitaka wasitake.