[1] Na Suleiman amani iwe juu yake alipokufa, mashetani waliandika aina za uchawi katika kitabu, kisha wakakipiga kwa muhuri wa Suleiman. Kisha wakakizika chini ya kiti chake. Baadaye Wana wa Israili wakakikuta na wakasema: Ufalme wa Suleiman haukuwa isipokuwa kwa haya. Kwa hivyo, wakaeneza uchawi katika watu. (Tafsir Al-Baqaa'ii)