[1] Ama herufi za mkato mwanzoni mwa sura mbalimbali. Lililo salama zaidi kuhusiana nazo ni kukaa kimya na kutoziingilia maana zake bila ya dalili ya Kisheria, pamoja na kuwa na yakini kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuziteremsha bure, bali kwa hekima tusiyoijua. (Tafsir As-Sa'dii)
[1] Na kwa sababu shaka ni kusitasita kati ya mambo, basi kitu chenye shaka hakiwezi kumuongoa mtu. Na kwa sababu sifa ya Qur-aani ni kwamba haina shaka yoyote, basi ikalazimu kwamba ni yenye kuongoa. Ndiyo maana Mwenyezi Mungu akasema: "Ni uwongofu kwa wachamungu" peke yao. Kwa sababu, wasiokuwa wachamungu na wakaidi hawakosi kuwa na shaka katika jambo hata kama halina shaka yoyote. (Tafsir Al-Baqa'ii)
[1] Na alitumia neno “min (katika)” linalomaanisha baadhi (ya kitu), ili awatanabahishe kuwa yeye kwa hakika hakuta kutoka kwao isipokuwa sehemu ndogo kutoka kwa mali zao, ambayo haina madhara kwao wala uzito wowote, bali wao wanafaidika kwa kuitoa, na pia ndugu zao wanafaidika kwayo.
[1] Kwa sababu Qur-ani ndio uwongofu wao, limetumika neno "juu" ili kuifananisha hali ya kuimarika kwa Waumini katika uwongofu na uthabiti wao juu yake; na kujaribu kwao kuuongeza na kutembea katika njia za heri. Na mwonekano wa (mtu) aliyepanda kipando (kama farasi) katika kuwa kwake juu ya kipando hicho, na uwezo wake wa kukiendesha na kukifanya kuwa kitiifu. (Tafsir At-Tahrir Wat-tanwiir cha Ibn 'Aashuur)