ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាស្វាហុីលី - អាលី ម៉ុហសុីន អាល់ពើវ៉ានី

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
107 : 10

وَإِن يَمۡسَسۡكَ ٱللَّهُ بِضُرّٖ فَلَا كَاشِفَ لَهُۥٓ إِلَّا هُوَۖ وَإِن يُرِدۡكَ بِخَيۡرٖ فَلَا رَآدَّ لِفَضۡلِهِۦۚ يُصِيبُ بِهِۦ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۚ وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ

Na Mwenyezi Mungu akikugusisha madhara, basi hapana wa kukuondolea ila Yeye. Na akikutakia kheri, basi hapana awezaye kurudisha fadhila yake.Huifikisha kwa amtakaye katika waja wake, na Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. info

Ewe Nabii! Yakikusibu madhara kutoka kwa Mwenyezi Mungu, hapana wa kuyaondoa ila Yeye. Na akikujaalia kheri hapana anaye weza kukunyima yeyote. Kwani yeye anagawa kheri kuwapa waja wake kwa fadhila yake. Na Yeye Subhanahu ni Mkunjufu wa maghfira, Mkuu wa rehema.

التفاسير:

external-link copy
108 : 10

قُلۡ يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنِ ٱهۡتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهۡتَدِي لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيۡهَاۖ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ

Sema: Enyi watu! Haki imekwisha kukujieni kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi anaye ongoka anaongoka kwa faida ya nafsi yake, na anaye potea anapotea kwa khasara ya nafsi yake. Na mimi si mwakilishi juu yenu. info

Ewe Mtume! Fikisha wito wa Mwenyezi Mungu kwa watu wote! Na waambie: Enyi watu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteremshieni Sharia ya Haki kutokana naye. Anaye taka kuongoka basi afanye haraka. Kwani faida ya uwongofu wake utamrejea mwenyewe. Na mwenye kushikilia upotovu utamuangukia mwenyewe. Na mimi sikuwakilishwa nikulazimisheni muamini, wala kukutawalini.

التفاسير:

external-link copy
109 : 10

وَٱتَّبِعۡ مَا يُوحَىٰٓ إِلَيۡكَ وَٱصۡبِرۡ حَتَّىٰ يَحۡكُمَ ٱللَّهُۚ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلۡحَٰكِمِينَ

Na wewe fuata yanayo funuliwa kwako kwa wahyi. Na vumilia mpaka Mwenyezi Mungu ahukumu, na Yeye ndiye mbora wa mahakimu. info

Ewe Mtume! Thibiti juu ya Dini ya Haki. Na fuata wahyi ulio teremshiwa, nawe uwe na subira kwa maudhi yanayo kufika kwa ajili ya Njia ya Da'wa (Wito), mpaka Mwenyezi Mungu ahukumu baina yako na wao, kwa vile alivyo kuahidi kuwa atawapa ushindi Waumini, na watahizika makafiri. Na Yeye ndiye mbora wa mahakimu.

التفاسير: