ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស

លេខ​ទំព័រ:close

external-link copy
21 : 9

يُبَشِّرُهُمۡ رَبُّهُم بِرَحۡمَةٖ مِّنۡهُ وَرِضۡوَٰنٖ وَجَنَّٰتٖ لَّهُمۡ فِيهَا نَعِيمٞ مُّقِيمٌ

Hakika Waumini hawa waliohama wana habari njema kutoka kwa Mola wao za rehema kunjufu na radhi ambayo hapatakuwa na hasira baada yake; na mwisho wao ni kwenda kwenye mabustani ya Pepo ya milele na neema zisizokoma. info
التفاسير:

external-link copy
22 : 9

خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًاۚ إِنَّ ٱللَّهَ عِندَهُۥٓ أَجۡرٌ عَظِيمٞ

Hali ya kukaa kwenye mabustani hayo ya Pepo neema hizo kikao kisicho na kikomo. Na hayo ni malipo ya yale waliyoyatanguliza ya utiifu na vitendo vyema katika maisha yao ya ulimwenguni. Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ana malipo makubwa kwa aliyeamini na akafanya mema kwa kuzifuata amri Zake na kuyaepuka Makatazo Yake. info
التفاسير:

external-link copy
23 : 9

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَتَّخِذُوٓاْ ءَابَآءَكُمۡ وَإِخۡوَٰنَكُمۡ أَوۡلِيَآءَ إِنِ ٱسۡتَحَبُّواْ ٱلۡكُفۡرَ عَلَى ٱلۡإِيمَٰنِۚ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمۡ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّٰلِمُونَ

Enyi ambao mlimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata sheria Yake kivitendo, msiwafanye jamaa zenu, miongoni mwa kina baba, watoto na wengineo, kuwa ni marafiki (mnaowategemea) mkawa mnawasambazia siri za Waislamu na mnawataka ushauri katika mambo yenu, iwapo bado wako kwenye ukafiri na kuufanyia uadui Uislamu. Na yoyote atakayewafanya wao kuwa ni marafiki na akawapa mapenzi, atakuwa amemuasi Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na ameidhulumu nafasi yake dhuluma kubwa. info
التفاسير:

external-link copy
24 : 9

قُلۡ إِن كَانَ ءَابَآؤُكُمۡ وَأَبۡنَآؤُكُمۡ وَإِخۡوَٰنُكُمۡ وَأَزۡوَٰجُكُمۡ وَعَشِيرَتُكُمۡ وَأَمۡوَٰلٌ ٱقۡتَرَفۡتُمُوهَا وَتِجَٰرَةٞ تَخۡشَوۡنَ كَسَادَهَا وَمَسَٰكِنُ تَرۡضَوۡنَهَآ أَحَبَّ إِلَيۡكُم مِّنَ ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَجِهَادٖ فِي سَبِيلِهِۦ فَتَرَبَّصُواْ حَتَّىٰ يَأۡتِيَ ٱللَّهُ بِأَمۡرِهِۦۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia Waumini, «Iwapo mtawafanya kina baba, watoto, ndugu , wake na jamaa wa karibu, mali mlizozikusanya, biashara ambazo mnaogopa zisikose soko na majumba yanayopendeza ambayo mumekaa ndani yake, (iwapo mtayafanya hayo) ni bora kuliko kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na jihadi katika njia Yake, basi yangojeni mateso ya Mwenyezi Mungu na adhabu Yake kwenu. Na Mwenyezi Mungu hawapi taufiki wenye kutoka nje ya utiifu Wake. info
التفاسير:

external-link copy
25 : 9

لَقَدۡ نَصَرَكُمُ ٱللَّهُ فِي مَوَاطِنَ كَثِيرَةٖ وَيَوۡمَ حُنَيۡنٍ إِذۡ أَعۡجَبَتۡكُمۡ كَثۡرَتُكُمۡ فَلَمۡ تُغۡنِ عَنكُمۡ شَيۡـٔٗا وَضَاقَتۡ عَلَيۡكُمُ ٱلۡأَرۡضُ بِمَا رَحُبَتۡ ثُمَّ وَلَّيۡتُم مُّدۡبِرِينَ

Hakika Mwenyezi Mungu Amewasaidia kwa kuwapa ushindi katika matukio ya vita mengi mlipozishikilia sababu za ushindi na mkamtegemea Mwenyezi Mungu. Na siku ya vita vya Hunayn mlisema, «Hatutashindwa leo kwa uchache.» Hapo wingi wenu ukawadanganya usiwafae, na adui yenu akawalemea msipate pa kukimbilia kwenye ardhi iliyo pana, mkakimbia katika hali ya kushindwa. info
التفاسير:

external-link copy
26 : 9

ثُمَّ أَنزَلَ ٱللَّهُ سَكِينَتَهُۥ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ وَعَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَأَنزَلَ جُنُودٗا لَّمۡ تَرَوۡهَا وَعَذَّبَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَذَٰلِكَ جَزَآءُ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Kisha Mwenyezi Mungu Alimteremshia utulivu Mtume Wake na Waumini wakasimama imara, na Mwenyezi Mungu Akawaongezea askari wasiowaona miongoni mwa Malaika. Hapo Aliwapa ushindi juu ya adui yao na akawaadhibu wale waliokufuru. Hayo ni mateso ya Mwenyezi Mungu kwa wenye kuzuia dini ya Mwenyezi Mungu isifuatwe, wenye kuwakanusha Mitume Wake. info
التفاسير: