クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis

ページ番号:close

external-link copy
3 : 25

وَٱتَّخَذُواْ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةٗ لَّا يَخۡلُقُونَ شَيۡـٔٗا وَهُمۡ يُخۡلَقُونَ وَلَا يَمۡلِكُونَ لِأَنفُسِهِمۡ ضَرّٗا وَلَا نَفۡعٗا وَلَا يَمۡلِكُونَ مَوۡتٗا وَلَا حَيَوٰةٗ وَلَا نُشُورٗا

Na washirikina wa kiarabu walitengeneza waungu, wasiokuwa Mwenyezi Mungu. Waungu hao hawawezi kuumba chochote, na Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyewaumba wao na wenye kuwaabudu, wala hawana uwezo wa kuzuia madhara wala kujiletea manufaa, wala hawawezi kukifisha kilicho hai wala kukihuisha kilichokufa au kumfufua yoyote, miongoni mwa wafu, akiwa hai kutoka kaburini mwake. info
التفاسير:

external-link copy
4 : 25

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ إِفۡكٌ ٱفۡتَرَىٰهُ وَأَعَانَهُۥ عَلَيۡهِ قَوۡمٌ ءَاخَرُونَۖ فَقَدۡ جَآءُو ظُلۡمٗا وَزُورٗا

Na wenye kumkanusha Mwenyezi Mungu walisema kwamba hii Qur’ani ni urongo tu na ni uzushi uliofanywa na Muhammad na akasaidiwa na watu wengine. Kwa hakika wamefanya udhalimu mbaya sana na wameleta uzushi wenye kuchukiza, kwani Qur’ani haikuwa inamkinika kwa binadamu yoyote kuizua. info
التفاسير:

external-link copy
5 : 25

وَقَالُوٓاْ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ ٱكۡتَتَبَهَا فَهِيَ تُمۡلَىٰ عَلَيۡهِ بُكۡرَةٗ وَأَصِيلٗا

Na walisema kuhusu Qur’ani, «Hiyo ni hadithi za wakale katika vitabu vyao, na Muhammad amezinakili. Basi hizo anasomewa asubuhi na jioni,» info
التفاسير:

external-link copy
6 : 25

قُلۡ أَنزَلَهُ ٱلَّذِي يَعۡلَمُ ٱلسِّرَّ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّهُۥ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Kwa hakika Aliyeiteremsha Qur’ani ni Mwenyezi Mungu Ambaye ujuzi Wake umevizunguka vilivyoko mbinguni na ardhini. Kwa hakika Yeye ni Msamehefu sana kwa waliotubia kutokana na madhambi na maasia, ni Mwenye huruma kwao kwa kuwa hakufanya haraka ya kuwatesa.» info
التفاسير:

external-link copy
7 : 25

وَقَالُواْ مَالِ هَٰذَا ٱلرَّسُولِ يَأۡكُلُ ٱلطَّعَامَ وَيَمۡشِي فِي ٱلۡأَسۡوَاقِ لَوۡلَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مَلَكٞ فَيَكُونَ مَعَهُۥ نَذِيرًا

Na walisema washirikina, «Ana nini huyu anayedai kwamba yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (wakimkusudia Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie), anakula chakula kama sisi na aenda sokoni kutafuta riziki? Basi si angalimtuma Malaika awe naye ashuhudilie ukweli wake, info
التفاسير:

external-link copy
8 : 25

أَوۡ يُلۡقَىٰٓ إِلَيۡهِ كَنزٌ أَوۡ تَكُونُ لَهُۥ جَنَّةٞ يَأۡكُلُ مِنۡهَاۚ وَقَالَ ٱلظَّٰلِمُونَ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا رَجُلٗا مَّسۡحُورًا

au imshukie kutoka mbinguni kanzi ya mali, au awe na shamba kubwa ambalo yeye anakula matunda yake.» Na wakaendelea kusema, hawa madhalimu wenye kukanusha, «Mumfuatao nyinyi si mwingine isipokuwa ni mtu aliyefanyiwa uchawi ulioathiri akili yake.» info
التفاسير:

external-link copy
9 : 25

ٱنظُرۡ كَيۡفَ ضَرَبُواْ لَكَ ٱلۡأَمۡثَٰلَ فَضَلُّواْ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ سَبِيلٗا

Tazama, ewe Mtume, namna walivyosema, hawa wakanushaji, juu yako maneno hayo ya ajabu yanayofanana na mifano kwa ugeni wake, ili wafikie kukukanusha, kwa hivyo wakawa mbali na haki, na kwa hivyo hawapati njia ya kuifikia (hiyo haki) ili wayarakibishe maneno waliyoyasema kuhusu wewe, ya urongo na uzushi. info
التفاسير:

external-link copy
10 : 25

تَبَارَكَ ٱلَّذِيٓ إِن شَآءَ جَعَلَ لَكَ خَيۡرٗا مِّن ذَٰلِكَ جَنَّٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ وَيَجۡعَل لَّكَ قُصُورَۢا

Ni kubwa mno baraka za Mwenyezi Mungu, na ni mengi sana mema Yake, Ambaye Akitaka Atakufanyia mema zaidi kuliko yale waliotamani uwe nayo, Angalikufanyia, ulimwenguni, mashamba mengi ambayo kati yake inapita mito, na Akufanye uwe na majumba makubwa ya fahari. info
التفاسير:

external-link copy
11 : 25

بَلۡ كَذَّبُواْ بِٱلسَّاعَةِۖ وَأَعۡتَدۡنَا لِمَن كَذَّبَ بِٱلسَّاعَةِ سَعِيرًا

Na hawakukanusha, kwa kuwa unakula chakula na unaenda sokoni, lakini wameikanusha Siku ya Kiyama na malipo yake yaliyoko. Na tumewatayarishia waliokikanusha Kiyama Moto mkali, watachomwa nao. info
التفاسير: