আল-কোৰআনুল কাৰীমৰ অৰ্থানুবাদ - শ্বাহিলি অনুবাদ- আলী মুহছিন আল-বাৰওৱানী

পৃষ্ঠা নং:close

external-link copy
29 : 11

وَيَٰقَوۡمِ لَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مَالًاۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِۚ وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْۚ إِنَّهُم مُّلَٰقُواْ رَبِّهِمۡ وَلَٰكِنِّيٓ أَرَىٰكُمۡ قَوۡمٗا تَجۡهَلُونَ

Na enyi watu wangu! Mimi sikuombeni mali kwa ajili ya haya. Mimi sina ujira ila kwa Mwenyezi Mungu; na mimi sitawafukuza walio amini. Hakika wao watakutana na Mola wao Mlezi, lakini mimi nakuoneni mnafanya ujinga. info

Enyi watu! Mimi sitaki mali kwa kufikisha Ujumbe wa Mola wangu Mlezi, bali nataraji malipo yangu kwa Mwenyezi Mungu. Wala mimi siwafukuzi kwenye baraza yangu na kuingiana nami walio muamini Mola wao Mlezi, kwa sababu ya kuwa nyinyi mnawadharau tu! Kwani wao watakuja kukutana na Mola wao Mlezi Siku ya Kiyama na watanishitaki kwake ikiwa nimewafukuza kwa ajili ya ufakiri wao. Lakini mimi nakuoneni nyinyi ni watu msio jua nini kinacho watukuza viumbe mbele ya Mwenyezi Mungu! Ni utajiri na cheo kama mnavyo dai, au kufuata Haki na kufanya kheri?

التفاسير:

external-link copy
30 : 11

وَيَٰقَوۡمِ مَن يَنصُرُنِي مِنَ ٱللَّهِ إِن طَرَدتُّهُمۡۚ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Na enyi watu wangu! Ni nani atakaye nisaidia kwa Mwenyezi Mungu nikiwafukuza hawa? Basi je, hamfikiri? info

Enyi watu! Hapana yeyote awezaye kunikinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu nikiwafukuza hao hali nao ni wenye kumuamini Yeye. Je, bado mngali mnashikilia ujinga wenu? Hamkumbuki basi kuwa hawa watu wanaye Mola wao Mlezi wa kuwalipia?

التفاسير:

external-link copy
31 : 11

وَلَآ أَقُولُ لَكُمۡ عِندِي خَزَآئِنُ ٱللَّهِ وَلَآ أَعۡلَمُ ٱلۡغَيۡبَ وَلَآ أَقُولُ إِنِّي مَلَكٞ وَلَآ أَقُولُ لِلَّذِينَ تَزۡدَرِيٓ أَعۡيُنُكُمۡ لَن يُؤۡتِيَهُمُ ٱللَّهُ خَيۡرًاۖ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا فِيٓ أَنفُسِهِمۡ إِنِّيٓ إِذٗا لَّمِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ

Wala sikwambiini kuwa nina khazina za Mwenyezi Mungu; wala kuwa mimi najua mambo ya ghaibu; wala sisemi: Mimi ni Malaika. Wala siwasemi wale ambao yanawadharau macho yenu kuwa Mwenyezi Mungu hatawapa kheri - Mwenyezi Mungu anajua yaliomo katika nafsi zao - hapo bila ya shaka ninge kuwa miongoni mwa wenye kudhulumu. info

Wala sikwambiini kuwa kwa sababu mimi ni Mtume, basi ninazo khazina za riziki ya Mwenyezi Mungu, nitumie nitakavyo, na kwa hivyo nimfanye anaye nifuata tajiri! Wala sikwambiini kuwa mimi najua mambo ya ghaibu, na kwa hivyo nikupeni khabari yale yaliyo mkhusu Mwenyezi Mungu tu kuyajua, kwa kuwa hapana mja yeyote anaye yajua! Wala mimi sikwambiini kuwa mimi ni Malaika, na kwa hivyo mnirudi kwa kauli yenu: Huyu si chochote ila mwanaadamu tu! Wala siwasemi wale mnao wadharau kwamba Mwenyezi Mungu hatowapa kheri yoyote kwa kutaka kuridhi myatakayo! Kwani Mwenyezi Mungu peke yake ndiye anaye jua ikhlasi iliomo katika nafsi zao!..Mimi nikisema myatakayo nitakuwa katika wenye kujidhulumu na kudhulumu wengineo.

التفاسير:

external-link copy
32 : 11

قَالُواْ يَٰنُوحُ قَدۡ جَٰدَلۡتَنَا فَأَكۡثَرۡتَ جِدَٰلَنَا فَأۡتِنَا بِمَا تَعِدُنَآ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Wakasema: Ewe Nuhu! Umejadiliana, na umekithirisha kutujadili. Basi tuletee hayo unayo tuahidi, ukiwa miongoni mwa wasemao kweli. info

Wakasema: Ewe Nuhu! Umebishana nasi ili tukuamini, na umezidisha kutujadili mpaka tumechoka. Sasa hatuyastahamilii tena maneno yako. Basi, hebu, tuletee hiyo adhabu unayo tutishia, kama wewe kweli unayo yasema kwamba Mwenyezi Mungu atatuadhibu tukito kuamini!

التفاسير:

external-link copy
33 : 11

قَالَ إِنَّمَا يَأۡتِيكُم بِهِ ٱللَّهُ إِن شَآءَ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ

Akasema (Nuhu) : Mwenyezi Mungu atakuleteeni akipenda, wala nyinyi siwenye kumshinda. info

Nuhu akasema: Mambo haya yamo mikononi mwa Mwenyezi Mungu pekee. Yeye ndiye atakuleteeni alitakalo kwa hikima yake. Wala nyinyi hamwezi kuikimbia adhabu yake itakapo kuja. Kwani Yeye, Subhanahu, haemewi na chochote katika ardhi wala katika mbingu.

التفاسير:

external-link copy
34 : 11

وَلَا يَنفَعُكُمۡ نُصۡحِيٓ إِنۡ أَرَدتُّ أَنۡ أَنصَحَ لَكُمۡ إِن كَانَ ٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يُغۡوِيَكُمۡۚ هُوَ رَبُّكُمۡ وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Wala nasaha yangu haikufaini kitu nikitaka kukunasihini, ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kukuachieni mpotee. Yeye ndiye Mola wenu Mlezi; na kwake mtarejeshwa. info

Wala nasaha yangu haitakufaeni kitu kwa kuwa tu nakutakieni kheri, ikiwa Mwenyezi Mungu anakutakeni mpotee kwa mujibu wa ilimu yake na uwezo wake kwa kuharibika nyoyo zenu, hata zimekuwa haziikubali Haki! Yeye Subhanahu ndiye Mola wenu Mlezi, naye atakurejesheni kwake Siku ya Kiyama. Na atakulipeni kwa mlivyo kuwa mkitenda.

التفاسير:

external-link copy
35 : 11

أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ إِنِ ٱفۡتَرَيۡتُهُۥ فَعَلَيَّ إِجۡرَامِي وَأَنَا۠ بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُجۡرِمُونَ

Au ndio wanasema: Ameizua? Sema: Ikiwa nimeizua, basi kosa hilo ni juu yangu, na mimi sikhusiki na makosa myatendayo. info

Nini msimamo wa washirikina kukhusu hadithi hizi za kweli? Watasema kazizua? Wakisema hivyo, basi waambie: Ikiwa nimezizua kama mnavyo dai, basi hilo ni kosa kubwa; ni juu yangu mimi tu dhambi zake! Na ikiwa nimesema kweli, basi nyinyi ndio wenye makosa, na mimi sikhusiki na matokeo ya makosa yenu.

التفاسير:

external-link copy
36 : 11

وَأُوحِيَ إِلَىٰ نُوحٍ أَنَّهُۥ لَن يُؤۡمِنَ مِن قَوۡمِكَ إِلَّا مَن قَدۡ ءَامَنَ فَلَا تَبۡتَئِسۡ بِمَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ

Na akafunuliwa Nuhu akaambiwa: Hataamini yeyote katika watu wako ila wale walio kwisha amini. Basi usisikitike kwa waliyo kuwa wakiyatenda. info

Mwenyezi Mungu akamletea wahyi Nuhu akamwambia: Hatakusadiki wala hataifuata Haki yeyote katika kaumu yako baada ya sasa, isipo kuwa wale walio kwisha tangulia kukuamini kabla ya hayo. Basi ewe Nuhu! Usihuzunike kwa sababu ya waliyo kuwa wakikutendea, ya kukukadhibisha, na kukuudhi. Kwani Sisi tutawalipiza karibu.

التفاسير:

external-link copy
37 : 11

وَٱصۡنَعِ ٱلۡفُلۡكَ بِأَعۡيُنِنَا وَوَحۡيِنَا وَلَا تُخَٰطِبۡنِي فِي ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ إِنَّهُم مُّغۡرَقُونَ

Na unda jahazi mbele ya macho yetu na kwa mujibu wa ufunuo wetu. Wala usinisemeze kuwatetea walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa. info

Tukamwambia: Tengeneza chombo chini ya uangalizi na ulinzi wetu, wala usinisemeze kwa ajili ya hawa madhaalimu, kwa sababu nilikwisha itikia ombi lako, na nimekwisha amrisha wateketezwe kwa kuzamishwa. Tazama Aya 27 Surat Al Muuminun (23).

التفاسير: