ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

external-link copy
86 : 28

وَمَا كُنتَ تَرۡجُوٓاْ أَن يُلۡقَىٰٓ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبُ إِلَّا رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۖ فَلَا تَكُونَنَّ ظَهِيرٗا لِّلۡكَٰفِرِينَ

Nawe hukuwa unataraji kuletewa Kitabu; lakini ni rehema tu ya Mola wako Mlezi. Basi usiwe msaidizi wa makafiri. info

Ewe Mtume! Wewe hukuwa wewe ukitaraji na ukingojea uteremshiwe hii Qur'ani. Lakini Mwenyezi Mungu amekuteremshia kutoka kwake kwa kukurehemu wewe na umma wako. Basi ikumbuke neema hii, na shikilia kuifikisha. Wala usiwe wewe na wanao kufuata kuwa wasaidizi wa makafiri kwa wanayo yataka.

التفاسير: