ترجمة معاني القرآن الكريم - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

رقم الصفحة:close

external-link copy
43 : 23

مَا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ

Hautangulii ummah wowote, miongoni mwa ummah hawa wanaokanusha Mitume wao, muda uliowekewa kuangamia kwake, wala hauchelewi. info
التفاسير:

external-link copy
44 : 23

ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا تَتۡرَاۖ كُلَّ مَا جَآءَ أُمَّةٗ رَّسُولُهَا كَذَّبُوهُۖ فَأَتۡبَعۡنَا بَعۡضَهُم بَعۡضٗا وَجَعَلۡنَٰهُمۡ أَحَادِيثَۚ فَبُعۡدٗا لِّقَوۡمٖ لَّا يُؤۡمِنُونَ

Kisha tukawapeleka Mitume wetu waende kwa ummah hao, wakifuatana: hawa baada wengine. Na kila Mtume akiwalingania watu wake, wanamkanusha. Basi tukawafuatisha, kundi baada ya kundi, kwa kuwaangamiza na kuwamaliza, na hakuna kilichosalia isipokuwa ni habari za kuangamia kwao.Na tukazifanya habari hizo ni maneno ya kuzungumzwa na watu waliokuja baada yao, wakizichukuwa kuwa ni mazingatio. Basi maangamivu na kuepushwa na kila kheri ni kwa watu wasiowaamini Mitume wala kuwatii. info
التفاسير:

external-link copy
45 : 23

ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ وَأَخَاهُ هَٰرُونَ بِـَٔايَٰتِنَا وَسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Kisha tukampeleka Mūsā na ndugu yake Hārūn kwa alama zetu tisa, nazo ni fimbo, mkono, nzige, chawa, vyura, damu, mafuriko, shida za maisha na upungufu wa matunda, zikiwa ushahidi uliyo wazi wenye kuzishinda nyoyo, zipate kulainika kwa alama hizo nyoyo zaWaumini, na isimame hoja juu ya washindani. Tuliwapeleka wao wawili info
التفاسير:

external-link copy
46 : 23

إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَٱسۡتَكۡبَرُواْ وَكَانُواْ قَوۡمًا عَالِينَ

kwa Fir'awn, hakimu wa Misri, na watukufu wa watu wake ambao walifanya kiburi wakakataa kumuamini Mūsā na ndugu yake. Na wao walikuwa ni watu wanaojiona bora kuliko watu wengine na walikuwa wakiwanyanyasa kwa kuwadhulumu. info
التفاسير:

external-link copy
47 : 23

فَقَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لِبَشَرَيۡنِ مِثۡلِنَا وَقَوۡمُهُمَا لَنَا عَٰبِدُونَ

Wakasema, «Je, tuwaamini watu wawili kama sisi, na jamaa zao Wana wa Isrāīl wako chini ya amri yetu, wanatutii na wanajidhalilisha kwetu.?» info
التفاسير:

external-link copy
48 : 23

فَكَذَّبُوهُمَا فَكَانُواْ مِنَ ٱلۡمُهۡلَكِينَ

Basi wakawakanusha katika yale waliyokuja nayo, wakawa ni wenye kuangamizwa kwa kuzamishwa baharini. info
التفاسير:

external-link copy
49 : 23

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ لَعَلَّهُمۡ يَهۡتَدُونَ

Hakika tulimletea Mūsā Taurati, ili watu wake wajiongoze nayo kwenye haki. info
التفاسير:

external-link copy
50 : 23

وَجَعَلۡنَا ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَأُمَّهُۥٓ ءَايَةٗ وَءَاوَيۡنَٰهُمَآ إِلَىٰ رَبۡوَةٖ ذَاتِ قَرَارٖ وَمَعِينٖ

Na tulimjaalia Īsā mwana wa Maryam na mamake ni alama yenye kuonesha uweza wetu, kwani tulimuumba bila ya baba, na tulimfanyia makao kwenye ardhi iliyopo mahali pa juu palipolingana ili apate utulivu juu yake, penye urutuba na maji yapitayo yanayoonekana waziwazi kwa macho. info
التفاسير:

external-link copy
51 : 23

يَٰٓأَيُّهَا ٱلرُّسُلُ كُلُواْ مِنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَٱعۡمَلُواْ صَٰلِحًاۖ إِنِّي بِمَا تَعۡمَلُونَ عَلِيمٞ

Enyi Mitume! Kuleni riziki ya halali na fanyeni matendo mema, kwani mimi kwa mnayoyafanya ni mjuzi, hakuna kitu chochote chenye kufichika kwangu katika matendo yenu. Wanaohutubiwa katika aya hii ni Mitume wote kwa jumla, amani iwashukie, na wafuasi wao. Na katika aya pana dalili kwamba kula halali inasaidia kufanya matendo mema na kwamba mwisho wa haramu ni mbaya na miongoni mwa ubaya wake ni kurudishwa dua kwa kutokubaliwa. info
التفاسير:

external-link copy
52 : 23

وَإِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱتَّقُونِ

Na kwa hakika Dini yenu, enyi Mitume, ni Dini moja, nayo ni Uislamu, na mimi ni Mola wenu niogopeni kwa kufuata maamrisho yangu na kujiepusha na makatazo yangu. info
التفاسير:

external-link copy
53 : 23

فَتَقَطَّعُوٓاْ أَمۡرَهُم بَيۡنَهُمۡ زُبُرٗاۖ كُلُّ حِزۡبِۭ بِمَا لَدَيۡهِمۡ فَرِحُونَ

Na wafuasi walipambanukana katika dini wakawa makundi na mapote, wakaifanya dini yao kuwa dini nyingi baada ya kuamrishwa wajikusanye pamoja. Kila kundi linajigamba kwa maoni yake, linadai kuwa kundi hilo liko kwenye haki na lingine liko kwenye batili. Katika haya pana onyo la kujiweka kwenye makundi na kupambanukana katika Dini. info
التفاسير:

external-link copy
54 : 23

فَذَرۡهُمۡ فِي غَمۡرَتِهِمۡ حَتَّىٰ حِينٍ

Basi waache , ewe Mtume, kwenye upotevu wao na ujinga wao wa kutoijua haki hadi pale adhabu itakapowashukia. info
التفاسير:

external-link copy
55 : 23

أَيَحۡسَبُونَ أَنَّمَا نُمِدُّهُم بِهِۦ مِن مَّالٖ وَبَنِينَ

Kwani wanadhani hawa makafiri kwamba yale tunayowapa ya mali na watoto ulimwenguni ni mazuri waliyoharakishiwa na kwamba wao wanastahiki hayo? info
التفاسير:

external-link copy
56 : 23

نُسَارِعُ لَهُمۡ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۚ بَل لَّا يَشۡعُرُونَ

Hakika tunawaharakishia haya mazuri kwa kuwatahini na kwa kuwavuta kidogo kidogo, lakini wao hawalihisi hilo. info
التفاسير:

external-link copy
57 : 23

إِنَّ ٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ خَشۡيَةِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Hakika wale ambao kwa kumcha Mola wao wanayaogopa na kujitahadhari na yale Aliyowaogopesha nayo Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. info
التفاسير:

external-link copy
58 : 23

وَٱلَّذِينَ هُم بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ يُؤۡمِنُونَ

Na wale ambao wao wanaziamini aya za Mwenyezi Mungu katika Qur’ani na wanazitumia. info
التفاسير:

external-link copy
59 : 23

وَٱلَّذِينَ هُم بِرَبِّهِمۡ لَا يُشۡرِكُونَ

Na wale ambao wao wanaitakasa ibada kwa Mwenyezi Mungu , Peke Yake, na hawamshirikishi na Yeye mwingine asiyekuwa Yeye. info
التفاسير: