Na mimi nimetumwa kwenu nisadikishe sharia ya Taurati aliyo teremshiwa Musa, na nikuhalalishieni, kwa amri ya Mwenyezi Mungu, baadhi ya mliyo harimishiwa zamani. Na mimi nimekuja na ishara kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuthibitisha ukweli wa ujumbe wangu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.(Katika Injili ya Mathayo 5.17 Yesu anasema: Msidhani ya kuwa nilikuja kuitangua torati au manabii, la, sikuja kutangua, bali kutimiza.)