قرآن کریم کے معانی کا ترجمہ - سواحلی ترجمہ - عبد اللہ محمد اور ناصر خمیس

At-Tahrim

external-link copy
1 : 66

يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَآ أَحَلَّ ٱللَّهُ لَكَۖ تَبۡتَغِي مَرۡضَاتَ أَزۡوَٰجِكَۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Ewe Mtume! Mbona unajizuia nafsi yako na halali Aliyokuhalalishia Mwenyezi Mungu kwa kuwa unataka kuwaridhisha wake zako? Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kukusamehe, ni Mwenye huruma kwako. info
التفاسير:

external-link copy
2 : 66

قَدۡ فَرَضَ ٱللَّهُ لَكُمۡ تَحِلَّةَ أَيۡمَٰنِكُمۡۚ وَٱللَّهُ مَوۡلَىٰكُمۡۖ وَهُوَ ٱلۡعَلِيمُ ٱلۡحَكِيمُ

Kwa hakika Amepasisha Mwenyezi Mungu kwenu, enyi Waumini, kuvihalalisha viapo vyenu kwa kuvitolea kafara. Kafara yenyewe ni kuwalisha masikini kumi au kuwavisha au kuacha shingo huru. Na asiyepata cha kutoa, basi afunge siku tatu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwanusuru nyinyi na kuyasimamia mambo yenu. Na Yeye Ndiye Mjuzi wa mambo yanayowafaa Akayapitisha kwenu, Ndiye Mwingi wa hekima kwenye maneno Yake na matendo Yake. info
التفاسير:

external-link copy
3 : 66

وَإِذۡ أَسَرَّ ٱلنَّبِيُّ إِلَىٰ بَعۡضِ أَزۡوَٰجِهِۦ حَدِيثٗا فَلَمَّا نَبَّأَتۡ بِهِۦ وَأَظۡهَرَهُ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ عَرَّفَ بَعۡضَهُۥ وَأَعۡرَضَ عَنۢ بَعۡضٖۖ فَلَمَّا نَبَّأَهَا بِهِۦ قَالَتۡ مَنۡ أَنۢبَأَكَ هَٰذَاۖ قَالَ نَبَّأَنِيَ ٱلۡعَلِيمُ ٱلۡخَبِيرُ

Na pindi Mtume alipompa siri mke wake Hafsah, radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, ya mazungumzo fulani, na yeye alipomwambia maneno hayo mke mwenzake 'Aishah, radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, na Mwenyezi Mungu Akamjulisha Mtume Wake kuwa mkewe ameitoa siri yake, alimjulisha Hafsah sehemu ya maneno aliyoyatoa na akayanyamazia mengine asimwambie kwa kuchunga heshima. Basi Mtume alipomwambia Hafsah yale mazungumzo aliyoyatangaza, alisema huyo mke, «Ni nani aliyekwambia maneno hayo?» Akasema Mtume, «Aliyenambia hayo ni Mwenyezi Mungu, Aliye Mwingi wa ujuzi na utambuzi, Ambaye hakifichamani Kwake chenye kujificha chochote. info
التفاسير:

external-link copy
4 : 66

إِن تَتُوبَآ إِلَى ٱللَّهِ فَقَدۡ صَغَتۡ قُلُوبُكُمَاۖ وَإِن تَظَٰهَرَا عَلَيۡهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ هُوَ مَوۡلَىٰهُ وَجِبۡرِيلُ وَصَٰلِحُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ بَعۡدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ

Iwapo mtarudi kwa Mwenyezi Mungu (ewe Hafsah na 'Aishah) basi yatakuwa yamepatikana kwenu yanayopelekea kukubaliwa toba yenu, kwa kuwa nyoyo zenu zilielekea kwenye kuyapenda yale aliyoyachukia Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ya kutoa siri yake. Na mtakaposaidiana juu yake kwa kufanya yanayomuudhi, basi Mwenyezi Mungu Ndiye Msimamizi wake na Mtetezi wake na Jibrili na Waumini wema. Na Malaika, baada ya usaidizi wa Mwenyezi Mungu, ni wasaidizi wake na watetezi juu ya yoyote anayemuudhi na kumfanyia uadui. info
التفاسير:

external-link copy
5 : 66

عَسَىٰ رَبُّهُۥٓ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبۡدِلَهُۥٓ أَزۡوَٰجًا خَيۡرٗا مِّنكُنَّ مُسۡلِمَٰتٖ مُّؤۡمِنَٰتٖ قَٰنِتَٰتٖ تَٰٓئِبَٰتٍ عَٰبِدَٰتٖ سَٰٓئِحَٰتٖ ثَيِّبَٰتٖ وَأَبۡكَارٗا

Linalotarajiwa kwa Mola wake iwapo atawaacha nyinyi, enyi wake zake, ni amuoze yeye, badala yenu nyinyi, wake wanyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu kwa kumtii, wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, wenye kumtii Mwenyezi mungu, wenye kurudi kwenye yale anayoyapenda Mwenyezi Mungu ya kumtii Yeye, wenye kumuabudu kwa wingi, wenye kufunga sana, wakiwa wake wakuu miongoni mwao na wanawali. info
التفاسير:

external-link copy
6 : 66

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَأَهۡلِيكُمۡ نَارٗا وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُ عَلَيۡهَا مَلَٰٓئِكَةٌ غِلَاظٞ شِدَادٞ لَّا يَعۡصُونَ ٱللَّهَ مَآ أَمَرَهُمۡ وَيَفۡعَلُونَ مَا يُؤۡمَرُونَ

Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo! Zilindeni nafsi zenu kwa kuyatenda yale ambayo Amewaamrisha kwayo Mwenyezi Mungu na kuyaepuka yale ambayo Amewakataza nayo, na walindeni watu wenu kwa kile mnachotumia kujilinda nyinyi wenyewe na Moto ambao kuni zake ni watu na majiwe. Watasimamia kuadhibiwa watu wa Motoni Malaika wenye nguvu walio thabiti katika usimamizi wao, wasioenda kinyume na Mwenyezi Mungu katika maamrisho Yake na wanaotekeleza yale wanayoamrishwa. info
التفاسير:

external-link copy
7 : 66

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَا تَعۡتَذِرُواْ ٱلۡيَوۡمَۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na wataambiwa wale waliokanusha kwamba Mwenyezi mungu Ndiye Mola wa haki na wakamkufuru, watakapoingizwa Motoni, «Msitafute nyudhuru Siku ya Leo, ukweli ni kwamba nyinyi mnapewa malipo ya yale ambayo mlikuwa mkiyafanya duniani. info
التفاسير: