[1] Unaonaje mtu ambaye atazinduka kutoka usingizini au katika hali ya kughafilika, (yani kuumbwa) na akakuta ametandikiwa zulia zuri (yani ardhi) na ameekewa hema (yani mbingu) hapo; na kuwekewa chakula na kinywaji. Je hapaswi kumshukuru aliyetenda haya? Basi hii ndiyo maana ya aya hii. (Tafsir Al-Baqqaa'ii)
[2] "Na hali nyinyi mnajua" kwamba, Mwenyezi Mungu peke yake ndiye aliyefanya vitendo hivyo vyote. Basi ni vipi mnamfanyia washirika? (Tafsir Ibn Al-Qayyim)