قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - ساۋاھىلچە تەرجىمىسى - روۋاد تەرجىمە مەركىزى

external-link copy
22 : 2

ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ فِرَٰشٗا وَٱلسَّمَآءَ بِنَآءٗ وَأَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجَ بِهِۦ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ رِزۡقٗا لَّكُمۡۖ فَلَا تَجۡعَلُواْ لِلَّهِ أَندَادٗا وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

(Mwenyezi Mungu) ambaye amekufanyieni ardhi hii kuwa kama tandiko, na mbingu kama paa. Na akateremsha maji kutoka mbinguni, na kwayo akatoa mazao yawe riziki zenu.[1] Basi msimfanyizie Mwenyezi Mungu washirika, na hali nyinyi mnajua.[2] info

[1] Unaonaje mtu ambaye atazinduka kutoka usingizini au katika hali ya kughafilika, (yani kuumbwa) na akakuta ametandikiwa zulia zuri (yani ardhi) na ameekewa hema (yani mbingu) hapo; na kuwekewa chakula na kinywaji. Je hapaswi kumshukuru aliyetenda haya? Basi hii ndiyo maana ya aya hii. (Tafsir Al-Baqqaa'ii)
[2] "Na hali nyinyi mnajua" kwamba, Mwenyezi Mungu peke yake ndiye aliyefanya vitendo hivyo vyote. Basi ni vipi mnamfanyia washirika? (Tafsir Ibn Al-Qayyim)

التفاسير: