Enyi mlio amini! Mmoja wenu anapoona alama za kukaribia mauti na akataka kuusia lolote basi kushuhudia wasia huo iwe: kushuhudia watu wawili waadilifu katika jamaa zenu, au watu wawili wengineo ikiwa mmo safarini na ishara za mauti zikatokea. Wazuieni wawili hao baada ya Swala wanapo kusanyika watu, na waape kwa jina la Mwenyezi Mungu wakisema: Hatubadilishi kwa kiapo chake kwa chochote, hata ikiwa ni kutufaa sisi au yeyote katika jamaa zetu. Wala hatutaficha ushahidi alio tuamrisha Mwenyezi Mungu kuutimiza baraabara. Kwani tukificha ushahidi au tukasema lisio la kweli, tutakuwa miongoni mwa wenye kudhulumu na kustahiki adhabu ya Mwenyezi Mungu.