قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - سەۋاھىلچە تەرجىمىسى. ئەلىي مۇھسىن بەرۋانىي قىلغان

external-link copy
48 : 28

فَلَمَّا جَآءَهُمُ ٱلۡحَقُّ مِنۡ عِندِنَا قَالُواْ لَوۡلَآ أُوتِيَ مِثۡلَ مَآ أُوتِيَ مُوسَىٰٓۚ أَوَلَمۡ يَكۡفُرُواْ بِمَآ أُوتِيَ مُوسَىٰ مِن قَبۡلُۖ قَالُواْ سِحۡرَانِ تَظَٰهَرَا وَقَالُوٓاْ إِنَّا بِكُلّٖ كَٰفِرُونَ

Ilipo wajia Haki kutoka kwetu walisema: Mbona hakupewa kama aliyo pewa Musa? Je! Kwani wao hawakuyakataa aliyo pewa Musa zamani? Walisema: Ni wachawi wawili wanasaidiana. Na wakasema: Hakika sisi tunawakataa wote. info

Na alipo ileta Mtume wa Mwenyezi Mungu Qur'ani kutokana na Mwenyezi Mungu, makafiri walisema: Laiti yeye angeli pewa miujiza ya kuonekana na kama aliyo pewa Musa, na Kitabu cha kuteremka mara moja kama Taurati! Na hali hao walimkataa Musa na Ishara zake, kama hivi leo wanavyo mkataa Muhammad na Kitabu chake, na wakasema: Sisi tunawakataa wote wawili. Basi kukataa ndiko kuliko pelekea kuikanya miujiza.

التفاسير: