قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - قۇرئان كەرىمنىڭ ساۋاھىلچە تەرجىمىسىنى ئابدۇللا مۇھەممەد ۋە ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان.

external-link copy
157 : 3

وَلَئِن قُتِلۡتُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوۡ مُتُّمۡ لَمَغۡفِرَةٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَحۡمَةٌ خَيۡرٞ مِّمَّا يَجۡمَعُونَ

Na iwapo mtauawa, enyi Waumini, katika hali ya kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu au mkafa vitani, Mwenyezi Mungu Atawasamehe madhmbi yenu na Atawarehemu rehema itokayo Kwake. Hapo mtafaulu kwa kuyapata mabustani ya Peponi yenye starehe nyingi. Hayo ni bora kuliko dunia na wanavyovikusanya wapenda dunia. info
التفاسير: