قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - قۇرئان كەرىمنىڭ ساۋاھىلچە تەرجىمىسىنى ئابدۇللا مۇھەممەد ۋە ناسىر خەمىيس تەرجىمە قىلغان.

external-link copy
171 : 2

وَمَثَلُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ كَمَثَلِ ٱلَّذِي يَنۡعِقُ بِمَا لَا يَسۡمَعُ إِلَّا دُعَآءٗ وَنِدَآءٗۚ صُمُّۢ بُكۡمٌ عُمۡيٞ فَهُمۡ لَا يَعۡقِلُونَ

Na sifa za waliokufuru na wale walinganizi wao katika uongofu na imani ni kama sifa ya mchunga anayewapigia kelele wanyama na kuwakaripia, hali wao hawaelewi maana ya maneno yake isipokuwa wanasikia mwito na mlio wa sauti tu. Makafiri hao ni viziwi wameziba masikizi yao wasisikie haki, ni mabubu wamezifunga ndimi zao wasiitamke haki, ni vipofu macho yao hayazioni hoja za haki zilizo wazi. Kwa hivyo, wao hawatumii akili zao kwa mambo yenye kuwafaa. info
التفاسير: