Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dili Tercüme - Ali Muhsin Al-Barvani

Qamar

external-link copy
1 : 54

ٱقۡتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلۡقَمَرُ

Saa imekaribia, na mwezi umepasuka! info

Kiyama kimekaribia na mwezi utapasuka hapana hivi wala hivi.

التفاسير:

external-link copy
2 : 54

وَإِن يَرَوۡاْ ءَايَةٗ يُعۡرِضُواْ وَيَقُولُواْ سِحۡرٞ مُّسۡتَمِرّٞ

Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea. info

Na makafiri wakiona Ishara, yaani muujiza mkubwa, wao hupuuza wakaacha kuuamini. Bali husema: Huu ni uchawi wa daima unaendelea!

التفاسير:

external-link copy
3 : 54

وَكَذَّبُواْ وَٱتَّبَعُوٓاْ أَهۡوَآءَهُمۡۚ وَكُلُّ أَمۡرٖ مُّسۡتَقِرّٞ

Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti. info

Na wamewakanusha Mitume na wakafuata yaliyo zainishwa na matamanio yao. Na kila jambo huishia mwisho wake linapo tulia na kuthibiti.

التفاسير:

external-link copy
4 : 54

وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّنَ ٱلۡأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزۡدَجَرٌ

Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio. info

Na ninaapa kuwa zimewajia makafiri khabari za mataifa yaliyo tangulia zenye ukweli wa uumbaji ambazo zina mikemeo ya kutosha.

التفاسير:

external-link copy
5 : 54

حِكۡمَةُۢ بَٰلِغَةٞۖ فَمَا تُغۡنِ ٱلنُّذُرُ

Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu! info

Haya yaliyo wajia ni hikima kubwa na lengo la kufikia mbali. Lakini maonyo yataleta faida gani kwa wanao zipinga hikima hizo?

التفاسير:

external-link copy
6 : 54

فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡۘ يَوۡمَ يَدۡعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَيۡءٖ نُّكُرٍ

Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha; . info

Ewe Muhammad! Waachilie mbali hawa makafiri, nawe ngojea siku atapoita mwitaji wa Mwenyezi Mungu kuitia jambo ambalo nafsi inalichukia mno!

التفاسير:

external-link copy
7 : 54

خُشَّعًا أَبۡصَٰرُهُمۡ يَخۡرُجُونَ مِنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ كَأَنَّهُمۡ جَرَادٞ مُّنتَشِرٞ

Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika! info

Macho yao yatainamia chini kwa wingi wa kitisho, wakitoka makaburini kama kwamba ni nzige walio tawanyika, kwa wingi wao na mbio zao.

التفاسير:

external-link copy
8 : 54

مُّهۡطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِۖ يَقُولُ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا يَوۡمٌ عَسِرٞ

Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu. info

Wakimkimbilia huyo mwitaji, wakimtazama kwa unyonge na unyenekevu, macho yao yanamwangalia yeye tu. Makafiri watasema Siku ya Kiyama: Hii leo ni siku nzito, siku ya shida!

التفاسير:

external-link copy
9 : 54

۞ كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ فَكَذَّبُواْ عَبۡدَنَا وَقَالُواْ مَجۡنُونٞ وَٱزۡدُجِرَ

Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa. info

Kabla ya makafiri wa Makka walikwisha kanusha kaumu ya Nuhu. Walimkadhibisha Nuhu, mja wetu na Mtume wetu, wakamsingizia kuwa ana wazimu. Wakaingiza baina yake na kufikisha kwake Ujumbe kila namna ya maudhi na vitisho.

التفاسير:

external-link copy
10 : 54

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَغۡلُوبٞ فَٱنتَصِرۡ

Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru! info

Nuhu akamwomba Mola wake Mlezi akisema: Hakika mimi nimeshindwa na hawa watu wangu, basi wapatilize hawa kwa ajili yangu!

التفاسير:

external-link copy
11 : 54

فَفَتَحۡنَآ أَبۡوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٖ مُّنۡهَمِرٖ

Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika. info

Basi tukaifungua milango ya mbingu ikamimina maji yasiyo katika;

التفاسير:

external-link copy
12 : 54

وَفَجَّرۡنَا ٱلۡأَرۡضَ عُيُونٗا فَٱلۡتَقَى ٱلۡمَآءُ عَلَىٰٓ أَمۡرٖ قَدۡ قُدِرَ

Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa. info

Na tukaipasua ardhi kwa chemchem zikitibuka maji. Yakakutana maji ya mbinguni na maji ya ardhi kuwahiliki, kama alivyo kadiria Mwenyezi Mungu Mtukufu.

التفاسير:

external-link copy
13 : 54

وَحَمَلۡنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلۡوَٰحٖ وَدُسُرٖ

Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba. info

Tukampakia Nuhu katika jahazi la mbao zinazo fungwa pamoja kwa kamba, kama mtepe.

التفاسير:

external-link copy
14 : 54

تَجۡرِي بِأَعۡيُنِنَا جَزَآءٗ لِّمَن كَانَ كُفِرَ

Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa. info

Likawa linakwenda baharini chini ya hifadhi yetu, kuwa ni malipo kwa Nuhu ambaye watu wake waliendelea kuukanya wito wake.

التفاسير:

external-link copy
15 : 54

وَلَقَد تَّرَكۡنَٰهَآ ءَايَةٗ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka? info

Na tumeliacha hilo tukio na kuzamishwa makafiri na kuokolewa Waumini liwe ni mawaidha, lakini yupo mwenye kuwaidhika?

التفاسير:

external-link copy
16 : 54

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu. info

Jee, vipi ilikuwa adhabu yangu na onyo langu kwa wakhalifu.

التفاسير:

external-link copy
17 : 54

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka? info

Ninaapa, tumeifanya Qur'ani iwe sahali kukumbukwa na kutoa mawaidha. Lakini je, yupo wa kuwaidhika?

التفاسير:

external-link copy
18 : 54

كَذَّبَتۡ عَادٞ فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu? info

Kina A'di walimkadhibisha Mtume wao Hudi. Je, hali gani adhabu yangu na onyo langu lilikuwa kwa wendao kinyume!

التفاسير:

external-link copy
19 : 54

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِيحٗا صَرۡصَرٗا فِي يَوۡمِ نَحۡسٖ مُّسۡتَمِرّٖ

Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo, info

Sisi kwa yakini tuliwapatiliza kwa upepo ubaridi unao vuma, katika siku ya ukorofi wa daima,

التفاسير:

external-link copy
20 : 54

تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٖ مُّنقَعِرٖ

Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa. info

Ukiwang'oa watu na kuwatupa nao wamekufa, kama vinavyo ng'olewa vigogo vya mitende na mizizi yake.

التفاسير:

external-link copy
21 : 54

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu? info

Hali gani adhabu yangu na onyo langu lilikuwa kwa walio kwenda kinyume!

التفاسير:

external-link copy
22 : 54

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka? info

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya sahali Qur'ani kwa ajili ya mawaidha na mazingatio, basi je, yupo wa kuwaidhika?

التفاسير:

external-link copy
23 : 54

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ

Thamudi waliwakanusha Waonyaji. info

Thamudi walikadhibisha maonyo ya Nabii wao, Saleh.

التفاسير:

external-link copy
24 : 54

فَقَالُوٓاْ أَبَشَرٗا مِّنَّا وَٰحِدٗا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٍ

Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa! info

Wakasema: Hivyo aje mtu tu katika sisi, watu wa kawaida, asiye na watu, nasi tumfuate? Tukimfuata huyo basi bila ya shaka sisi tutakuwa mbali mno na haki, na tutakuwa tuna wazimu basi.

التفاسير:

external-link copy
25 : 54

أَءُلۡقِيَ ٱلذِّكۡرُ عَلَيۡهِ مِنۢ بَيۡنِنَا بَلۡ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٞ

Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi! info

Uteremshiwe wahyi kwake yeye katika sisi na hali wapo wanao stahiki zaidi? Bali huyo kazikdi katika uwongo, mwenye kukanya neema.

التفاسير:

external-link copy
26 : 54

سَيَعۡلَمُونَ غَدٗا مَّنِ ٱلۡكَذَّابُ ٱلۡأَشِرُ

Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi. info

Karibu watakuja jua siku itapo wateremkia adhabu ni nani mwongo anaye ikanya neema. Wao au Saleh, Mtume wao?

التفاسير:

external-link copy
27 : 54

إِنَّا مُرۡسِلُواْ ٱلنَّاقَةِ فِتۡنَةٗ لَّهُمۡ فَٱرۡتَقِبۡهُمۡ وَٱصۡطَبِرۡ

Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili. info

Hakika Sisi tunampelekea Mtume wetu Saleh ngamia mke, awe ni mtihani wao. Basi wangojee, na uwatazame watafanya nini. Na subiri, uvumilie maudhi yao mpaka itapo kuja amri ya Mwenyezi Mungu.

التفاسير:

external-link copy
28 : 54

وَنَبِّئۡهُمۡ أَنَّ ٱلۡمَآءَ قِسۡمَةُۢ بَيۡنَهُمۡۖ كُلُّ شِرۡبٖ مُّحۡتَضَرٞ

Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika. info

Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao na ngamia. Kila mmoja wao atakuwa na zamu yake aje kunywa katika siku yake.

التفاسير:

external-link copy
29 : 54

فَنَادَوۡاْ صَاحِبَهُمۡ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja. info

Wakamwita mtu wao mmoja akapania kumchinja yule ngamia, akamchinja.

التفاسير:

external-link copy
30 : 54

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu! info

Basi vipi ilikuwa adhabu yangu na onyo langu kwa hao wakhalifu walio kwenda kinyume na amri.

التفاسير:

external-link copy
31 : 54

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَكَانُواْ كَهَشِيمِ ٱلۡمُحۡتَظِرِ

Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa. info

Sisi tuliwapatiliza kwa ukelele mmoja tu, wakawa kama miti mikavu anayo ikusanya yeyote atakaye kujengea boma la uwa wake.

التفاسير:

external-link copy
32 : 54

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye? info

Na bila ya shaka Sisi tumeisahilisha Qur'ani iwe nyepesi kwa ajili ya mawaidha na kuzingatia. Lakini je, yupo wa kuwaidhika?

التفاسير:

external-link copy
33 : 54

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطِۭ بِٱلنُّذُرِ

Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji. info

Kaumu Lut'i nao walikadhibisha maonyo ya Mtume wao.

التفاسير:

external-link copy
34 : 54

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٖۖ نَّجَّيۡنَٰهُم بِسَحَرٖ

Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri. info

Hakika Sisi tuliwapelekea upepo mkali wa kuwatupia changarawe. Isipo kuwa watu wa Lut'i walio amini. Hao tuliwaokoa na adhabu hii mwisho wa usiku.

التفاسير:

external-link copy
35 : 54

نِّعۡمَةٗ مِّنۡ عِندِنَاۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي مَن شَكَرَ

Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru. info

Kwa kuwapa neema iliyo toka kwetu. Neema kama hizo kubwa kubwa ndivyo tunavyo walipa wenye kuishukuru neema yetu kwa imani yao na ut'iifu.

التفاسير:

external-link copy
36 : 54

وَلَقَدۡ أَنذَرَهُم بَطۡشَتَنَا فَتَمَارَوۡاْ بِٱلنُّذُرِ

Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo. info

Na hakika Lut'i aliwahadharisha watu wake vipi mshiko wetu ulivyo mkali, wakatilia shaka maonyo yake kwa kuwa wanamwona mwongo.

التفاسير:

external-link copy
37 : 54

وَلَقَدۡ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيۡفِهِۦ فَطَمَسۡنَآ أَعۡيُنَهُمۡ فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu! info

Wakamtaka awape wageni wake wawatende fiili yao, tukayafuta macho yao kuwa ni malipo kwa hilo walilo litaka. Basi waambie kwa kuwakejeli: Igugumieni adhabu yangu, na maonyo yangu!

التفاسير:

external-link copy
38 : 54

وَلَقَدۡ صَبَّحَهُم بُكۡرَةً عَذَابٞ مُّسۡتَقِرّٞ

Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea. info

Na asubuhi mapema ikawashitua adhabu ya kuthibiti milele.

التفاسير:

external-link copy
39 : 54

فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!< info

Wakaambiwa: Igugumieni adhabu yangu na maonyo yangu!

التفاسير:

external-link copy
40 : 54

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka? info

Na hakika tumeifanya Qur'ani ni sahali kwa ajili ya mawaidha na mazingatio. Je! Yupo anaye waidhika?

التفاسير:

external-link copy
41 : 54

وَلَقَدۡ جَآءَ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ ٱلنُّذُرُ

Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni. info

Na watu wa Firauni yaliwajia maonyo ya mfululizo.

التفاسير:

external-link copy
42 : 54

كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذۡنَٰهُمۡ أَخۡذَ عَزِيزٖ مُّقۡتَدِرٍ

Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza. info

Walikadhibisha Ishara zetu na miujiza yetu waliyo kuja nayo Mitume wetu. Tukawaangamiza kwa maangamizo ya nguvu yasiyo shindika, ya uwezo mkubwa.

التفاسير:

external-link copy
43 : 54

أَكُفَّارُكُمۡ خَيۡرٞ مِّنۡ أُوْلَٰٓئِكُمۡ أَمۡ لَكُم بَرَآءَةٞ فِي ٱلزُّبُرِ

Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani? info

Ati nyinyi, makafiri, mna nguvu zaidi kuliko hao wa kaumu zilizo tangulia ambao wameangamizwa? Au nyinyi mmetolewa makosani kwa ilivyo teremka katika Vitabu vya mbinguni?

التفاسير:

external-link copy
44 : 54

أَمۡ يَقُولُونَ نَحۡنُ جَمِيعٞ مُّنتَصِرٞ

Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu. info

Bali ati wanasema hawa makafiri: Sisi ni kikundi kilicho ungana chenye nguvu juu ya maadui wake, hakishindwi.

التفاسير:

external-link copy
45 : 54

سَيُهۡزَمُ ٱلۡجَمۡعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ

Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma. info

Kikundi hicho kitashindwa, na watakimbia mbio wakifurushwa.

التفاسير:

external-link copy
46 : 54

بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوۡعِدُهُمۡ وَٱلسَّاعَةُ أَدۡهَىٰ وَأَمَرُّ

Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi. info

Bali Kiyama ndio miadi ya adhabu yao. Na Kiyama ni kizito zaidi, na kichungu zaidi.

التفاسير:

external-link copy
47 : 54

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٖ

Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu. info

Hakika wakosefu kutokana na hawa na hao watakuwa katika hilaki na Jahannamu inayo waka moto.

التفاسير:

external-link copy
48 : 54

يَوۡمَ يُسۡحَبُونَ فِي ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ ذُوقُواْ مَسَّ سَقَرَ

Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu! info

Siku watapo bururwa kifudifudi katika Moto wakiambiwa: Hilikini kwa machungu ya Jahannamu na joto lake!

التفاسير:

external-link copy
49 : 54

إِنَّا كُلَّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَٰهُ بِقَدَرٖ

Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo. info

Hakika Sisi tumeumba kila kitu. Tumeviumba kwa kukadiria inavyo hitajia hikima.

التفاسير:

external-link copy
50 : 54

وَمَآ أَمۡرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٞ كَلَمۡحِۭ بِٱلۡبَصَرِ

Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho. info

Na haikuwa amri yetu tukitaka kitu ila neno moja tu, nalo ni kusema: "Kuwa", nacho huwa, papo hapo kama kupepesa kwa jicho.

التفاسير:

external-link copy
51 : 54

وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَآ أَشۡيَاعَكُمۡ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka? info

Na bila ya shaka Sisi tumekwisha waangamiza wengine walio fanana nanyi katika ukafiri. Je! Yupo aliye waidihika?

التفاسير:

external-link copy
52 : 54

وَكُلُّ شَيۡءٖ فَعَلُوهُ فِي ٱلزُّبُرِ

Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni. info

Na kila kitu walicho kifanya duniani kimeandikwa katika madaftari, kimeambatishwa nao.

التفاسير:

external-link copy
53 : 54

وَكُلُّ صَغِيرٖ وَكَبِيرٖ مُّسۡتَطَرٌ

Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa. info

Na kila dogo na kubwa katika vitendo limeandikwa. Hakipotei kitu.

التفاسير:

external-link copy
54 : 54

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَنَهَرٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito. info

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani yenye shani kuu, na mito ya namna mbali mbali.

التفاسير:

external-link copy
55 : 54

فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ

Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza. info

Katika baraza ya Haki, hakuna porojo huko wala madhambi, kwa Mwenyewe Mfalme Mtukufu wa uweza

التفاسير: