Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dilinde Tercüme - Abdullah Muhammed ve Nasır Hamiys

Sayfa numarası:close

external-link copy
28 : 17

وَإِمَّا تُعۡرِضَنَّ عَنۡهُمُ ٱبۡتِغَآءَ رَحۡمَةٖ مِّن رَّبِّكَ تَرۡجُوهَا فَقُل لَّهُمۡ قَوۡلٗا مَّيۡسُورٗا

Na ukiwaepuka hawa ambao uliamrishwa uwape, kwa kuwa hakuna kitu cha kuwapa, kwa kungojea riziki kutoka kwa Mola wako, basi waambie maneno laini ya upole kama vile kuwaombea dua awatajirishe na awape riziki kunjufu, na uwaahidi kwamba Mwenyezi Mungu Akiyafanya mambo ya riziki kuwa mapesi kwa wema Wake basi wewe utawapatia nao. info
التفاسير:

external-link copy
29 : 17

وَلَا تَجۡعَلۡ يَدَكَ مَغۡلُولَةً إِلَىٰ عُنُقِكَ وَلَا تَبۡسُطۡهَا كُلَّ ٱلۡبَسۡطِ فَتَقۡعُدَ مَلُومٗا مَّحۡسُورًا

Wala usiuzuie mkono wako kutumia katika njia njema, ukaidhiki nafsi yako na watu wako na wahitaji, na wala usipite kiasi katika matumizi ukatoa zaidi ya uwezo wako, kwani ukifanya hivyo utaketi hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa, kwani watu watakulaumu na watakutukana, na ni mwenye kujuta juu ya ufujaji wako na mali yako kupotea. info
التفاسير:

external-link copy
30 : 17

إِنَّ رَبَّكَ يَبۡسُطُ ٱلرِّزۡقَ لِمَن يَشَآءُ وَيَقۡدِرُۚ إِنَّهُۥ كَانَ بِعِبَادِهِۦ خَبِيرَۢا بَصِيرٗا

Hakika Mola wako nawakunjulia riziki baadhi ya watu na Anawabania wengine kulingana na ujuzi Wake na hekima Yake, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake. Yeye Ndiye Mwenye kuyaona mambo ya ndani ya waja Wake, hakuna chochote katika hali zao kilicho nje ya ujuzi Wake. info
التفاسير:

external-link copy
31 : 17

وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُمۡ خَشۡيَةَ إِمۡلَٰقٖۖ نَّحۡنُ نَرۡزُقُهُمۡ وَإِيَّاكُمۡۚ إِنَّ قَتۡلَهُمۡ كَانَ خِطۡـٔٗا كَبِيرٗا

Na mkijua kwamba riziki iko kwenye mkono wa Mwenyezi Mungu, kutkata na sifa za upungufu ni Kwake, basi msiwaue watoto wenu kwa kuchelea umasikini, kwani Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Mwenye kuwaruzuku waja Wake, Anawruzuku wana kama Anavyowaruzuku wazazi. Hakika kuua watoto ni dhambi kubwa. info
التفاسير:

external-link copy
32 : 17

وَلَا تَقۡرَبُواْ ٱلزِّنَىٰٓۖ إِنَّهُۥ كَانَ فَٰحِشَةٗ وَسَآءَ سَبِيلٗا

Wala msikaribie uzinifu na mambo yanayopelekea huko ili msiingie ndani yake, hakika hilo ni tendo baya sana, na njia mbaya zaidi ni njia ya tendo hilo. info
التفاسير:

external-link copy
33 : 17

وَلَا تَقۡتُلُواْ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَمَن قُتِلَ مَظۡلُومٗا فَقَدۡ جَعَلۡنَا لِوَلِيِّهِۦ سُلۡطَٰنٗا فَلَا يُسۡرِف فِّي ٱلۡقَتۡلِۖ إِنَّهُۥ كَانَ مَنصُورٗا

Wala msiiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuawa, isipokuwa kwa haki ya kisharia, kama kisasi au kumpiga mawe mzinifu aliyeingia kwenye hifadhi ya ndoa au kumuua aliyeritadi. Na mwenye kuuawa pasi na haki ya kisheria, basi tumempa msimamizi wa mambo yake , awe ni mrithi au ni hakimu, uwezo wa kutaka muuaji auawe au kutaka dia. Na haifai kwa msimamizi wa mambo ya aliouawa kupita mpaka wa Mwenyezi Mungu katika kuchukua kisasi, kama vile kuua watu wawili au wengi kwa mmoja au kumua muuaji kwa njia ya kumtesa. Mwenyezi Mungu ni Mwenye kumsaidia msimamizi wa aliyeuawa juu ya aliyeua mpaka aweze kumuua kwa njia ya kisasi. info
التفاسير:

external-link copy
34 : 17

وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ بِٱلۡعَهۡدِۖ إِنَّ ٱلۡعَهۡدَ كَانَ مَسۡـُٔولٗا

Wala msitumie mali ya watoto waliofiliwa na wazazi wao nao wako chini ya miaka ya kubaleghe na wakawa wako chini ya usimamizi wenu, isipokuwa kwa njia ambayo ni nzuri kwao, nayo ni kuyazalisha na kuyakuza, mpaka afikie mtoto yatima miaka ya kubaleghe na utumiaji mzuri wa mali. Na timizeni utekelezaji wa kila ahadi mliyojilazimisha nayo, kwani Mwenyezi Mungu Atamuuliza mwenye kuweka ahadi kuhusu hiyo ahadi Siku ya Kiyama, Atamlipa akiitimiza na kuitekeleza na Atamtesa akienda kinyume nayo. info
التفاسير:

external-link copy
35 : 17

وَأَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ إِذَا كِلۡتُمۡ وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِۚ ذَٰلِكَ خَيۡرٞ وَأَحۡسَنُ تَأۡوِيلٗا

Na timizeni kipimo wala msikipunguze mnapowapimia wasiokuwa nyinyi, na mfanye mizani ya sawa, kwani kufanya uadilifu katika upimaji wa vibaba na mizani ni bora kwenu nyinyi ulimwenguni na kuna mwisho mwema mbele ya Mwenyezi Mungu kesho Akhera. info
التفاسير:

external-link copy
36 : 17

وَلَا تَقۡفُ مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٌۚ إِنَّ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡبَصَرَ وَٱلۡفُؤَادَ كُلُّ أُوْلَٰٓئِكَ كَانَ عَنۡهُ مَسۡـُٔولٗا

Na usiyafuate, ewe binadamu, usiyoyajua, lakini hakikisha na uthibitishe. Hakika ya biadamu ni mwenye kuulizwa juu ya yale ambayo alitumia masikizi yake, maangalizi yake na moyo wake kuyafikia. Basi akivitumia vitu hivyo katika wema atapata malipo mema na akivitumia katika uovu atapata mateso. info
التفاسير:

external-link copy
37 : 17

وَلَا تَمۡشِ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَرَحًاۖ إِنَّكَ لَن تَخۡرِقَ ٱلۡأَرۡضَ وَلَن تَبۡلُغَ ٱلۡجِبَالَ طُولٗا

Na usitembee ardhini kwa kujigamba na kujivuna, kwani wewe hutaipasua ardhi kwa kutembea juu yake kwa namna hiyo na hutaifikia milima katika urefu kwa kujigamba kwako, kujivuna kwako na kutakabari kwako. info
التفاسير:

external-link copy
38 : 17

كُلُّ ذَٰلِكَ كَانَ سَيِّئُهُۥ عِندَ رَبِّكَ مَكۡرُوهٗا

Yote yaliyotangulia kutajwa, ya maamrisho na makatazo, Mwenyezi Mungu Anayachukia mabaya yake na hayaridhii kwa waja wake. info
التفاسير: