ශුද්ධවූ අල් කුර්ආන් අර්ථ කථනය - ස්වහීලී පරිවර්තනය - අලි මුහ්සන් අල්බර්වානි

පිටු අංක:close

external-link copy
31 : 35

وَٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ هُوَ ٱلۡحَقُّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ بِعِبَادِهِۦ لَخَبِيرُۢ بَصِيرٞ

Na hayo tuliyo kufunulia kutoka Kitabuni ni Kweli yenye kusadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Hakika Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni Mwenye khabari na Mwenye kuona. info

Na tuliyo kuletea Wahyi wewe katika hii Qur'ani ni Haki tupu isiyo kuwa na shaka yoyote. Tumeiteremsha kuthibitisha Vitabu vilivyo teremshwa kwa Mitume walio kuwa kabla yako, kwa kuwa vyote ni asli moja. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu wa kujua na kuona kwa waja wake.

التفاسير:

external-link copy
32 : 35

ثُمَّ أَوۡرَثۡنَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلَّذِينَ ٱصۡطَفَيۡنَا مِنۡ عِبَادِنَاۖ فَمِنۡهُمۡ ظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ وَمِنۡهُم مُّقۡتَصِدٞ وَمِنۡهُمۡ سَابِقُۢ بِٱلۡخَيۡرَٰتِ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَضۡلُ ٱلۡكَبِيرُ

Kisha tumewarithisha Kitabu hao ambao tuliwateuwa miongoni mwa waja wetu. Kati yao yupo aliye jidhulumu nafsi yake, na yupo wa katikati, na yupo aliye tangulia katika mambo ya kheri, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Hiyo ndiyo fadhila kuu. info

Tena tumekifanya Kitabu hichi ni mirathi ya kurithiwa na waja wetu tulio wateuwa. Basi kati yao yupo aliye jidhulumu nafsi yake kwa kuzidi maovu yake kuliko mema yake; na yupo wa kiasi, hakupita mpaka katika maovu yake na wala hakukithirisha mema yake; na miongoni mwao yupo aliye washinda wenginewe kwa kufanya mambo ya kheri, kwa kusahilishiwa na Mwenyezi Mungu. Huko kushinda katika mambo ya kheri ndio kufuzu kukubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

التفاسير:

external-link copy
33 : 35

جَنَّٰتُ عَدۡنٖ يَدۡخُلُونَهَا يُحَلَّوۡنَ فِيهَا مِنۡ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٖ وَلُؤۡلُؤٗاۖ وَلِبَاسُهُمۡ فِيهَا حَرِيرٞ

Mabustani ya milele watayaingia. Huko watavikwa vikuku vya dhahabu, na lulu, na nguo zao humo ni za hariri. info

Malipo yao Akhera ni Mabustani ya daima watayo yaingia. Humo watajipamba kwa vikuku vya dhahabu na lulu. Na nguo zao za Peponi ni hariri.

التفاسير:

external-link copy
34 : 35

وَقَالُواْ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِيٓ أَذۡهَبَ عَنَّا ٱلۡحَزَنَۖ إِنَّ رَبَّنَا لَغَفُورٞ شَكُورٌ

Na watasema: Alhamdulillahi, Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu aliye tuondolea huzuni zote. Hakika Mola wetu Mlezi bila ya shaka ni Mwenye kusamehe, Mwenye shukrani. info

Na watasema wakisha ingia: Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu aliye tuondolea ya kutuhuzunisha. Hakika Mola wetu Mlezi ni Mwingi wa maghfira, Mwingi wa shukra.

التفاسير:

external-link copy
35 : 35

ٱلَّذِيٓ أَحَلَّنَا دَارَ ٱلۡمُقَامَةِ مِن فَضۡلِهِۦ لَا يَمَسُّنَا فِيهَا نَصَبٞ وَلَا يَمَسُّنَا فِيهَا لُغُوبٞ

Ambaye kwa fadhila yake ametuweka makao ya kukaa daima; humu haitugusi taabu wala humu hakutugusi kuchoka. info

Aliye tuweka kwenye Nyumba ya neema ya milele kwa fadhila zake hatupi taabu humo, wala hatuletei machofu.

التفاسير:

external-link copy
36 : 35

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَهُمۡ نَارُ جَهَنَّمَ لَا يُقۡضَىٰ عَلَيۡهِمۡ فَيَمُوتُواْ وَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُم مِّنۡ عَذَابِهَاۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي كُلَّ كَفُورٖ

Na walio kufuru watakuwa na Moto wa Jahannamu, hawahukumiwi wakafa, wala hawatapunguziwa adhabu yake. Hivyo ndivyo tunavyo mlipa kila mwenye kuzidi ukafiri. info

Na walio kufuru malipo yao waliyo ahidiwa ni Moto wa Jahannamu watakao uingia. Mwenyezi Mungu hatawahukumia mauti wakafa, wala hawatapunguziwa chembe ya adhabu wakapumzika. Ni kama hivyo tunavyo mlipa kila mwenye kuendelea katika ukafiri na akaushikilia.

التفاسير:

external-link copy
37 : 35

وَهُمۡ يَصۡطَرِخُونَ فِيهَا رَبَّنَآ أَخۡرِجۡنَا نَعۡمَلۡ صَٰلِحًا غَيۡرَ ٱلَّذِي كُنَّا نَعۡمَلُۚ أَوَلَمۡ نُعَمِّرۡكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن تَذَكَّرَ وَجَآءَكُمُ ٱلنَّذِيرُۖ فَذُوقُواْ فَمَا لِلظَّٰلِمِينَ مِن نَّصِيرٍ

Na humo watapiga makelele: Mola wetu Mlezi! Tutoe tufanye mema sio yale tuliyo kuwa tukiyafanya. Kwani hatukukupeni umri wa kutosha kukumbuka mwenye kukumbuka? Na akakujieni Mwonyaji? Basi onjeni! Kwani walio dhulumu hawana wa kuwanusuru. info

Na humo watapiga makelele kuomba msaada wakisema: Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni, tupate kutenda mema siyo yale tuliyo kuwa tukiyatenda duniani. Atawaambia: Hatukukupeni fursa ya kufanya a'mali, tukaufanya mrefu umri wenu kwa muda unao mkinika mtu ndani yake kuzingatia kwa mwenye kuzingatia? Na akukujieni Mtume akakuhadharisheni na adhabu hii. Basi onjeni katika Jahannamu malipo ya udhalimu wenu. Kwani mwenye kudhulumu hapati wa kumnusuru wala kumsaidia.

التفاسير:

external-link copy
38 : 35

إِنَّ ٱللَّهَ عَٰلِمُ غَيۡبِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّهُۥ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa siri za mbinguni na ardhi. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliomo vifuani. info

Hakika Mwenyezi Mungu anajua vyema kila kilicho fichikana katika mbingu na ardhi. Hapana chenye kufichikana kwake. Na lau ange kukubalieni akakurudisheni duniani mngeli rejea yale yale aliyo kukatazeni. Hakika Yeye Mtukufu anavijua vyema vishawishi na vivutio viliomo ndani ya vifua.

التفاسير: