Ibisobanuro bya qoran ntagatifu - Ibisobanuro bya Qur'an mu rurimi rw'igiswahili - Abdallah Mohamed na Nassor Khamis

numero y'urupapuro:close

external-link copy
102 : 6

ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ خَٰلِقُ كُلِّ شَيۡءٖ فَٱعۡبُدُوهُۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٞ

Huyo, enyi washirikina, Ndiye Mola wenu, Aliyeshinda na kutukuka; hapana Mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye; Mwenye kuumba kila kitu. Basi mwandameni na mumnyenyekee kwa kumtii na kumuabudu. Na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, ni Mtegemewa na ni Mtunzi, Anayaendesha mambo ya viumbe vyake. info
التفاسير:

external-link copy
103 : 6

لَّا تُدۡرِكُهُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ وَهُوَ يُدۡرِكُ ٱلۡأَبۡصَٰرَۖ وَهُوَ ٱللَّطِيفُ ٱلۡخَبِيرُ

Macho hayamuoni Mwenyezi Mungu ulimwenguni. Ama kwenye nyumba ya Akhera, Waumini watamuona Mola wao bila kumuenea. Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, anayafikia macho na kuyazunguka, na kuyajua vile yalivyo. Na Yeye ni Al-Latīf (Mpole) kwa mawalii Wake, Anayejua mambo yenye upeo wa udogo, Al-Khabīr (Mtambuzi) Anayejua mambo ya ndani. info
التفاسير:

external-link copy
104 : 6

قَدۡ جَآءَكُم بَصَآئِرُ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنۡ أَبۡصَرَ فَلِنَفۡسِهِۦۖ وَمَنۡ عَمِيَ فَعَلَيۡهَاۚ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِحَفِيظٖ

Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Mumejiwa na hoja zilizo wazi kutoka kwa Mola wenu, mnaonea nazo uongofu na upotevu, miongoni mwa zile zilizokusanywa na Qur’ani na akaja nazo Mtume, rehema na amani zimshukiye. Basi mwenye kufunukiwa na hoja hizi na akayaamini yale yanayolekezwa nazo, faida yake itamfikia mwenyewe. Na yule ambaye hakuuona uongofu baada ya hoja kumfunukia , basi amejikosea mwenyewe. Na mimi si mtunzi wa kudhibiti matendo yenu. Mimi ni mfikishaji tu. Na Mwenyezi Mungu Anamuongoza Anayemtaka na Anampoteza Anayemtaka kulingana na ujuzi Wake na hekima Yake.» info
التفاسير:

external-link copy
105 : 6

وَكَذَٰلِكَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ وَلِيَقُولُواْ دَرَسۡتَ وَلِنُبَيِّنَهُۥ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Na kama tulivyowafafanulia washirikina, katika hii Qur’ani, hoja zilizo wazi juu ya jambo la kumpwekesha Mwenyezi Mungu, utume na marejeo ya Kiyama, tunawafafanulia hoja katika kila wasichokijua. Na hapo wanasema urongo, «Umejifunza kutoka kwa watu wa Kitabu!» Na ili tufafanue haki, kwa kuzileta aya, kwa watu wanaoijua na kuikubali na kuifuata, nao ni waliomuamini Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kile alichoteremshiwa. info
التفاسير:

external-link copy
106 : 6

ٱتَّبِعۡ مَآ أُوحِيَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Fuata, ewe Mtume, wahyi tuliokuteremshia, wenye maamrisho na makatazo ambayo, kubwa lake ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, na kuita watu huko. Na usijali ushindani wa washirikina na madai yao ya urongo. info
التفاسير:

external-link copy
107 : 6

وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَآ أَشۡرَكُواْۗ وَمَا جَعَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗاۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِوَكِيلٖ

Na lau Mwenyezi Mungu Alitaka wasishirikishe hawa washirikina hawangalishirikisha, lakini Yeye, Aliyetukuka, ni Mjuzi wa yatakayokuwa ya ubaya wa uchaguzi wao na kufuata kwao matamanio yaliyopotoka. Na hatukukufanya wewe ni mchunguzi wa kuwatunzia matendo yao wala hukuwa ni msimamizi wao wa kuwapangia maslahi yao. info
التفاسير:

external-link copy
108 : 6

وَلَا تَسُبُّواْ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ فَيَسُبُّواْ ٱللَّهَ عَدۡوَۢا بِغَيۡرِ عِلۡمٖۗ كَذَٰلِكَ زَيَّنَّا لِكُلِّ أُمَّةٍ عَمَلَهُمۡ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّهِم مَّرۡجِعُهُمۡ فَيُنَبِّئُهُم بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Na msiyatukane, enyi Waislamu, masanamu ambyo washirikina wanayaabudu, kwa ajili ya kuziba kipengele, ili hilo lisije likawafanya wao wamtukane Mwenyezi Mungu kwa ujinga na kwa uadui, bila ya kuwa na ujuzi. Na kama tulivyowapambia hawa matendo yao mabaya, yakiwa ni mateso kwao kwa uchaguzi wao mbaya, ndivyo tulivyowapambia kila umma matendo yao. Kisha marejeo yao wote ni kwa Mola wao; hapo Mwenyezi Mungu Awaambie matendo yao waliokuwa wakiyatenda ulimwenguni kisha Awalipe kwayo. info
التفاسير:

external-link copy
109 : 6

وَأَقۡسَمُواْ بِٱللَّهِ جَهۡدَ أَيۡمَٰنِهِمۡ لَئِن جَآءَتۡهُمۡ ءَايَةٞ لَّيُؤۡمِنُنَّ بِهَاۚ قُلۡ إِنَّمَا ٱلۡأٓيَٰتُ عِندَ ٱللَّهِۖ وَمَا يُشۡعِرُكُمۡ أَنَّهَآ إِذَا جَآءَتۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Na waliapa washirikina hawa viyapo vya mkazo, «Lau Atatujia Muhammad kwa alama yenye miujiza, tutayaamini yale aliyoyaleta.» Sema, ewe Mtume, «Kuja kwa miujiza yenye kushinda kunatokana na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Yeye Ndiye Mwenye uwezo wa kuileta Akitaka.» Na nilipi liwajulishalo nyinyi, enyi Waumini: huenda miujiza hii ikija hawataiamini hawa washirikina?.» info
التفاسير:

external-link copy
110 : 6

وَنُقَلِّبُ أَفۡـِٔدَتَهُمۡ وَأَبۡصَٰرَهُمۡ كَمَا لَمۡ يُؤۡمِنُواْ بِهِۦٓ أَوَّلَ مَرَّةٖ وَنَذَرُهُمۡ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

Na tutazigeuza nyoyo zao na macho yao, tuweke kizuizi baina yake na kunufaika na alama za Mwenyezi mungu, wasiziamini kama walivyokuwa hawakuziamini aya za Qur’ani zilipoteremka kwa mara ya kwanza, na tutawaacha wao wameduwaa katika kumuasi kwao Mwenyezi Mungu, hawaongoki kwenye haki na usawa. info
التفاسير: