Na baada ya hawa Manabii tulimtuma Isa mwana wa Maryamu, naye ni mwenye kufuata njia yao, na kuithibitisha Taurati iliyo mtangulia. Naye tulimteremshia Injili yenye uwongofu kuelekea Haki, na yenye kubainisha hukumu, na tuliiteremsha ili isadikishe Taurati iliyo tangulia, na ndani yake pana uwongofu wa kupelekea Haki, na ni mawaidha kwa wachamngu. (Tazama Injili ya Mathayo 5.17 maneno ya Nabii Isa: "Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.")