د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - عبد الله محمد او ناصر خمیس

د مخ نمبر:close

external-link copy
60 : 23

وَٱلَّذِينَ يُؤۡتُونَ مَآ ءَاتَواْ وَّقُلُوبُهُمۡ وَجِلَةٌ أَنَّهُمۡ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ رَٰجِعُونَ

Na wale wanaojibidiisha kufanya matendo ya kheri na wema, mioyo yao ina kicho cha kuogopa yasikubaliwe matendo yao na yasiwaokoe na adhabu ya Mola wao warejeapo Kwake kwa kuhesabiwa. info
التفاسير:

external-link copy
61 : 23

أُوْلَٰٓئِكَ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِ وَهُمۡ لَهَا سَٰبِقُونَ

Hao wanaojibidiisha kutii, dasturi yao ni kukimbilia kufanya kila kitendo chema, na wao kwa kuyaendea mambo mema ni wenye kutangulia. info
التفاسير:

external-link copy
62 : 23

وَلَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ وَلَدَيۡنَا كِتَٰبٞ يَنطِقُ بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Hatumlazimishi mja yoyote miongoni mwa waja wetu isipokuwa kile kinachomkunjukia kukifanya, na matendo yao yamesajiliwa kwetu ndani ya Kitabu cha kudhibiti matendo, ambacho Malaika watakiinua, kitakachosema ukweli juu yao, na hakuna yoyote kati yao Atakayedhulumiwa. info
التفاسير:

external-link copy
63 : 23

بَلۡ قُلُوبُهُمۡ فِي غَمۡرَةٖ مِّنۡ هَٰذَا وَلَهُمۡ أَعۡمَٰلٞ مِّن دُونِ ذَٰلِكَ هُمۡ لَهَا عَٰمِلُونَ

Lakini nyoyo za makafiri ziko kwenye upotevu uliowafinika, zimejiepusha na Qur’ani na yaliyomo ndani yake. Na wao, pamoja na ushirikina wao, wana matendo mabaya, Mwenyezi Mungu Anawapa muhula wayafanye, ili ziwapate wao hasira za Mwenyezi Mungu na mateso Yake. info
التفاسير:

external-link copy
64 : 23

حَتَّىٰٓ إِذَآ أَخَذۡنَا مُتۡرَفِيهِم بِٱلۡعَذَابِ إِذَا هُمۡ يَجۡـَٔرُونَ

Mpaka tutakapowashika wenye gogi na kiburi miongoni mwao kwa adhabu yetu, hapo ndipo watainua sauti zao wakinyenyekea na wakiomba waokolewe. info
التفاسير:

external-link copy
65 : 23

لَا تَجۡـَٔرُواْ ٱلۡيَوۡمَۖ إِنَّكُم مِّنَّا لَا تُنصَرُونَ

Na hapo waambiwe, «Msipige kelele wala msiombe kuokolewa leo! Nyinyi hamuwezi kuziokoa nafsi zenu, na hakuna yoyote atakayewaokoa na adhabu ya Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
66 : 23

قَدۡ كَانَتۡ ءَايَٰتِي تُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فَكُنتُمۡ عَلَىٰٓ أَعۡقَٰبِكُمۡ تَنكِصُونَ

«Zilikuwa aya za Qur’ani zikisomwa kwenu, ili mupate kuziamini, na mlikuwa mnazikimbia hamtaki kuzisikia na kuzikubali na kuzitumia, kama anavyofanya mwenye kurudi nyuma kwa kule kurudi kwake nyuma. info
التفاسير:

external-link copy
67 : 23

مُسۡتَكۡبِرِينَ بِهِۦ سَٰمِرٗا تَهۡجُرُونَ

«Mnalifanya hilo na huku mnawaonesha watu kiburi pasi na haki kwa sababu ya Nyumba ya Mwenyezi Mungu tukufu. Mnasema, ‘Sisi ni watu wa Nyumba hiyo, hatushindwi tukiwa hapo,’ na mnakesha mkiwa kando-kando yake kwa maneno maovu.» info
التفاسير:

external-link copy
68 : 23

أَفَلَمۡ يَدَّبَّرُواْ ٱلۡقَوۡلَ أَمۡ جَآءَهُم مَّا لَمۡ يَأۡتِ ءَابَآءَهُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kwani hawayafikirii yaliyomo ndani ya Qur’ani wakapata kujua ukweli wake au limewazuia wao kuamini kwa kuwa wamejiwa na Mtume na kitabu ambacho mfano wake hakikuwajia baba zao wa mwanzo, wakakikanusha kwa ajili hiyo na wakakipa mgongo? info
التفاسير:

external-link copy
69 : 23

أَمۡ لَمۡ يَعۡرِفُواْ رَسُولَهُمۡ فَهُمۡ لَهُۥ مُنكِرُونَ

Au limewazuia wao kuifuata haki kwa kuwa Mtume wao, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hajulikani kwao na kwa hivyo wanamkataa? info
التفاسير:

external-link copy
70 : 23

أَمۡ يَقُولُونَ بِهِۦ جِنَّةُۢۚ بَلۡ جَآءَهُم بِٱلۡحَقِّ وَأَكۡثَرُهُمۡ لِلۡحَقِّ كَٰرِهُونَ

Au wanamdhania kuwa ni mwendawazimu? Kwa hakika wamedanganya. Ukweli ni kuwa amewajia na Qur’ani, upwekeshaji Mwenyezi Mungu na dini ya kweli. Na wengi wao wanaichukia haki kwa uhasidi na uadui. info
التفاسير:

external-link copy
71 : 23

وَلَوِ ٱتَّبَعَ ٱلۡحَقُّ أَهۡوَآءَهُمۡ لَفَسَدَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَن فِيهِنَّۚ بَلۡ أَتَيۡنَٰهُم بِذِكۡرِهِمۡ فَهُمۡ عَن ذِكۡرِهِم مُّعۡرِضُونَ

Lau kama Mwenyezi Mungu Angaliwawekea sheria inayolingana na mapendeleo yao, zingaliharibika mbingu na ardhi na vilivyomo humo. Bali tumewaletea yale ambayo ndani yake muna alama za nguvu yao na utukufu wao, nayo ni Qur’ani, na wao wanaipa mgongo. info
التفاسير:

external-link copy
72 : 23

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ خَرۡجٗا فَخَرَاجُ رَبِّكَ خَيۡرٞۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلرَّٰزِقِينَ

Au limewazuia wao kukuamini kwa kuwa wewe, ewe Mtume, unawaomba malipo juu ya ulinganizi wako kwao, hivyo basi wakafanya ubahili? Hukufanya hivyo, kwa kuwa zile thawabu zilizoko kwa Mwenyezi Mungu na vipewa ni bora zaidi. Na Yeye ni bora wa wanaoruzuku, hakuna awezaye kuruzuku kama Yeye Anavyoruzuku, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake. info
التفاسير:

external-link copy
73 : 23

وَإِنَّكَ لَتَدۡعُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Kwa hakika wewe, ewe Mtume, unawalingania watu wako na wengineo kwenye Dini iliyolingana sawa, nayo ni Dini ya Uislamu. info
التفاسير:

external-link copy
74 : 23

وَإِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ عَنِ ٱلصِّرَٰطِ لَنَٰكِبُونَ

Na kwa hakika, wale ambao hawaamini kufufuliwa na kuhesabiwa wala hawayafanyii kazi hayo mawili, basi hao wamepotoka kando ya njia ya Dini iliyonyoka, nayo ni dini ya Uislamu. info
التفاسير: