ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫

ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ:close

external-link copy
68 : 25

وَٱلَّذِينَ لَا يَدۡعُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ وَلَا يَقۡتُلُونَ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَا يَزۡنُونَۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ يَلۡقَ أَثَامٗا

Na ambao wanampwekesha Mwenyezi Mungu na hawamuombi wala kumuabudu mola asiyekuwa Yeye, wala hawaiui nafsi ambayo Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuawa isipokuwa kwa kitu kinachopasisha kuuawa, kama vile kukufuru baada ya kuamini au kuzini baada ya ndoa au kumuua mtu kwa uadui, wala hawazini bali wanazihifadhi tupu zao isipokuwa kwa wake zao au wale ambao mikono yao ya kulia imemiliki. Na mwenye kuyafanya madhambi haya makubwa atakuta mateso huko Akhera. info
التفاسير:

external-link copy
69 : 25

يُضَٰعَفۡ لَهُ ٱلۡعَذَابُ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَيَخۡلُدۡ فِيهِۦ مُهَانًا

Ataongezewa adhabu maradufu Siku ya Kiyama na ataketi milele akiwa mdhalilifu mnyonge. Onyo la kukaa milele ni kwa wale wanaoyafanya yote hayo au ni kwa yule aliyemshirikisha Mwenyezi Mungu. info
التفاسير:

external-link copy
70 : 25

إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ عَمَلٗا صَٰلِحٗا فَأُوْلَٰٓئِكَ يُبَدِّلُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِهِمۡ حَسَنَٰتٖۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Lakini mwenye kutubia kutokana na madhambi haya toba ya dhati na akaamini imani ya kukata yenye kuambatana na matendo mema, basi hao Mwenyezi Mungu Atawafutia makosa yao na Atawaweka mahali Pake mema, kwa sababu ya kutubia kwao na kujuta kwao. Na kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe kwa anayetubia, ni Mwingi wa rehema kwa waja Wake kwa kuwa Amewaita watubie baada ya kushindana na Yeye kwa kufanya maasia makubwa kabisa. info
التفاسير:

external-link copy
71 : 25

وَمَن تَابَ وَعَمِلَ صَٰلِحٗا فَإِنَّهُۥ يَتُوبُ إِلَى ٱللَّهِ مَتَابٗا

Na yoyote anayetubia kwa madhambi aliyoyafanya na akafanya matendo mema, basi yeye, kwa hilo, atakuwa amerudi kwa Mwenyezi Mungu kisawasawa, na hapo Mwenyezi Mungu Ataikubali toba yake na Atazifuta dhambi zake. info
التفاسير:

external-link copy
72 : 25

وَٱلَّذِينَ لَا يَشۡهَدُونَ ٱلزُّورَ وَإِذَا مَرُّواْ بِٱللَّغۡوِ مَرُّواْ كِرَامٗا

Na ambao hawatoi ushahidi wa urongo wala hawahudhurii vikao vyake, na wapitapo kwa watu wa ubatilifu na ulaghai bila ya kukusudia wanapita hali ya kupa mgongo na kupinga, wanajiepusha nao (huo ubatilifu na ulaghai) na hawauridhii kwa wengine. info
التفاسير:

external-link copy
73 : 25

وَٱلَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُواْ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ لَمۡ يَخِرُّواْ عَلَيۡهَا صُمّٗا وَعُمۡيَانٗا

Na ambao wakipewa mawaidha kwa aya za Qur’ani na dalili za upweke wa Mwenyezi Mungu hawajighafilishi nazo wakawa kama ambao ni viziwi hawakuzisikia na vipofu hawakuziona, lakini nyoyo zao zinazielewa na akili zao zinafunguka kuzikubali, na basi hapo wanajipomosha kwa Mwenyezi Mungu hali ya kusujudu na kutii. info
التفاسير:

external-link copy
74 : 25

وَٱلَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا هَبۡ لَنَا مِنۡ أَزۡوَٰجِنَا وَذُرِّيَّٰتِنَا قُرَّةَ أَعۡيُنٖ وَٱجۡعَلۡنَا لِلۡمُتَّقِينَ إِمَامًا

Na ambao wanamuomba Mwenyezi Mungu Aliyetukuka wakisema, «Mola wetu! Tutunukie miongoni mwa wake zetu na wana wetu cha kutuliza macho yetu na chenye maliwazo na furaha kwetu, na utufanye ni kiigizo chema kwa wachamungu kutuiga.» info
التفاسير:

external-link copy
75 : 25

أُوْلَٰٓئِكَ يُجۡزَوۡنَ ٱلۡغُرۡفَةَ بِمَا صَبَرُواْ وَيُلَقَّوۡنَ فِيهَا تَحِيَّةٗ وَسَلَٰمًا

Hao waja wa Mwingi wa rehema, waliosifika kwa sifa zilizopita, watalipwa majumba ya Peponi ya juu kabisa, kwa rehema ya Mwenyezi Mungu na kwa sababu ya uvumilivu wao juu ya kufanya matendo ya utiifu, na watalakiwa humo Peponi kwa maamkizi na salamu kutoka kwa Malaika, na watakuta maisha mema na kusalimika na maafa, info
التفاسير:

external-link copy
76 : 25

خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ حَسُنَتۡ مُسۡتَقَرّٗا وَمُقَامٗا

hali ya kukaa milele humo bila ya kufa. Ni nzuri mno hiyo Pepo kuwa ni mahali pa wao kutulia na makao ya wao kukaa, hawatataka kuondoka hapo. info
التفاسير:

external-link copy
77 : 25

قُلۡ مَا يَعۡبَؤُاْ بِكُمۡ رَبِّي لَوۡلَا دُعَآؤُكُمۡۖ فَقَدۡ كَذَّبۡتُمۡ فَسَوۡفَ يَكُونُ لِزَامَۢا

Mwenyezi Mungu Anatoa habari kuwa Yeye hawajali watu wala hashughuliki nao lau si wao kumlingania Yeye ulinganizi wa ibada na ulinganizi wa maombi. Hakika yenu nyinyi, enyi makafiri, mumekanusha, na ukanushaji wenu utapelekea mupate adhabu yenye kuwa na nyinyi kama vile mwenye kudai anavyokuwa na mdaiwa wake, na Atawaangamiza duniani na Akhera. info
التفاسير: