ߞߎ߬ߙߣߊ߬ ߞߟߊߒߞߋ ߞߘߐ ߟߎ߬ ߘߟߊߡߌߘߊ - ߛߊߥߊ߯ߤߟߌߞߊ߲ ߘߟߊߡߌ߬ߘߊ - ߊ߳ߺߓߑߘߎ-ߟߟߊ߯ߤߌ߫ ߡߎ߬ߤߊߡߡߊߘߎ߫ ߣߌ߫ ߣߊ߯ߛ߫ߌߙߎ߫ ߞ߭ߊ߬ߡߌ߯ߛߎ߫ ߓߟߏ߫

ߞߐߜߍ ߝߙߍߕߍ:close

external-link copy
44 : 25

أَمۡ تَحۡسَبُ أَنَّ أَكۡثَرَهُمۡ يَسۡمَعُونَ أَوۡ يَعۡقِلُونَۚ إِنۡ هُمۡ إِلَّا كَٱلۡأَنۡعَٰمِ بَلۡ هُمۡ أَضَلُّ سَبِيلًا

Au unadhani kwamba wengi wao wanazisikia aya za Mwenyezi Mungu, kusikia kwa kuzingatia, au wanayaelewa yaliyomo ndani yake? Hawakuwa isipokuwa ni kama wanyama, katika kutonufaika kwa wanayoyasikia, bali wao wamepotea njia zaidi kuliko hao wanyama. info
التفاسير:

external-link copy
45 : 25

أَلَمۡ تَرَ إِلَىٰ رَبِّكَ كَيۡفَ مَدَّ ٱلظِّلَّ وَلَوۡ شَآءَ لَجَعَلَهُۥ سَاكِنٗا ثُمَّ جَعَلۡنَا ٱلشَّمۡسَ عَلَيۡهِ دَلِيلٗا

Kwani huoni vipi Mwenyezi Mungu Alivyokinyosha kivuli kuanzia kutokea alfajiri mpaka kutokea jua? Na lau Mwenyezi Mungu Alitaka Angalikifanya kisimame na kitulie, kisiondolewe na jua kisha tungalilifanya jua kuwa ni alama ambayo kwa hali zake inachukuliwa dalili ya hali za kivuli. info
التفاسير:

external-link copy
46 : 25

ثُمَّ قَبَضۡنَٰهُ إِلَيۡنَا قَبۡضٗا يَسِيرٗا

Kisha kivuli kinapotea kidogo- kidogo, kila kunapoongezeka kupaa juu kwa jua ndipo kunapoongezeka kupungua kwake. Hilo ni miongoni mwa dalili za uweza wa Mwenyezi Mungu, ukubwa Wake na kwamba Yeye Peke Yake Ndiye Anayestahiki kuabudiwa, si mwengine. info
التفاسير:

external-link copy
47 : 25

وَهُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا وَٱلنَّوۡمَ سُبَاتٗا وَجَعَلَ ٱلنَّهَارَ نُشُورٗا

Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ndiye Aliyewawekea usiku kuwa ni wenye kuwasitiri nyinyi kwa giza lake, kama vile mavazi yanavyowasitiri. Na Amewawekea usingizi kuwa ni raha ya miili yenu, ndani yake mnatulia na mnapumzika. Na Amewawekea mchana ili mtapakae kwenye ardhi na mtafute maisha yenu. info
التفاسير:

external-link copy
48 : 25

وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ ٱلرِّيَٰحَ بُشۡرَۢا بَيۡنَ يَدَيۡ رَحۡمَتِهِۦۚ وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ طَهُورٗا

Na Yeye Ndiye Aliyezituma pepo zinazobeba mawingu, zenye kuwabashiria watu mvua ikiwa ni rehema kutoka Kwake; na tumeyateremsha kutoka mbinguni maji ya kujisafisha nayo, info
التفاسير:

external-link copy
49 : 25

لِّنُحۡـِۧيَ بِهِۦ بَلۡدَةٗ مَّيۡتٗا وَنُسۡقِيَهُۥ مِمَّا خَلَقۡنَآ أَنۡعَٰمٗا وَأَنَاسِيَّ كَثِيرٗا

ili tutoe kwayo mimea mahali pasipo na mimea, ipate kuhuika ardhi ya ukame baada ya kuwa imekufa (kwa ukavu), na ili tuwanyweshe maji hayo wanyama howa na watu miongoni mwa viumbe vyetu vyingi. info
التفاسير:

external-link copy
50 : 25

وَلَقَدۡ صَرَّفۡنَٰهُ بَيۡنَهُمۡ لِيَذَّكَّرُواْ فَأَبَىٰٓ أَكۡثَرُ ٱلنَّاسِ إِلَّا كُفُورٗا

Na hakika tunateremsha mvua juu ya sehemu ya ardhi bila ya nyingine, ili wale walioteremshiwa mvua wapate kukumbuka neema ya Mwenyezi Mungu juu yao na wamshukuru, na ili wale walionyimwa mvua wafanye haraka kutubia kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Apate kuwarehemu wao na kuwanywesha. Lakini wengi wa watu wanakataa isipokuwa ni kukanusha neema zetu juu yao, kama neno lao wanalolisema, «tumeletewa mvua kwa sababu ya nyota kadha na kadha.» info
التفاسير:

external-link copy
51 : 25

وَلَوۡ شِئۡنَا لَبَعَثۡنَا فِي كُلِّ قَرۡيَةٖ نَّذِيرٗا

Na lau tungalitaka tungalimpeleka muonyaji katika kila mji, wa kuwalingania wao kwa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, na kuwaonya wao adhabu Yake. Lakini tumekufanya wewe, ewe Mtume, ni mwenye kupelekwa kwa watu wote wa ardhini, na tumekuamrisha wewe uwafikishie hii Qur’ani. info
التفاسير:

external-link copy
52 : 25

فَلَا تُطِعِ ٱلۡكَٰفِرِينَ وَجَٰهِدۡهُم بِهِۦ جِهَادٗا كَبِيرٗا

Basi usiwatii makafiri kwa kuacha kitu chochote kile ambacho umetumilizwa nacho. Lakini fanya bidii yako katika kuufikisha ujumbe na upigane jihadi na wenye kuikanusha hii Qur’ani, kupigana jihadi kukubwa kusikochanganyika na udhaifu. info
التفاسير:

external-link copy
53 : 25

۞ وَهُوَ ٱلَّذِي مَرَجَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ هَٰذَا عَذۡبٞ فُرَاتٞ وَهَٰذَا مِلۡحٌ أُجَاجٞ وَجَعَلَ بَيۡنَهُمَا بَرۡزَخٗا وَحِجۡرٗا مَّحۡجُورٗا

Na Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyezichanganya bahari mbili: ya tamu yenye ladha nzuri, na ya chumvi yenye uchumvi mwingi, na Akaweka baina ya hizo mbili kizuizi chenye kuzuia kila mojawapo ya hizo isiiharibu nyingine na pingamizi ili mojawapo isiifikie nyingine. info
التفاسير:

external-link copy
54 : 25

وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ مِنَ ٱلۡمَآءِ بَشَرٗا فَجَعَلَهُۥ نَسَبٗا وَصِهۡرٗاۗ وَكَانَ رَبُّكَ قَدِيرٗا

Na Yeye Ndiye Aliyeumba kizazi cha kiume na kike kutokamana na manii ya mwanamume, na kutokana na hayo ukapatikana ujamaa wa kinasaba na ujamaa wa ukwe. Na Mola wako ni Mwenye uweza wa kuumba Anachotaka. info
التفاسير:

external-link copy
55 : 25

وَيَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَنفَعُهُمۡ وَلَا يَضُرُّهُمۡۗ وَكَانَ ٱلۡكَافِرُ عَلَىٰ رَبِّهِۦ ظَهِيرٗا

Na pamoja na dalili hizi za uweza wa Mwenyezi Mungu na wema Wake kwa viumbe Wake, makafiri wanaabudu, badala ya Mwenyezi Mungu, kitu ambacho hakiwanufaishi wakikiabudu wala hakiwadhuru wakiacha kukiabudu. Na kafiri ni msaidizi wa Shetani juu ya Mola wake, kwa kufanya ushirikina katika ibada ya Mwenyezi Mungu, na ni mwenye kumpa nguvu huyo Shetani juu kumuasi Mwenyezi Mungu. info
التفاسير: